Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/04 uku. 1
  • Kutambua Umaana wa Kutenda kwa Haraka!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kutambua Umaana wa Kutenda kwa Haraka!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tuendelee Kutambua Uhitaji Wa Kutenda Kwa Haraka
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Unapaswa Kufanya Nini ili Uendelee Kutambua Lazima ya Kuhubiri kwa Haraka?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Kuzidisha Ushahidi Kadiri Mwisho Unavyokaribia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Tuhubiri Tukiwa Wenye Kutambua Uhitaji wa Kutenda kwa Haraka!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 11/04 uku. 1

Kutambua Umaana wa Kutenda kwa Haraka!

1 Yesu alijua kwamba wakati aliokuwa nao ili kufanya mapenzi ya Baba yake duniani ulikuwa mchache. (Yoh. 9:4) Kwa hiyo, alitimiza huduma yake akitambua umaana wa kutenda kwa haraka, naye alizoeza wafuasi wake kufanya vivyohivyo. (Luka 4:42-44; 8:1; 10:2-4) Kwake yeye vitu vya kimwili vilichukua nafasi ya pili. (Mt. 8:20) Kwa sababu hiyo, aliweza kumaliza kazi ambayo Yehova alimpa aifanye.—Yoh. 17:4.

2 Wakati Ni Mchache: Wakati wa kuhubiri habari njema katika “dunia yote inayokaliwa” ni mchache pia. (Mt. 24:14) Unabii wa Biblia unafunua kwamba tunakuwa mbali sana katika kipindi hiki cha wakati wa mwisho. Hivi karibuni “wale wasiomjua Mungu na wale wasiotii habari njema juu ya Bwana wetu Yesu . . . watahukumiwa adhabu ya uharibifu wa milele.” (2 The. 1:6-9) Hukumu hiyo itakuja kwa ghafula kabisa. (Luka 21:34, 35; 1 The. 5:2, 3) Watu wanahitaji kutambua kwamba wamo katika hali yenye hatari. Ni daraka letu kuwasaidia ili watafute kibali cha Yehova kukiwa bado na wakati.—Sef. 2:2, 3.

3 Kufanya Yote Tuwezayo: Wakitambua kwamba “wakati uliobaki umepungua,” watumishi wa Mungu wanatanguliza kazi ya kuhubiri. (1 Kor. 7:29-31; Mt. 6:33) Wengine wamekataa nafasi bora zaidi kiuchumi na ufuatiaji mwingine wa mambo ya kibinafsi ili kuongeza ushiriki wao katika kazi ya kuhubiri. (Marko 10:29, 30) Wengine wanaendelea kuwa na “mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana” ijapokuwa majaribu yenye kuendelea. (1 Kor. 15:58) Wengi wamekuwa wenye kutangaza peupe habari njema kwa miaka mingi bila kuyumbayumba. (Ebr. 10:23) Yehova anathamini sana dhabihu zote hizo zinazofanywa ili kutegemeza faida za Ufalme.—Ebr. 6:10.

4 Kwa kufanya maisha yetu yategemee ibada ya Yehova, inayotia ndani kazi ya kuhubiri, kunatusaidia tuendelee kuweka siku ya Yehova karibu katika akili. Kunatulinda tusikengeushwe na ulimwengu wa Shetani na kunatia nguvu azimio letu la kudumisha mwenendo mtakatifu. (2 Pet. 3:11-14) Kwa kweli, kutimiza huduma yetu huku tukitambua umaana wa kutenda kwa haraka kunaweza kuokoa uhai wetu na wa wale wanaotusikiliza.—1 Tim. 4:16.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine