Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Tumia Broshua Habari Njema Inayotoka kwa Mungu! Ili Kuanzisha Funzo la Biblia Kwenye Mulango
Sababu Gani Ni Lazima Kufanya Hivyo: Ili kufanya watu kuwa wanafunzi, tunapaswa kuwafundisha Neno la Mungu. (Mat. 28:19, 20) Kila mumoja wetu anaweza kuwa mwalimu muzuri kama anatumia vyombo vyenye tumepewa. Broshua Habari Njema Inayotoka kwa Mungu! ilifanywa ili itusaidie kuwafundisha wengine kweli. Kwa hiyo, tunaweza kuitumia ili kuanzisha funzo la Biblia kwenye mulango wa mutu mwenye tunakutana mara ya kwanza.
Tumikisha Shauri Hili Katika Mwezi:
Umuambie Yehova katika sala kwamba unapenda kuongoza funzo. Umuombe pia ili akusaidie kuanzisha funzo la Biblia na kuwa mwalimu muzuri wa Biblia.—Fil. 2:13.
Katika ibada ya familia ao funzo la pekee, ujifunze muzuri sana namna ya kuanzisha mazungumuzo. Kufanya hivyo kutakusaidia kusema kwa usadikisho na kuanzisha funzo la Biblia kwenye mulango.