Tuhubiri Tukiwa Wenye Kutambua Uhitaji wa Kutenda kwa Haraka!
1. Ni shauri gani la Paulo ambalo tunapaswa kufikiria katika siku za leo?
1 “Lihubiri neno, fanya hivyo kwa bidii.” (2 Tim. 4:2) Kwa nini shauri la Paulo ni la maana sana katika siku za leo? Maneno haya yanaweza kuwa na matokeo gani katika maisha yetu na ya wengine?
2. Kwa nini tunatafuta kwa bidii wale ambao hawajasikia habari njema?
2 Maisha ya Watu Yako Katika Hatari: Mamilioni ya watu ulimwenguni pote bado wanahitaji kusikia habari njema inayoweza kuwasaidia wapate wokovu. (Rom. 10:13-15; 1 Tim. 4:16) Hata katika eneo linalohubiriwa mara kwa mara, tunakutana na watu wengi wenye mioyo ya haki. Ikiwa tunabadili siku ao wakati wa kutembelea watu wa eneo hilo, tunaweza kukutana na watu tofauti na wale tuliokutana nao hapo mbele. Kutafuta watu kwa bidii kwa njia hiyo kutatusaidia tuwe na zamiri safi na kutatufanya tusiwe na hatia ya damu.—Mdo. 20:26.
3. Namna gani tunaweza kutumia wakati wetu kwa hekima katika mahubiri?
3 Hata ikiwa Wakristo wa karne ya kwanza walipatwa na upinzani mkali, ‘walijaza Yerusalemu fundisho lao.’ (Mdo. 5:28) Je, sisi pia tunakusudia sana “kutoa ushahidi kamili”? (Mdo. 10:42) Tunapokuwa katika mahubiri, je, tunatumia wakati kwa hekima? Ikiwa tunangojea wahubiri wengine wanaorudilia mutu fulani, je, tunatumia nafasi hiyo ili kuhubiria wapita-njia?
4. Namna gani kuhubiri tukiwa wenye kutambua uhitaji wa kutenda kwa haraka kunatusaidia tuendelee kukesha?
4 Tunakuwa Waangalifu Zaidi: Kwa kuwa mwisho wa ulimwengu huu unakaribia sana, tunapaswa kuwa waangalifu, na kuendelea kukesha. (1 The. 5:1-6) Tunapozungumza kwa kawaida kuhusu tumaini letu la Ufalme, tunaepuka kulemewa na mambo ya ulimwengu huu. (Luka 21:34-36) Pia, tunapolinda siku ya Yehova “karibu akilini,” tunachochewa kushiriki zaidi katika kazi ya kuhubiri inayookoa uzima.—2 Pet. 3:11, 12.
5. Kuheshimu uzima kunatuchochea kufanya nini katika kazi ya kuhubiri?
5 Tunapohubiri tukiwa wenye kutambua uhitaji wa kutenda kwa haraka, tunaonyesha kwamba tuna maoni ya Yehova kuhusu maisha: “Hataki yeyote aangamizwe bali hutaka wote wafikie toba.” (2 Pet. 3:9; Eze. 33:11) Acheni basi tukusudie sana kuhubiria watu wengi kadiri iwezekanavyo katika eneo letu, yote hayo kwa utukufu wa Yehova!—Zab. 109:30.