MAISHA YA MUKRISTO
Tujiendeshe Muzuri Wakati Tuko Kwenye Mulango
Wakristo ni “tamasha kwa ulimwengu” (1Kor 4:9) kwa hiyo, haishangaze kama wenye nyumba fulani wanatuchungulia kwenye dirisha ao wanatusikiliza nyuma ya mulango. Pengine nyumba inaweza kuwa na camera ao microfone yenye kuwezesha mwenye nyumba kutuona, kutusikiliza, ao kurekodi sauti zetu. Tuone namna tunaweza kujiendesha wakati tuko kwenye mulango wa mutu.—2Kor 6:3.
MWENENDO WETU (Flp 1:27):
Tuheshimie mwenye nyumba kwa kuepuka kuchungulia ndani ya nyumba yake. Tusikule, tusikunywe, tusiongee ao kutuma ujumbe kwenye telefone wakati tunasimama kwenye mulango wa mutu
MANENO YETU (Efe 4:29):
Wakati tuko kwenye mulango, tusiseme jambo lenye hatungependa mwenye nyumba asikie. Wahubiri fulani wameamua kuacha kuzungumuza ili wakazie akili mambo yenye watasema kama mwenye nyumba anatokea