TUNGO LA MWEZI: “LIHUBIRI NENO, FANYA HIVYO KWA BIDII [KWA HARAKA].”—2 TIM. 4:2.
Unapaswa Kufanya Nini ili Uendelee Kutambua Lazima ya Kuhubiri kwa Haraka?
Unapaswa kuendelea kutambua lazima ya kuhubiri kwa haraka ikiwa unataka kuokoka mwisho wa ulimwengu huu muovu. Ili uendelee kutambua lazima hiyo, unapaswa kufanya mambo yanayofuata.
Sali kila mara kuhusu Ufalme.—Mt. 6:10.
Linda moyo wako kwa kusoma Biblia kila siku.—Ebr. 3:12.
Tumia wakati wako vizuri.—Efe. 5:15, 16; Flp.1:10.
Endelea kuwa na jicho “rahisi.” Usiache tamaa za ulimwengu zikukengeushe.—Mt. 6:22, 25; 2 Tim. 4:10.
Uwe macho siku zote kwa kuendelea kutambua utimizo wa unabii wa Biblia. —Mk. 13:35-37.
Kutambua lazima ya kuhubiri kwa haraka kutatuchochea tuendelee kufanya kazi hiyo kwa bidii mupaka mwisho!—Yoh. 4:34, 35.