Shiriki Kikamili Katika Mavuno
1 Manabii wa kale wa Yehova na Yesu Kristo mwenyewe walisema kuhusu kazi ya ukusanyaji. (Isa. 56:8; Ezek. 34:11; Yn. 10:16) Kazi kama hiyo ni yenye kutimizwa sasa kadiri habari njema ya Ufalme inavyohubiriwa ulimwenguni pote. (Mt. 24:14) Tofauti kati ya wale wanaomtumikia Mungu na wale wasiomtumikia ni yenye kuwa wazi sana. (Mal. 3:18) Hilo linamaanisha nini kwetu?
2 Daraka la Kibinafsi: Tunaweza kujifunza kutokana na mfano wa Paulo, aliyehusika kikamili katika kuongoza huduma ya Kikristo. Alijihisi kuwa na deni kuhusiana na daraka la kuhubiri ili watu wote wawe na nafasi ya kusikia habari njema na kuokolewa. Hilo lilimsukuma afanye kazi ya jasho bila kuacha kwa ajili yao. (Rom. 1:14-17) Kwa sababu ya hali yenye hatari ambayo wanadamu wanapambana nayo leo, je, hatujisikii kuwa wenye kuchochewa zaidi kuhubiria watu wa eneo tulilogawiwa?—1 Kor. 9:16.
3 Wakati wa Kutenda Haraka: Kazi ya kuhubiri inaweza kulinganishwa na utendaji wa kutafuta na kuokoa watu. Tunapaswa kupata watu mahali walipo, na kuwasaidia wafikie usalama kabla haijakuwa kuchelewa mno. Wakati ni mdogo. Uhai uko katika hatari! Si jambo la kushangaza kwamba Yesu alihimiza wanafunzi wake “[waombe] Bwana-mkubwa wa mavuno atume wafanyakazi katika mavuno yake.”—Mt. 9:38.
4 Wakitambua hali ya uharaka ya leo, wafanyakazi wengi wa Ufalme wameongeza ushiriki wao katika utendaji huo wenye kuokoa uhai. Kijana mmoja anayeitwa Hirohisa aliishi katika familia yenye mzazi mmoja pamoja na ndugu na dada zake. Alitegemeza familia yake kifedha kwa kuamka pa saa 9 za usiku ili kutoa magazeti ya habari. Hata hivyo, Hirohisa alitaka kufanya zaidi katika huduma; kwa hiyo, akaanza upainia wa kawaida. Je, kuna njia ambazo katika hizo unaweza kushiriki kikamili zaidi katika kazi hii ambayo haitarudiwa tena kamwe?
5 “Wakati ubakio umepunguzwa.” (1 Kor. 7:29) Kwa hiyo, acheni tufanye yote tuwezayo katika ile kazi ya maana zaidi inayotimizwa duniani leo—kuhubiri habari njema ya Ufalme na kufanya wanafunzi. Yesu alilinganisha huduma hiyo na kazi ya mavuno. (Mt. 9:35-38) Kupitia kushiriki kwetu kikamili katika mavuno, matokeo ya kazi yetu ya jasho inaweza kutia ndani kusaidia mtu fulani awe sehemu ya ule mkutano mkubwa wa waabudu wanaoelezwa kwenye Ufunuo 7:9, 10.