Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 9/96 uku. 1
  • Tutangaze Bila Kuacha Habari Njema

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tutangaze Bila Kuacha Habari Njema
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Watasikia Namna Gani?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
  • Hubiri Bila Kuacha
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Ili Kufanya Wanafunzi, Tunapaswa Kuhubiri na Kufundisha
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2018
  • Kwa Mfano wa Yesu Tutangaze Kweli Kila Siku
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 9/96 uku. 1

Tutangaze Bila Kuacha Habari Njema

1 Wakristo wa kwanza walichukua huduma yao kwa uzito sana. Luka anaripoti: “Kila siku katika hekalu na katika nyumba kwa nyumba wakaendelea bila kuacha kufundisha na kutangaza ile habari njema juu ya yule Kristo, Yesu.” (Mdo. 5:​42, NW) Hakuna kitu kingeweza kuwazuia, wala hata mateso! (Mdo. 8:4) Walikuwa wakijulisha ukweli kila siku.

2 Namna gani sisi? Tujiulize: ‘Je! mimi ni mwenye kutambua uharaka wa nyakati? Je! mimi ni tayari kuendelea kutangaza bila kuacha habari njema?’

3 Wanahubiri Bila Kuacha: Dada mmoja aliyeshikwa na ugonjwa wa kupooza viungo alifungiliwa katika chombo cha chuma cha kupumulia. Lilikuwa jambo lisilowezekana kwake kujielekeza kwenye Jumba la Ufalme au kuhudhuria kwenye kusanyiko. Lakini alikuwa mwenye kushughulika sana kutangaza habari njema. Muda wa miaka 37 aliyopitisha ndani ya chombo hicho cha chuma cha kupumulia, alisaidia watu 17 kuujua ukweli! Alifikia hilo namna gani? Ingawa alikuwa asiyeweza kwenda nyumba kwa nyumba, alipata njia ya kutoa ushuhuda kwa namna ya vivi hivi kwa wale waliokuwa wakionana naye.

4 Ndugu zetu wa Bosnia waliweza kukabiliana na vita na ukosefu wa vitu vya kimwili. Wanaendelea hata hivyo kuhubiri. Katika Sarajevo, wahubiri wanapitisha kwa wastani saa 20 kwa mwezi wakisema juu ya habari njema, na kila mmoja anaongoza kwa wastani mafunzo mawili ya Biblia. Ijapokuwa hali yao ya magumu, wanahubiri na kufundisha bila kuacha.

5 Vijana pia ni wenye bidii kwa ajili ya huduma. Katika Rwanda, washiriki wa familia moja ya Mashahidi waliongozwa ndani ya chumba kimoja ambamo maaskari walikuwa wakijitayarisha kuwaua. Familia hiyo iliomba ruhusu ya kufanya kwanza sala. Waliwaruhusu, na msichana mdogo, Debora, alifanya sala kwa sauti kubwa: “Yehova, juma hili, Baba na mimi tuliangusha magazeti tano. Namna gani tutarudi kuwaona watu hao ili tuwafundishe ukweli na kuwasaidia kupata uzima?” Kwa msaada wa imani yake imara na upendo wake kwa ajili ya huduma, familia yote iliokolewa.

6 Katika siku zetu, ni lazima kuwa wenye makini kwa uwezekano wote mbalimbali wa kutoa ushuhuda na kutafuta wale walio katika “mwelekeo ufaao kwa ajili ya uhai udumuo milele.” (Mdo. 13:​48, NW) Huku wakifikiria hali ya mahali, wazee wanapanga mikutano kwa ajili ya mahubiri kwa nyakati zinazofaa kwa wote, iwe asubuhi, kisha-mchana au jioni. Makala ya Huduma Yetu ya Ufalme na pia vipindi vinavyotolewa wakati wa mkutano wa utumishi, makusanyiko ya mzunguko na ya wilaya ni nafasi mbalimbali za kupokea madokezo na vitia moyo kuhusu sehemu mbalimbali za mahubiri. Zaidi ya hilo, waangalizi wa mzunguko na wa wilaya wanazoeza wahubiri katika mahubiri barabarani, wanawaonyesha jinsi ya kuhubiri katika mtaa wa kibiashara na wanavutia uangalifu juu ya ufundi mwingine ili kutoa ushuhuda mahali ambapo watu wanapatikana. Yote hayo yanatukumbusha kwamba tunapaswa kutangaza bila kuacha habari njema.

7  Mitume wa Yesu walisema kwa uhodari: “Sisi hatuwezi kukoma kusema juu ya mambo ambayo tumeyaona na kuyasikia.” Jinsi gani walifikia kudumu ingawa vipingamizi vingi? Walitafuta msaada wa Yehova, na aliwatolea wenyewe, hivi kwamba “wote wakajazwa na roho takatifu na wakawa wakisema neno la Mungu kwa ujasiri.” (Mdo. 4:20, 29, 31, NW) Watu wote hawana furaha ya kuona mambo yaliyoonwa yenye kupendeza katika huduma, lakini ikiwa tunatamani hakika kutangaza bila kuacha habari njema na ikiwa tunajikaza kufanya hivyo kila siku, Yehova atatusaidia.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine