Toa ushahidi ukiwa jirani mwema
1 Yesu alisema “umpende jirani yako kama wewe mwenyewe.” (Mt. 22:39) Bila shaka, ‘unafanya lililo jema’ kuelekea waamini wenzako, lakini je, unaweza kupanuka katika upendo wako kuelekea watu wale wanaoishi kando-kando? (Gal. 6:10) Katika njia gani?
2 Kwa kujitambulisha: Je, majirani wako wanajua kwamba wewe ni Shahidi? Ikiwa sivyo, kwa nini usiwatembelee katika utumishi wa shambani? Matokeo huenda yakakushangaza! Au ikiwa utajisikia mwenye kutulia zaidi kwa kuwatolea ushahidi kivivi-hivi, jaribu kufanya hivyo. Unapokuwa nje, unaweza kuwaona wakifanya kazi katika uwanja kando-kando ya nyumba au wakijitembeza barabarani. Wakaribie kwa kicheko chenye shauku. Jitahidi kusema kuhusu imani zako, mahali ambapo Jumba la Ufalme linapatikana, na mambo yanayofanyika hapo, na uwajulishe mtu mwingine yeyote katika ujirani anayehudhuria. Watolee mwaliko wa kuhudhuria mikutano. Uwe mwenye kuazimia kutoa ushahidi kamili kuhusu habari njema kwa kila mtu unayemjua.—Mdo. 10:42; 28:23.
3 Kwa mwenendo wako wa kuigwa: Mwenendo wako wa kirafiki husema mengi kukuhusu wewe na unaweza kufungua njia ili kutoa ushahidi. Huo pia ‘hupamba fundisho la Mungu.’ (Tito 2:7, 10) Onyesha kwamba unapendezwa kwelikweli na majirani zako. Uwe mwenye urafiki na msikivu. Heshimu haki yao ya kuwa na mambo ya siri na mazingira yenye utulivu. Ikiwa mmoja wao anagonjwa, uwe na ufikirio, na upendekeze kutoa msaada. Wakati familia mpya inapohamia katika ujirani, watembelee kwa kifupi ili kuwakaribisha. Matendo kama hayo ya wema huacha alama yenye kufaa na ni yenye kupendeza Yehova.—Ebr. 13:16.
4 Kupitia hali ya nje ya kiwanja chako: Kuwa jirani mwema kunatia ndani kushughulikia nyumba yako ili iwe yenye kupendeza. Nyumba na uwanja ambavyo ni safi na vyenye kuvutia, vyenyewe ni ushahidi. Lakini nyumba ambayo ni chafu au yenye vitu vinavyotupwa kando-kando hupunguza sifa ya ujumbe wa Ufalme. Hivyo, ni jambo la maana sana kufanya nyumba yako, uwanja wako, na magari yako viendelee kuwa safi na vyenye hali nzuri.
5 Kuonyesha hangaiko kuelekea wale walio nje ya kutaniko la Kikristo kunaonyesha upendo kwa majirani. Matokeo yanaweza kuwa nini? “Likiwa tokeo la kazi zenu bora ambazo wamekuwa mashahidi wa kujionea,” inawezekana kwamba wengine ‘watamtukuza Mungu.’—1 Pet. 2:12.