Tumwige Yehova Kwa Kuhangaikia Kwelikweli Wengine
1 Yehova ni kielelezo bora cha yule anayehangaikia kwelikweli wengine. Yeye akiwa Mwenye Enzi kuu ya ulimwengu wote, ni mwenye huruma kwa mahitaji ya viumbe vyake vya kibinadamu. (1 Pt. 5:7) Yesu aliwatia moyo wanafunzi wake kuonyesha sifa za Baba yake, ambaye anachomoza jua na kunyesha mvua juu ya waadilifu na wasio waadilifu. (Mt. 5:45) Tunaweza kumwiga Yehova kwa kuonyesha kupendezwa kwa kweli kwa wengine, kwa kuwa wenye kujitayarisha kutangaza ujumbe wa Ufalme kwa kila mtu tunayekutana naye. Ikiwa tunafahamiana kikamilifu na broshua ambazo tutatumia katika huduma mnamo mwezi wa Agosti, tutakuwa tayari kutolea msaada wa kiroho kwa wengine. Madokezo yanayofuata yanatutolea mawazo fulani fulani juu ya namna ya kutayarisha mazungumzo ya kwanza baadaye kutunza kupendezwa kwa njia ya ziara za kurudia zifaazo.
2 Ikiwa tunatolea broshua “Je! Kweli Mungu Anatujali?” tunaweza kusema:
◼ “Je! umewahi kujiuliza kwa nini Mungu anaruhusu mateso, ikiwa kwelikweli anawajali wanadamu? [Tuache mtu ajibu.] Si kwamba tu broshua hii inatoa jibu lenye kuridhisha kwa ulizo hilo, lakini inaonyesha pia kwamba Mungu aliahidi kufutilia mbali maafa (mateso) yote ambayo mwanadamu alifanyia wanadamu wenzake na dunia.” Tusome fungu 23 kwenye ukurasa 27. Tuonyeshe picha inayopatikana chini na tusome Zaburi 145:16 inayotajwa kwenye fungu 22. Tutolee broshua. Ikiwa mtu anaikubali, tutokeze ulizo ambalo tutajibu wakati wa ziara ya kurudia ijayo, kwa mfano: “Je! ungependa kujua jinsi gani Mungu atatimiza kusudi lake la kutawanya baraka juu ya wanadamu na kuigeuza dunia kuwa Paradiso?”
3 Tunaporudi kuwaona wale ambao tuliachia broshua “Je! Kweli Mungu Anatujali?” tunaweza kuanzisha mazungumzo ya pili kwa namna ifuatayo:
◼ “Mara ya mwisho nilipopita, tuliona kwamba Mungu anatujali kwelikweli na kwamba ana kusudi la kufutilia mbali maafa yote ambayo mwanadamu alifanyia wanadamu wenzake na dunia.” Tufungue broshua kwenye kurasa 2 na 3, ambapo tunakuta picha, na tuendelee: “Tuliachana kwa ulizo hili: jinsi gani Mungu atatimiza kusudi lake la kutawanya baraka juu ya wanadamu na kuigeuza dunia kuwa Paradiso? Wewe unafikiri nini?” Baada ya kusikiliza jibu, tusome fungu la 2 kwenye ukurasa 17 na Danieli 2:44. Tusome baadaye fungu 12 kwenye ukurasa 18. Tumuulize msikilizaji wetu ikiwa angependa kuchunguza pamoja nasi sehemu ya 9 ya broshua. Ikiwa anakubali, tujifunze yenyewe pamoja naye.
4 Angalia utangulizi unaoweza kutusaidia ikiwa tunatolea broshua “Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa. . . ” Tuonyeshe jalada na tuseme:
◼ “Tunatolea leo broshua hii inayoleta faraja na tumaini kwa mamilioni ya watu waliopoteza mpendwa wao. Je! umewahi kujiuliza ni tumaini gani lililo kwa ajili ya wafu? [Tusikilize jibu.] Biblia inasema waziwazi kwamba Mungu aliahidi ufufuo.” Tusome Yohana 5:28, 29. Tufungue broshua na tueleze mafasirio ya fungu la mwisho kwenye ukurasa 28 na ya fungu lifuatalo kwenye ukurasa 31. Tuonyeshe picha zinazoyashindikiza. Tutolee broshua. Tunaweza kutayarisha uwanja kwa ajili ya ziara ya kurudia kwa kuuliza: “Jinsi gani tunaweza kuwa hakika kwamba hatimaye kifo kitaondolewa kabisa kabisa?”
