Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/01 uku. 3-4
  • Adabu Nzuri—Sifa Yenye Kutofautisha Watu wa Mungu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Adabu Nzuri—Sifa Yenye Kutofautisha Watu wa Mungu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ni Lazima Kabisa Kuwa na Adabu?
    Vijana Wanauliza
  • Tuwe Vielelezo Katika Usemi Na Katika Mwenendo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Wazazi—Toeni mfano mzuri kwa watoto wenu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Wafundishe Watoto Wako Kuonyesha Heshima
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 8/01 uku. 3-4

Adabu Nzuri​​—Sifa Yenye Kutofautisha Watu wa Mungu

1 Adabu nzuri hazipatikani sana leo. Kwa nini hivyo? Watu wako haraka sana hivi kwamba wanafikiri mara chache sana kuhusu tabia nzuri za msingi, kama vile kusema “Tafadhali,” “Asante,” au “Nisamehe.” Neno la Mungu lilitabiri kuharibika kwa adabu katika siku za mwisho wakati liliposema kwamba watu wangekuwa ‘wenye kujipenda wenyewe, wenye kujitanguliza, wenye kiburi, wasio na shukrani, wasio na shauku ya kiasili, wasiojizuiza, wasio na upendo wa mema, wenye kichwa kigumu.’ (2 Tim. 3:​1-4) Tabia hizo zote ni ukosefu wa adabu nzuri. Wakiwa watu wa Mungu, Wakristo wanapaswa kuwa waangalifu ili wasiwe na ukosefu wa adabu wa ulimwengu kuelekea wengine.

2 Adabu Ni Nini? Adabu nzuri zinaweza kufafanuliwa kuwa hali ya kujua sana jinsi wengine wanavyohisi, uwezo wa kuishi na wengine kwa amani. Adabu nzuri zinatia ndani kufikiria wengine, heshima, wema, kujua mambo ya kufanya au kusema ili kuendeleza uhusiano mzuri, na kutambua kimbele na kutenda kulingana na mahitaji ya wengine. Msingi wa tabia hizo ni upendo wa mtu kwa Yehova na kwa jirani. (Luka 10:27) Tabia hizo hazigharimu lolote, lakini ni za thamani sana katika kuboresha uhusiano wetu pamoja na wengine.

3 Yesu Kristo ndiye aliyetoa mfano mkamilifu. Alitenda sikuzote kulingana na ile Kanuni Bora: “Kama vile mtakavyo watu wawafanyie nyinyi, wafanyieni wao kwa njia hiyohiyo.” (Luka 6:​31) Je, hatushangazwi na ufikirio wa Yesu na tabia yake yenye upendo katika kushughulika na wanafunzi wake? (Mt. 11:​28-​30) Tabia zake nzuri hazikutokana na kanuni zilizoandikwa katika vitabu vyenye kuzungumzia adabu. Zilitoka katika moyo mnyofu na wenye ukarimu. Tunapaswa kujaribu kuiga mfano wake mwema.

4 Ni wakati gani Wakristo wanapohitaji adabu nzuri? Wakati wa matukio ya pekee tu, wanapohangaikia kuvutia wengine? Je, yanahitajiwa tu wakati wanapojaribu kuwa na uvutano juu ya wengine? Hapana! Tunapaswa kuonyesha adabu nzuri nyakati zote. Ni katika njia gani hasa tunapaswa kuhangaikia hilo katika kushirikiana kwetu na wengine katika kutaniko?

5 Kwenye Jumba la Ufalme: Jumba la Ufalme ndipo mahali petu pa ibada. Ni Yehova Mungu anayetualika tuje hapo. Katika maana hiyo, sisi ni wageni-waalikwa. (Zab. 15:1) Je, sisi ni wageni-waalikwa wenye kutoa mfano wa kuigwa wakati tunapokuja kwenye Jumba la Ufalme? Je, tunatoa uangalifu wenye kufaa kwa mavazi yetu na kujipamba kwetu? Bila shaka, tunapaswa kuepuka kujipamba kwa namna ya ovyoovyo au yenye kupita kiasi. Iwe kwamba wanahudhuria mikusanyiko au mikutano yetu ya kutaniko ya kila juma, watu wa Yehova wanajulikana kwa sababu ya hali yao ya nje yenye adabu na yenye kustahili wale wanaosema kwamba wanamheshimu Mungu. (1 Tim. 2:​9, 10) Hivyo, tunaonyesha ufikirio na heshima yenye kufaa kwa Mkaribishaji wetu wa mbinguni na kwa wageni wengine walioalikwa.

