Majibu Kwa Maulizo Yenu
◼ Jinsi gani inafaa kutumia maneno “ndugu” na “dada”?
Katika maana halisi, maneno “ndugu” na “dada” yanamaanisha watu walio na wazazi wamoja. Uhusiano huo wa kiasili hutokana kwa ujumla na ushikamanifu wa kina kirefu; zaidi ya hilo, ukaribiano uliopo kati ya watu hao unatiwa nguvu na vifungo vyenye shauku na sababu ya kwamba wanatoka mahali pamoja kijamii na wana mazingira mamoja.
Yesu alifundisha wanafunzi wake kumwendea Yehova katika sala kwa kusema “Baba yetu.” Sisi tukiwa Wakristo tunatumia usemi huo; hivyo sisi sote ni sehemu kati ya familia moja ndani yayo tunafaidika na uhusiano bora mbalimbali wa kiroho. Ni yale Yesu aliweza kukazia aliposema kwa wanafunzi wake: “Nyinyi nyote ni akina ndugu.”— Mt. 6:9 ; 23:8, NW.
Tunafurahia uhusiano wa karibu wa kiroho katika nyumba ya Mungu na ni kwa sababu hiyo tunaitana “ndugu” na “dada,” hasa wakati wa mikutano ya kutaniko. Yule anayesimamia mkutano anawatambua watu wenye kubatizwa ambao anawatolea maulizo kwa kutanguliza jina lao [la familia] badala ya jina la kigeni, neno “ndugu” au “dada.” Kwa mfano: ndugu FULANI (Jacques), badala ya ndugu Jacques. Dada FULANI (Jacqueline), badala ya dada Jacqueline.
Nini la kufanya ikiwa mtu ambaye hajabatizwa anatamani kushiriki kwenye mikutano? Mtu anapokuwa karibu na kujiweka wakfu na anashirikiana na watu wa Mungu tangu wakati fulani, akijitambulisha kuwa Shahidi wa Yehova, hakuna kizuizi kwa sisi kutanguliza jina lake na neno “ndugu” au “dada.” Hilo ni halali kuelekea wale ambao wamekuwa wahubiri wasiobatizwa.
Kwa upande mwingine, watu wenye kupendezwa wanaohudhuria kwenye mikutano tangu tu wakati mfupi hawajafanya bado hatua zitakazowatambulisha kuwa washiriki wa nyumba ya Mungu. Hatutawaita “ndugu” au “dada,” kwani hawafaidike na uhusiano wa kiroho unaounganisha washiriki wa familia ya Mungu. Ni kwa sababu hiyo, wakati wa mikutano, tutajielekeza kwao kwa namna isiyo ya ukaribiano zaidi kwa kutanguliza jina lao [la familia] na “bwana,” kwa mfano.
Kwa kutumia maneno “ndugu” na “dada” wakati wa mikutano ya kutaniko, tunaonyesha kifungo chenye ukaribiano zaidi na kilicho bora badala ya kutumia tu majina ya kigeni (kwa mfano Jacques, Jacqueline). Hilo linatukumbusha kwamba tunafaidika na uhusiano wa pekee kati ya familia ya kiroho ambayo Baba ni Yehova Mungu. Tunakazia pia upendo wa kina kirefu na shauku tuliyo nayo wamoja kwa wengine.—Efe. 2:19 ; 1 Pt. 3:8.