5 Tutakaporudi kuwaona watu waliokubali broshua “Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa. . . ” tutapenda labda kusema:
◼ “Mara ya mwisho, tulizungumza juu ya tumaini la ajabu la ufufuo. Broshua niliyokuachia inafasiria kwa nini tunaweza kuwa hakika kwamba hatimaye kifo kitaondolewa kabisa kabisa. Je! hauoni kwamba ahadi hizo za Mungu zinatufariji na hututolea uhakika?” Tuache mtu ajibu. Kisha tufungue broshua kwenye ukurasa 31 na tusome fungu la pili na la tatu, na pia Ufunuo 21:1-4. Tia mkazo juu tumaini tulilo nalo la kuishi bila kupatwa na kifo. Kulingana na kupendezwa ambako mtu anaonyesha na hali, tupendekeze funzo la Biblia kwa msingi wa kitabu Ujuzi au tuulize ulizo lingine ambalo litatoa mawazo kwa ajili ya ziara ijayo.
6 Angalia yale tungeweza kusema ikiwa tunatolea broshua “Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?—Wewe Waweza Kulipataje?”:
◼ “Watu wengi wanajiuliza ni nini kusudi la uhai. Wanasema: ‘Kwa nini mimi nipo hapa? Uhai unaongoza wapi? Wakati ujao unaniandalia nini?’ Kwa maoni yako, wapi tunaweza kupata majibu? [Tumsikilize mtu.] Angalia yale Biblia inayosema. [Tusome Zaburi 36:9.] Je! si jambo la akili kukubali kwamba Muumba wa mwanadamu ni yeye anayeweza kutufasiria vizuri zaidi kile tunachofanya hapa? [Tuache mtu ajibu.] Broshua hii inaonyesha kusudi kubwa ambalo Mungu alifanya kwa ajili yetu.” Tufungue broshua kwenye kurasa 20 na 21, tusome maandishi pembeni ya picha na tufasirie picha, kisha tupendekeze broshua. Ikiwa mtu anaikubali, tuulize: “Jinsi gani tunaweza kuwa hakika kwamba sikuzote Mungu ana mradi wa kwamba wanadamu waishi milele katika Paradiso duniani?” Tupange kuonana tena wakati ujao.
7 Ikiwa tuliacha broshua “Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?—Wewe Waweza Kulipataje?” tunaweza kusema, kwa mfano, wakati wa kupita kwetu kwa mara ya pili:
◼ “Mara ya mwisho nilipokuja, kwa kweli nilithamini mazungumzo yetu juu ya yale Biblia inayosema, yaani kwamba uhai kwa kweli una kusudi.” Tuonyeshe picha kwenye ukurasa 31 na tuulize: “Jinsi gani kuwa hakika kwamba mapenzi ya Mungu sikuzote ni kwamba wanadamu waishi milele katika Paradiso duniani?” Tusome fungu la 3 kwenye ukurasa 20. Tuzungumzie mawazo yanayoelezwa chini ya kichwa kidogo cha habari: “Kusudi la Mungu Linabaki Lisilobadilika,” ukurasa 21. Tusome nyuma ya broshua toleo linalohusu funzo la Biblia la bure la nyumbani. Tutolee kitabu Ujuzi na tupendekeze kwa mtu kumwonyesha jinsi tunavyotumia kitabu hicho ili kujifunza Biblia.
8 Huduma yetu ingepaswa kuonyesha hangaiko letu la kweli la kuwasaidia watu wenye moyo mnyofu ‘kufikia ujuzi sahihi wa kweli.’ (1 Tim. 2:4) Pia, tujiwekee wakati katika programu ya utendaji ili kurudi kuwaona wale wote ambao tuliachia broshua. Kwa kuwaonyesha kupendezwa kunyofu kwa namna hiyo, tutaweza labda kusaidia wale wanaougua na kulia kwa sababu ya mambo maovu yanayotendeka katika dini isiyo ya kweli ili kupokea alama kwa ajili ya wokovu. (Ezek. 9:4, 6) Tutapata pia shangwe na uradhi wa kujua kwamba tunamwiga Yehova kwa kuwahangaikia kwelikweli wengine.—Ona Wafilipi 2:20.