6 Njia nyingine ambayo katika hiyo tunaonyesha adabu nzuri kuhusiana na mikutano ni kwa kufika pa wakati. Ni kweli kwamba hilo si jambo jepesi sikuzote. Wengine huenda wakawa wenye kuishi mbali au huenda wakawa na familia kubwa za kutayarisha. Hata hivyo, imeonekana katika makutaniko fulani kwamba asilimia 75 ya wahubiri hufika kwa kawaida baada ya wimbo na sala ya kufungua. Hilo ni jambo zito. Tunapaswa kukumbuka kwamba adabu nzuri zinahusiana na kujua jinsi wengine wanavyohisi. Mkaribishaji wetu mwenye rehema, Yehova, amepanga karamu hizo za kiroho kwa faida yetu. Tunaonyesha uthamini na ufikirio wetu kuelekea hisia zake kwa kufika pa wakati. Kwa kuongezea, kuchelewa mikutano kunakengeusha fikira na kunaonyesha ukosefu wa heshima kuelekea wale ambao tayari wako katikati ya wasikilizaji.

7 Wakati tunapokusanyika, je, tunatambua wapya kati ya wasikilizaji? Kuwakaribisha ni njia moja ya kuwa wenye adabu nzuri. (Mt. 5:​47; Rom. 15:7) Salamu ya upole, kupeana mikono kwa shauku, ucheshi mwema​​—hayo yote ni mambo madogo-madogo, lakini ni sehemu ya yale yanayotutambulisha kuwa Wakristo wa kweli. (Yn. 13:35) Baada ya kuja kwenye Jumba la Ufalme kwa mara ya kwanza, mwanamume mmoja alisema: “Kwa siku moja, nilikutana na watu wenye upendo wa kweli​​—watu nisiowajua hata kidogo​​—wengi zaidi kuliko wale niliopata kukutana nao katika kanisa ambamo nilikomalia. Ilionekana kwamba nilikuwa nimepata kweli.” Kama tokeo, alibadili maisha yake, na miezi saba baadaye akabatizwa. Ndiyo, adabu nzuri zinaweza kuwa na uvutano wenye matokeo sana!

8  Ikiwa sisi ni wenye adabu kuelekea watu tusiowajua ambao tunakutana nao, je, haipaswi kuwa hivyo “hasa kuelekea wale ambao katika imani ni jamaa zetu”? (Gal. 6:​10) Kanuni ifuatayo inatumika: “Heshimu uso wa muzee [wa kike au wa kiume].” (Law. 19:32) Hao hawapaswi kamwe kupuuzwa kwenye mikusanyiko yetu.

9 Kusikiliza kwa Uangalifu Sana: Wakati wa mikutano ya kutaniko, Wakristo walio wahudumu wa Mungu husema ili kutoa zawadi fulani ya kiroho kwa ajili ya kutujenga. (Rom. 1:​11) Bila shaka, tutakuwa tukionyesha ukosefu mwingi wa adabu ikiwa tunasinzia-sinzia, ikiwa tunafanya makelele kwa kutafuna peremende, ikiwa tunazungumza-zungumza na mtu fulani anayekaa karibu nasi, ikiwa tunakwenda chooni mara nyingi isivyo lazima, ikiwa tunasoma habari zisizohusiana na mkutano, au ikiwa tunashughulika na mambo mengine muda wa mikutano. Wazee wanapaswa kutoa mfano katika mambo hayo. Adabu nzuri za Kikristo zitatuchochea tuonyeshe heshima yenye kufaa kuelekea msemaji na ujumbe wake wenye msingi juu ya Biblia kwa kumsikiliza kikamili.

