Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/99 uku. 1
  • Kuzidisha Ushahidi Kadiri Mwisho Unavyokaribia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kuzidisha Ushahidi Kadiri Mwisho Unavyokaribia
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tuendelee Kutambua Uhitaji Wa Kutenda Kwa Haraka
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Unapaswa Kufanya Nini ili Uendelee Kutambua Lazima ya Kuhubiri kwa Haraka?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • “Lihubiri neno . . . kwa hima”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Kwa Mfano wa Yesu Tutangaze Kweli Kila Siku
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 4/99 uku. 1

Kuzidisha Ushahidi Kadiri Mwisho Unavyokaribia

1 Majira ya mavuno ni wakati wenye furaha. Huo pia ni wakati wa kazi ngumu. Kuna wakati mchache tu ili kukusanya mazao. Wafanyakazi hawapaswi [must] kuchezacheza kazini.

2 Akisema kwa njia ya mfano, Yesu alilinganisha “umalizio wa mfumo wa mambo” na wakati wa mavuno. (Mt. 13:39) Tunaishi katika umalizio wa mfumo huu wa mambo, kukiwa kunabaki wakati mchache wa kutoa ushahidi “katika dunia yote inayokaliwa.” (Mt. 24:14) Kwa kuwa mwisho unakaribia zaidi na zaidi, tunahitaji kuzidisha kushiriki kwetu katika huduma. Kwa nini? Yesu alifasiria: “Mavuno ni mengi, lakini wafanyakazi ni wachache.”​—Mt. 9:​37, 38; Rom. 12:11.

3 Fanyeni Hilo kwa Haraka: Yesu alipoanza kazi yake kubwa ya kuhubiri, alikuwa na miaka mitatu na nusu tu ili kutimiza yale aliyogawiwa kufanya. Alihubiri akiwa na ufahamu wa hali ya haraka; alisema: “Ni lazima nitangaze habari njema ya ufalme wa Mungu, kwa sababu kwa ajili ya hili nilitumwa.”​—Luka 4:​43.

4 Yesu aliingiza ufahamu huohuo wa hali ya haraka katika wanafunzi wake. (Mk. 13:32-​37) Kwa sababu hiyo, “kila siku katika hekalu na kutoka nyumba hadi nyumba wakaendelea bila kuacha kufundisha na kutangaza habari njema juu ya Kristo, Yesu.” (Mdo 5:​42) Utendaji wa maana kidogo haukuchukua nafasi ya kwanza katika maisha zao. Ingawa walikuwa wachache, walifaulu kuhubiri habari njema “katika viumbe vyote chini ya mbingu.”​—Kol. 1:​23.

5 Tunayo hata sababu kubwa zaidi ya kusitawisha ufahamu huohuo wa hali ya haraka sasa, kwa kuwa “mwisho wa mambo yote umekaribia.” (1 Pet 4:7) Yehova ameweka siku na saa ya mwisho wa mfumo huu wa mambo. (Mt. 24:36) Kazi ya kuhubiri itaongeza [W step up vt 2] jitihada zetu za kufanya habari njema ifikie watu wengi zaidi na zaidi.

6 Kwa kuzidisha kushiriki kwetu katika kazi ya kutoa ushahidi kadiri mwisho unavyokaribia, tutakuwa wenye kutosheka kumwambia Yehova, kama alivyosema Yesu: ‘Tumemaliza kazi ambayo umetupatia tuifanye.’​—Yn. 17:4.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine