Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 7/07 uku. 4
  • Kwa Nini Tunarudilia Watu Mara Nyingi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kwa Nini Tunarudilia Watu Mara Nyingi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Tumetumika Eneo Letu Mara Nyingi!”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Kwa Nini Uendelee Kuhubiri?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Kwa Nini Kuendelea?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Endelea Kuwa na Mawazo ya Muzuri juu ya Mahubiri
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2007
km 7/07 uku. 4

Kwa Nini Tunarudilia Watu Mara Nyingi

1 Mahali pengi, tunamaliza kuhubiri eneo lote na tunalirudilia-rudilia. Tunaendelea kurudia kwenye nyumba zilezile, hata ikiwa mwenye nyumba ametuambia kwamba hapendezwi na ujumbe wetu. Kwa nini tunaendelea tena kurudilia wale ambao hawakukubali ujumbe wetu wakati uliopita?

2 Upendo Wetu kwa Yehova na kwa Watu: Sababu kubwa inayotufanya tuvumilie katika kazi ya kuhubiri ni upendo wetu kwa Yehova. Mioyo yetu inatuchochea tuendelee kuelezea wengine kuhusu Mungu wetu mkuu. (Luka 6:45) Upendo wetu kwa Yehova unatusukuma tutii amri zake na kusaidia wengine nao wafanye hivyo. (Met. 27:11; 1 Yoh. 5:3) Tunaendelea kuvumilia kwa uaminifu katika kazi hii, watu wakubali au wasikubali ujumbe wetu. Hata wakati Wakristo wa karne ya kwanza walipoteswa, waliendelea kuhubiri “bila kuacha.” (Mdo. 5:42) Watu wanapokataa kutusikiliza, kuliko kuacha jambo hilo lituvunje moyo, tunabaki imara, tukionyesha upendo wetu mwingi na ujitoaji kwa Yehova.

3 Tunavumilia pia kwa sababu tunapenda jirani yetu. (Luka 10:27) Yehova hataki mtu yeyote aharibiwe. (2 Pet. 3:9) Hata katika eneo linalohubiriwa mara kwa mara, tunaendelea kupata wale wanaopenda kumtumikia Yehova. Kwa mfano, katika Guadeloupe, ambako mtu 1 kati ya 56 ni Shahidi wa Yehova, watu 214 walibatizwa mwaka jana. Karibu watu 20,000 walihuzuria Ukumbusho, ni kama vile mtu 1 kati ya 22 alihuzuria Ukumbusho katika Guadeloupe!

4 Mabadiliko Katika Eneo: Katika eneo letu, tunaendelea kukutana na watu ambao hatukukutana nao wakati uliopita. Wakati ujao tutakapopiga hodi kwenye mlango fulani, mahali ambapo watu hawakukubali ujumbe wetu wakati uliopita, huenda mtu fulani katika familia hiyo—labda mtu ambaye hajasikia hata kidogo habari yetu—anaweza kufungua mlango na kusikiliza. Ao tunaweza kukuta nyumba hiyo ikiwa sasa na wakaaji wengine ambao wamehamia humo na wanaopendezwa na ujumbe wetu. Watoto walio na wazazi wanaopinga, wanaweza kukomaa na kuondoka nyumbani. Watu hao wanaweza kuwa tayari kusikiliza habari ya Ufalme.

5 Watu pia wanabadilika. Mtume Paulo alikuwa kwanza “mkufuru na mtesaji na mwenye dharau.” (1 Tim. 1:13) Vivyo hivyo, wengi ambao wanamtumikia Yehova leo, hawakupendezwa na kweli wakati uliopita. Wengine wao walipinga sana habari njema wakati fulani. Kwa kuwa mara kwa mara hali za ulimwengu zinabadilika, watu fulani ambao walikuwa wakipinga ao wale ambao hawakupendezwa wanaweza kutaka kusikiliza. Wengine wanaweza kuitikia vizuri kisha kupatwa na msiba fulani, kama vile kifo cha mshiriki wa familia, kupoteza kazi, tatizo la feza ao ugonjwa.

6 Ulimwengu huu unakaribia mwisho, lakini kazi yetu ya kuhubiri na kufundisha ni yenye kuharakishwa. (Isa. 60:22) Kwa hiyo, tunaendelea kuhubiri kwa uchangamfu na tunajikaza kuendelea kuwa na maoni ya kutokuwazia watu vibaya ao eneo. Labda mtu tutakayezungumza naye baadaye atasikiliza. Ni lazima tuendelee kusema! ‘Kwa kufanya hivyo tutajiokoa sisi wenyewe na wale wanaotusikiliza pia.’—1 Tim. 4:16.

[Maulizo ya Funzo]

1. Ni ulizo gani linalotokea kuhusu kazi yetu ya kuhubiri?

2. Ni nini iliyo sababu kubwa inayotufanya tuvumilie katika kazi ya kuhubiri?

3. Jinsi gani kuwapenda watu kunatusaidia tuendelee kuhubiri?

4. Hali katika maeneo zinabadilika katika njia gani mbalimbali?

5. Ni mambo gani yanayoweza kufanya watu waitikie vizuri?

6. Kwa nini tunapaswa kuendelea kuhubiri kwa uchangamfu?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine