Kuzidisha Ushahidi Kadiri Mwisho Unavyokaribia
1 Majira ya mavuno ni wakati wenye furaha. Huo pia ni wakati wa kazi ngumu. Kuna wakati mchache tu ili kukusanya mazao. Wafanyakazi hawapaswi [must] kuchezacheza kazini.
2 Akisema kwa njia ya mfano, Yesu alilinganisha “umalizio wa mfumo wa mambo” na wakati wa mavuno. (Mt. 13:39) Tunaishi katika umalizio wa mfumo huu wa mambo, kukiwa kunabaki wakati mchache wa kutoa ushahidi “katika dunia yote inayokaliwa.” (Mt. 24:14) Kwa kuwa mwisho unakaribia zaidi na zaidi, tunahitaji kuzidisha kushiriki kwetu katika huduma. Kwa nini? Yesu alifasiria: “Mavuno ni mengi, lakini wafanyakazi ni wachache.”—Mt. 9:37, 38; Rom. 12:11.
3 Fanyeni Hilo kwa Haraka: Yesu alipoanza kazi yake kubwa ya kuhubiri, alikuwa na miaka mitatu na nusu tu ili kutimiza yale aliyogawiwa kufanya. Alihubiri akiwa na ufahamu wa hali ya haraka; alisema: “Ni lazima nitangaze habari njema ya ufalme wa Mungu, kwa sababu kwa ajili ya hili nilitumwa.”—Luka 4:43.
4 Yesu aliingiza ufahamu huohuo wa hali ya haraka katika wanafunzi wake. (Mk. 13:32-37) Kwa sababu hiyo, “kila siku katika hekalu na kutoka nyumba hadi nyumba wakaendelea bila kuacha kufundisha na kutangaza habari njema juu ya Kristo, Yesu.” (Mdo 5:42) Utendaji wa maana kidogo haukuchukua nafasi ya kwanza katika maisha zao. Ingawa walikuwa wachache, walifaulu kuhubiri habari njema “katika viumbe vyote chini ya mbingu.”—Kol. 1:23.
5 Tunayo hata sababu kubwa zaidi ya kusitawisha ufahamu huohuo wa hali ya haraka sasa, kwa kuwa “mwisho wa mambo yote umekaribia.” (1 Pet 4:7) Yehova ameweka siku na saa ya mwisho wa mfumo huu wa mambo. (Mt. 24:36) Kazi ya kuhubiri itaongeza [W step up vt 2] jitihada zetu za kufanya habari njema ifikie watu wengi zaidi na zaidi.
6 Kwa kuzidisha kushiriki kwetu katika kazi ya kutoa ushahidi kadiri mwisho unavyokaribia, tutakuwa wenye kutosheka kumwambia Yehova, kama alivyosema Yesu: ‘Tumemaliza kazi ambayo umetupatia tuifanye.’—Yn. 17:4.