Tutangaze Habari Njema Ya Ufalme Kwa Msaada Wa Broshua
1 Shangwe kama nini kujua ukweli na kupatikana katikati ya wahubiri wenye bidii wa habari njema! Watu wasiokuwa katika tengenezo la Mungu wasio na tumaini wana uhitaji wa kusikiliza habari njema ya Ufalme. Ukweli juu ya Ufalme unatolewa kwa urahisi katika broshua Kuishi Milele Duniani Katika Furaha! “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya” na Serikali Itakayoleta Paradiso. Zinaeleza uhai duniani chini ya utawala wa Ufalme wa Mungu kana kwamba tulikuwa ndani na, kwa mwangaza wa Neno lake, zinaongoza msomaji kwenye uhakika mbalimbali wa Ufalme. Kwa kawaida, kuacha broshua kwa mtu anayeonyesha kupendezwa ni mwanzo tu. (1 Kor. 9:23) Turudi haraka kuwaona watu wote waliokubali broshua, tukiwa na kusudi la kuwatolea funzo kwa msaada wa kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Jinsi gani kufanya hilo mwezi wa Septemba?
2 Broshua “Kuishi Milele Duniani Katika Furaha!” inaweza kutolewa kisha utangulizi mfupi sana. Angalia yale tunaweza kusema kwa kuonyesha jalada:
◼ “Ningependa kukuonyesha kitu fulani kilicho na ujumbe mzuri sana.” Tufungue broshua Kuishi Milele Katika Furaha na tusome fungu la kwanza la utangulizi. Tuendelee: “Broshua hii inajibu pia kwenye ulizo [tusome kichwa kidogo cha habari kinachopatikana juu ya picha Na. 8]: ‘Sababu Gani Mwanadamu Anakufa?’ Utaona kwamba ni jambo lenye kupendeza kuchunguza picha na kusoma maandiko yanayotolewa kwa kutajwa katika broshua hii. Ikiwa unataka, unaweza kulinda nakala hiyo.” Ikiwa mtu anakubali broshua, tuonyeshe mchango wa sasa na kwa nini tunauomba.
3 Tutasema nini tutakaporudi kumwona mtu aliyekubali broshua “Kuishi Milele Katika Furaha?” Tungeweza kujaribu utangulizi huu:
◼ Tuonyeshe picha Na. 49 ya broshua Kuishi Milele Katika Furaha na tuulize: “Ni picha nzuri, sivyo? [Tusikilize jibu.] Hii ni broshua ambayo nilikuachia wakati wa nyuma. Ningependa kukutolea ulizo lipatikanalo kwenye ukurasa ufuatao.” Tusome ulizo la picha Na. 50: “ ‘Je! unapenda kuishi milele katika paradiso hiyo nzuri?’ [Tuache mtu ajibu.] Ikiwa hiyo ndiyo hakika tamaa yako, angalia yale ungepaswa kufanya: ‘Ikiwa ndiyo, unapaswa kujifunza zaidi mambo hayo juu ya yale Mungu anayosema.’ [Tusome Yohana 17:3.] Nitafurahi kujifunza kwa bure Biblia pamoja nawe. Unafikiri nini juu ya hilo?” Tupange siku kamili ya kukutana.
4 Ikiwa tunatolea broshua “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya,” tungeweza kuanza kwa kuonyesha picha ya jalada kwa kuikunjua na kuuliza:
◼ “Kwa maoni yako, nini lingefanywa ili kwamba dunia yote ifanane hivi?” Tusikilize jibu. Tuonyeshe sehemu fulani za pekee za picha zinazoonyeshwa kwenye ukurasa wa 3. Tuendelee: “Watu walio wengi wanafikiri kwamba haiwezekani kubadili ulimwengu kufikia hali hii. Lakini kwa Mungu, si jambo lisilowezekana. [Tueleze fungu la 43; kisha tusome Isaya 9:6, 7.] Mungu aliahidi kusimamisha ulimwengu mpya, paradiso nzuri ambamo watu wa mataifa yote wataishi. Ningependa kwamba usome broshua hii. Itakuonyesha jinsi wewe na familia yako mnavyoweza kuona kwa msaada wa Mungu wakati ujao ulio wa ajabu.”
5 Wakati wa ziara ifuatayo, tungeweza, kwa kutumia broshua “Tazama!,” kufasiria kwa nini ni lazima kujua mengi zaidi juu ya Biblia. Ingetosha tu, kwa mfano, kuonyesha tena jalada na kusema:
◼ “Mara ya mwisho, nilipokuonyesha picha hii, tulikubaliana kwamba, wewe na mimi, tungependa kuishi katika ulimwengu nzuri kama huu. Kwa hiyo, ili hilo liwe hakika, kuna jambo fulani ambalo sote tunapaswa kufanya.” Tufungue broshua “Tazama!” na tusome fungu 52, na pia Yohana 17:3. Tuunganishe wazo hilo na kilinganisho cha fungu 53 kufuatana na elimu inayofaa ya Biblia, kisha tufasirie kwamba Mashahidi wa Yehova wanatolea elimu kama hiyo, kwa bure na nyumbani. Tupendekeze kumfanyia mtu onyesho moja la namna yetu ya kufundisha, kwa msaada wa kitabu Ujuzi.
6 Ikiwa tunatolea broshua “Serikali Itakayoleta Paradiso,” tungeweza kuanza hivi:
◼ “Ninasikia watu wengi wakisema kwamba wangependa kuishi chini ya serikali ambayo ingekuwa na uwezo—wa kwelikweli—wa kutatua matatizo makubwa. [Tutaje matatizo yanayogusa eneo lenu, kama vile ukosefu wa kazi, jeuri inayoongezeka au matumizi ya dawa za kulevya.] Kwa sababu ya hali hiyo, tunajiuliza wakati wetu ujao utakuwa nini na ule wa watu tuwapendao. Je! unafikiri kwamba serikali fulani itaweza siku moja kupata masuluhisho? [Tusikilize jibu.] Labda umekwisha kutaja sala ya Baba Yetu. Katika njia hiyo, je! unajua kwamba wakati uohuo ulikuwa ukiomba serikali ya haki?” Tufungue broshua Serikali kwenye ukurasa 3 na tusome mafungu ya kwanza mawili. Tutolee baadaye broshua.
7 Ikiwa tuliacha broshua “Serikali Itakayoleta Paradiso,” tungeweza kufungua mazungumzo wakati ujao kwa kusema:
◼ “Mara ya mwisho, tulizungumza juu ya ulazima wa serikali ya haki inayoweza kutatua matatizo ya jamii. Broshua ambayo nilikuachia inataja Ufalme wa Mungu kama tumaini letu pekee. Watu fulani wanajiuliza kile serikali hiyo inaweza kufanya ili kutengeneza hali yetu. Biblia inaonyesha kwamba Kristo amekwisha kuonyesha kwamba atafaulu pale ambapo viongozi wa kibinadamu wameshindwa.” Tufungue broshua Serikali kwenye ukurasa 29 na tusome mafungu manne ya mwisho mwisho. Tuongeze: “Ni wakati gani ujao mzuri ajabu, sivyo? Je! ungependa kuuona?” Tusikilize jibu. Tusome Yohana 17:3. Tumtie mtu moyo kujifunza mengi zaidi kwa msaada wa funzo la Biblia la nyumbani.
8 Ikiwa tunatolea broshua nyingine, tunaweza kutumia vielelezo vinavyotangulia ili kutayarisha matangulizi yetu wenyewe. Ikiwa inafaa, tufasirie kwa kifupi kwa msikilizaji wetu kwa nini tunamtolea broshua kwa kuomba mchango mdogo. Tujitayarishe kwa makini na tumwombe Yehova baraka yake huku tunapotangaza habari njema ya Ufalme.