10 Kwa kuongezea, ufikirio kuelekea msemaji na wasikilizaji unapaswa utuchochee tulinde vyombo vyetu vidogo-vidogo vya simu katika hali itakayofanya visivuruge mikutano yetu.

11 Adabu na Watoto: Wazazi wanapaswa sikuzote kuwa macho kuhusu mwenendo wa watoto wao. Ikiwa mtoto mdogo anaanza kulalamika au anakuwa asiyetulia muda wa mkutano na kwamba jambo hilo linavuruga wengine, ni vizuri kutoa mtoto huyo nje ya mahali wanapokaa wasikilizaji mapema zaidi iwezekanavyo ili kumtuliza. Nyakati nyingine hilo linaweza kuwa jambo gumu, lakini kumbukeni kwamba hilo linaonyesha ya kuwa tunajali hisia za wengine. Wazazi walio na watoto wadogo wanaoelekea kuwa wasiotulia mara nyingi huchagua kukaa sehemu za nyuma za mahali wanapokaa wasikilizaji kusudi wasivuruge wengine sana ikiwa wanalazimika kusimama-simama muda wa mkutano. Bila shaka, wasikilizaji wengine wanaweza kuonyesha ufikirio wenye kufaa kwa familia kwa kuacha mistari ya nyuma ikiwa wazi ili familia hizo ziitumie, ikiwa hiyo inatakiwa.

12 Wazazi wanapaswa pia kujua jinsi watoto wao wanavyojiendesha kabla na baada ya mikutano. Watoto hawapaswi kukimbia-kimbia ndani ya jengo, kwa kuwa hilo linaweza kutokeza misiba. Kwenda huku na huku nje ya Jumba la Ufalme ili kujifurahisha kunaweza kuwa na hatari pia, hasa jioni wakati ambapo haiwezekani kuona mbali. Kusema kwa sauti kubwa tunapokuwa nje kunaweza kuvuruga majirani na kuwafanya wawe na maoni mabaya juu ya ibada yetu. Wazazi wanaofanya jitihada yenye kuongozwa na dhamiri ili kuangalia watoto wao ndani na nje ya Jumba la Ufalme wanapaswa kusifiwa kwa kuwa jambo hilo huongeza uzuri wa kukaa kwetu pamoja kwa umoja.​​—Zab. 133:1.

13 Kwenye Funzo la Kitabu: Tunathamini ukaribishaji wa ndugu zetu wanaotoa nyumba zao kwa ajili ya mikutano ya kutaniko. Wakati tunapohudhuria, tunapaswa kuonyesha heshima na ufikirio kuelekea mali yao. Kabla ya kuingia, tunapaswa kupangusa viatu kwa uangalifu ili kuepuka kuchafua sakafu au zulia. Wazazi wanapaswa kuangalia watoto wao, wahakikishe kwamba wanakaa katika sehemu ya nyumba iliyotayarishwa kwa ajili ya funzo la kitabu. Ingawa huenda kikundi kikawa kidogo na hali ikawa ya vivi hivi kwa kiasi fulani, hatupaswi kujiruhusu kufanya kila kitu katika nyumba za wengine. Mzazi wa mtoto mdogo anapaswa kumshindikiza wakati anapolazimika kutumia choo. Zaidi ya hayo, kwa kuwa funzo la kitabu ni mkutano wa kutaniko, tunapaswa kuvaa kama tunavyovaa wakati tunapokwenda kwenye Jumba la Ufalme.

14 Adabu Nzuri Ni za Maana Sana: Kutenda kulingana na adabu za Kikristo kunafanya wengine wawe na maoni mazuri kuhusu huduma yetu, lakini pia kunaendeleza mahusiano mazuri na wengine. (2 Kor. 6:​3, 4, 6) Tukiwa waabudu wa Mungu mwenye furaha, linapaswa kuwa jambo la asili kwetu kuwa wenye ucheshi, wenye kupendeza, na hata kufanya mambo madogo-madogo na yenye wema yanayoletea wengine furaha. Tabia hizo zenye adabu zitapamba maisha zetu tukiwa watu wa Mungu.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine