Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 5/02 uku. 1
  • Je, Unatumia Broshua Anataka ili Kuanzisha Mafunzo?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je, Unatumia Broshua Anataka ili Kuanzisha Mafunzo?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Namna ya Kutumia Broshua Habari Njema Inayotoka kwa Mungu!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Tutumie Broshua Mbalimbali Katika Mahubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Tumtegemee Yehova ili ‘Kufululiza Kukuza’
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Tutangaze Habari Njema Ya Ufalme Kwa Msaada Wa Broshua
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 5/02 uku. 1

Je, Unatumia Broshua Anataka ili Kuanzisha Mafunzo?

1 Ikiwa una mazungumzo, hata mafupi, ya Biblia pamoja na mtu mwenye kupendezwa, na ikiwa unazungumzia kwa ukawaida na kwa utaratibu habari fulani katika kimoja cha vichapo vinavyopendekezwa, je, unatambua kwamba unaongoza funzo la Biblia? Ndiyo, hilo ni kweli hata ikiwa funzo linafanyika mlangoni au kwa njia ya simu. Kwa nini usifanye jitihada ya pekee mnamo Mei na Juni ili kuanzisha funzo la namna hiyo ukitumia broshua Anataka?

2 Jitayarishe ili Kuwa na Mafanikio: Unapotolea mtu broshua Anataka, jua vizuri akilini kile unachotaka kuzungumzia. Ikiwa unafanya ziara ya kurudia, fikiria mazungumzo mliyokuwa nayo kwenye ziara ya kwanza. Jiulize: ‘Ni mafungu gani katika broshua ninayoweza kukazia ili kuendeleza mazungumzo yale na ambayo yanaweza kuongoza kwenye funzo la Biblia?’ Ikiwa unatembelea watu nyumba kwa nyumba, fikiria habari itakayovutia kijana, mzee, mwanamume, au mwanamke. Rudilia vichwa vya habari vinavyozungumziwa katika broshua, na uchague habari yenye kupendeza. Baada ya kuamua utoaji wa kutumia, fanya mazoezi mara nyingi. Huo ni mmoja wa funguo ili kupata mafanikio.

3 Nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2002 inatoa Mapendekezo manane kwa Ajili ya Kutoa Broshua Anataka. Kisanduku “Utoaji wa Moja kwa Moja” kinaonyesha jinsi ya kutumia broshua hiyo ili kuanzisha mafunzo. Unaweza kurekebisha pendekezo la kwanza na kulipatanisha na hali kama ifuatavyo:

◼ “Je, unajua kwamba kwa dakika chache tu unaweza kupata jibu kwa ulizo la maana la Biblia? Kwa mfano, sababu gani kuna dini nyingi sana ambazo zinasema kuwa ni za Kikristo? Je, umekwisha kujiuliza kuhusu jambo hilo?” Mtu akiisha kujibu, fungua somo la 13 na mzungumzie mafungu mawili ya kwanza. Kama wakati unaruhusu, soma na uzungumzie andiko moja au mawili. Kisha, soma ulizo la mwisho kwenye sehemu ya juu ya ukurasa, na useme: “Sehemu inayobaki ya somo hili inakazia alama tano zenye kutambulisha dini ya kweli. Nitakuwa mwenye furaha kurudi na kuchunguza hizo pamoja nawe.”

4 Uwe Mwenye Kudumu: Faidika na kila nafasi inayojitokeza ili kuonyesha jinsi funzo la Biblia linavyoendeshwa katika broshua Anataka. Omba baraka ya Yehova. (Mt. 21:​22) Kwa kudumu katika jitihada zako, unaweza kuonja furaha ya kusaidia mtu fulani aitikie habari njema!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine