Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/96 uku. 1
  • Kwa Mfano wa Yesu Tutangaze Kweli Kila Siku

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kwa Mfano wa Yesu Tutangaze Kweli Kila Siku
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kuzidisha Ushahidi Kadiri Mwisho Unavyokaribia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Mashamba Ni Meupe kwa Ajili ya Kuvunwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Matokeo ya Kazi ya Kuhubiri: ‘Mashamba Yamekwisha Kuwa Meupe, Tayari kwa Mavuno’
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Shiriki Kikamili Katika Mavuno
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 3/96 uku. 1

Kwa Mfano wa Yesu Tutangaze Kweli Kila Siku

1 Yesu alipokuja duniani, alikuwa na kazi ya pekee ya kutimiza. Kazi hiyo ilikuwa ni: “Kutoa ushahidi kwa ile kweli.” (Yn. 18:37) Kweli aliyoitangaza ilihusiana na sifa za ajabu na pia makusudi ya Baba yake. Kazi hiyo ilikuwa kama chakula kwake; maisha yake yote yalitegemea kazi yake. (Yn. 4:34) Luka aliripoti kwamba Yesu ‘[alikuwa] akifundisha kila siku katika hekalu.’ (Luka 19:47) Yesu alitumia kikamilifu wakati aliokuwa nao. (Yn. 9:4) Muda mfupi kabla ya kifo chake, aliweza kumwambia Babaye : “Mimi nimekutukuza duniani, nikiwa nimemaliza ile kazi ambayo umenipa kufanya.”—Yn. 17:​4, NW.

2 Hivyo hivyo, ikiwa mioyo yetu inajaa na shukurani kwa ajili ya yale yote ambayo Yehova amefanya, tutajisikia kusukumwa kusema juu yake kila siku. Tutafikia hivyo kuwa kama wanafunzi wa Yesu waliosema kwa ujasiri: “Sisi hatuwezi kukoma kusema juu ya mambo ambayo tumeyaona na kuyasikia.” (Mdo. 4:​20, NW) Wao waliendelea kusema juu ya Yehova, kwa kuwa habari yahakikisha kwamba “kila siku...wakaendelea bila kuacha.” (Mdo. 5:​42, NW) Kila mmoja anapaswa kujiuliza: ‘Je! mimi ninamwiga Yesu Mfundishaji wangu?’

3 Tuhubiri Bila Kukawia: Yesu alitangaza kwamba ujumbe wa Ufalme utakapokuwa umehubiriwa duniani kote, “ndipo ule mwisho utakapokuja.” (Mat. 24:14) Jambo hilo lingepaswa kutusukuma kuona ulazima na uharaka wa kazi yetu. Tunapojua kwamba uhai wa mamilioni ya watu umo hatarini, hilo linatufanya tutambue kwamba hakuna jambo lililo la maana sana na pia la lazima sana kuliko kuhubiri. Kwa kuwa mfumo huu wa mambo unakaribia mwisho wao, kunabaki wakati mdogo ili kumaliza kazi hii.

4 Ripoti zaonyesha kwamba Yehova anaharakisha kukusanywa kwa watu walio mfano wa kondoo. (Isa. 60:22) Katika maeneo mengi ulimwenguni, watu wanamiminika kihalisi kuja kwenye kweli, wakisema: “Tutakwenda pamoja nanyi, kwa maana tumesikia ya kuwa Mungu ni pamoja nanyi.” (Zek. 8:23) Maneno ya Yesu ni yenye maana kubwa zaidi kuliko wakati alipoyasema: “Mavuno ni makubwa, lakini wafanya-kazi ni wachache. Kwa hiyo, ombeni Bwana-Mkubwa wa mavuno atume wafanya-kazi katika mavuno yake.” (Mat. 9:37, 38, NW) Je! jambo hilo halitutie moyo kuonyesha bidii, kama wale wanafunzi wa Yesu ambao “kwa kuendelea walikuwa katika hekalu wakimbariki Mungu?”—Lk. 24:53.

5 Tujulishe Kweli Kila Siku: Tungepaswa kufikiri kila siku juu ya namna tunavyoweza kujulisha ile kweli kwa wengine. Nafasi za kufanya hivyo hazikosekani. Je! tunaweza kuchukua dakika fulani ili kumpigia simu rafiki fulani au mtu tunayemjua ambaye, kulingana nasi, ataweza labda kusikiliza? Au labda, ikiwa hatukumkuta mtu fulani nyumbani kwake, kwa nini tusimuandikie? Je! tumekwisha kufikiria kuacha trakti kwa mfanya biashara ambaye kwake tunanunua vitu? Bila shaka, tunaweza kufikiri juu ya nafasi mbalimbali zinazojitokeza kwetu kila siku ili kujulisha tumaini letu kwa wengine. Ikiwa sisi tunajitahidi na pia kuongezea kwa hilo ujasiri mdogo, Yehova atatusaidia.—1 Tes. 2:2.

6 Kwa hiyo, kabla ya kuanza kazi zetu mbalimbali za kila siku, tujiulize hivi: ‘Je! mimi nitachukua hatua ya kwanza kuanzisha mazungumzo ili kujulisha tumaini langu ikiwa nafasi inajitokeza leo?’ Tuige msimamo wa Yesu ambaye alifasiria sababu iliyofanya atumwe duniani: “Ni lazima nitangaze habari njema za ufalme wa Mungu.” (Luka 4:​43, NW) Ikiwa tunapenda kuwa kama Mfundishaji wetu, tutafanya vivyo hivyo.—Lk. 6:40.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine