Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 1/09 uku. 1
  • Watasikia Namna Gani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Watasikia Namna Gani?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2009
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tutangaze Bila Kuacha Habari Njema
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Kwa Nini Tunarudilia Watu Mara Nyingi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Hubiri Bila Kuacha
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • “Akafikiri Nao kwa Kutumia Maandiko”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2009
km 1/09 uku. 1

Watasikia Namna Gani?

1. Kwa nini inaweza kuwa vigumu kuhubiri, na kwa nini tunavumilia?

1 Kwa kuwa siku ya Yehova inakaribia sana, kuna uhitaji wa kutenda kwa haraka ili kusaidia watu wengi wapate ujuzi sahihi wa Mungu na wa kusudi lake kuhusu wanadamu. (Yoh. 17:3; 2 Pet. 3:9, 10) Wakati mwingine inaweza kuwa vigumu kuhubiri kwa kuwa watu wengi hawapendezwi na ujumbe wetu na wanaweza hata kutucheka kwa sababu ya kazi yetu ya kuhubiri. (2 Pet. 3:3, 4) Hata hivyo, tunaamini kwamba bado kuna watu fulani katika eneo letu ambao watakubali habari njema watakapohubiriwa. Watu kama hao, watasikia namna gani bila mutu kuhubiri?—Rom. 10:14, 15.

2. Namna gani mfano wa mtume Paulo unatutia moyo?

2 Kushindana na Upinzani: Kwa kuwa bado kungali watu wengi walio tayari kusikia ujumbe wa Ufalme, hatupaswi kuacha kuhubiri. Jiji la Filipi lilikuwa la kwanza huko Ulaya kusikia mtume Paulo akihubiri habari njema. Paulo na Sila waliposhitakiwa kwa uongo, walipigwa kwa fimbo na kutupwa gerezani. (Mdo. 16:16-24) Hata hivyo, mateso hayo, hayakumfanya Paulo aache kuhubiri kwa sababu ya woga. Paulo alipotembelea Thesalonike, jiji la pili katika safari yake ya umishonari, ‘alijipa ujasiri kwa njia ya Mungu.’ (1 The. 2:2) Mfano wa Paulo unatuonyesha kabisa kwa nini hatupaswi ‘kufa moyo.’—Gal. 6:9.

3. Ni nini linaloweza kufanya watu fulani wabadili maoni yao ijapokuwa hawakupendezwa na habari ya Ufalme hapo mbele?

3 Watu wengi ambao kwa muda wa miaka mingi wamekataa kusikiliza habari ya Ufalme, wamebadili maoni yao. Matatizo ya kupata feza, magonjwa, kifo katika familia ao habari zenye kusumbua watu katika ulimwengu zinaweza kutokeza badiliko hilo. (1 Kor. 7:31) Watu fulani ambao hapo mbele walipingwa na wazazi wao wamekuwa sasa watu wazima na wako sasa tayari kusikiliza. Tunapoendelea kuhubiria watu kama hao, wanapata nafasi ya ‘kuliitia jina la Yehova’ kabla haijakuwa kuchelewa.—Rom. 10:13.

4. Ni nini kinachotuchochea tuendelee kuhubiri “bila kuacha”?

4 “Bila Kuacha”: Upendo wetu kwa Mungu na jirani utatuchochea kuendelea kuhubiri na kufanya wanafunzi “bila kuacha,” kama mitume walivyofanya katika karne ya kwanza. (Mdo. 5:42) Leo watu wengi ni wenye ‘kuugua na kulia kwa sababu ya machukizo’ yanayotendeka sasa. (Eze. 9:4) Watu kama hao wanapata tumaini kabisa na kitulizo wanaposikia habari njema! Hata wakati ambapo watu wengi zaidi hawatusikilize, Maandiko yanatuhakikishia kwamba Yehova anapendezwa anapoona jinsi tunavyojikaza.—Ebr. 13:15, 16.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine