Kwa Nini Kuendelea?
1 Labda umekwisha kujiuliza ulizo hilo, kwa kujitayarisha kwa mfano kupitisha mchana katika mahubiri. Katika mahali fulani, eneo letu linatembelewa mara kwa mara, na inawezekana kwamba watu wanatutambua na kuwa tayari kutufukuza. Ni wachache tu ndio wanaopokea vizuri ujumbe wetu. Kuna hata hivyo sababu nzuri za kuendelea.
2 Kabla ya yote, tunapaswa kuendelea kuhubiri ujumbe wa Ufalme mpaka mwisho utakapofika. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Nabii Isaya alimuuliza Mungu mpaka wakati gani angeendelea na kazi ya mahubiri. Jibu, linaloripotiwa katika Isaya 6:11, lipo wazi. Yehova alimuambia aendelee kutoa ujumbe wa kimungu kwa taifa. Hivyo ndivyo ilivyo leo. Yehova anataka kwetu kwamba tuendelee na kuwatembelea watu wa eneo letu, hata ikiwa kweli kwamba watatufukuza. (Ezek. 3:10, 11) Hilo ndilo daraka takatifu ambalo tulikabidhiwa.—1 Kor. 9:17.
3 Jambo la pili, kuendelea kuhubiri ni nafasi kwetu ya kuonyesha kina kirefu cha ushikamanifu wetu kwa Yehova. (1 Yn. 5:3) Zaidi ya hilo, tunapofikiria wakati ujao ambao wanadamu wanawekewa akiba, namna gani basi tungeweza kujizuia kujaribu kuwaonya watu, jirani yetu, kwa upendo? (2 Tim. 4:2; Yk. 2:8) Ikiwa tunatimiza kiaminifu kazi yetu kwao, tutaongeza bahati yao ya kukubali ujumbe wa wokovu wa Mungu, na hawataweza kusema kwamba hawakuonywa.—Ezek. 5:13.
4 Zaidi ya hilo, nani ajuaye? moyo wa wamoja unaweza kugeuka. Labda kwa sababu ya mabadiliko ya hali, msiba katika familia au hali za ulimwengu ambazo zinawafanya kufikiri kwa uzito juu ya wakati wao ujao. Au pengine, siku fulani mlangoni pao, wataambiwa jambo fulani litakalotokeza kuitikia vizuri. (Muh. 9:11; 1 Kor. 7:31) Na pia kuna kuhama. Inawezekana kwamba tuwakute watu waliohamia hivi karibuni katika eneo letu watakaoitikia vizuri habari njema, au vijana wakubwa wanaoishi sasa wenyewe na wanaojiuliza juu ya kusudi la uhai wao.
5 Je! tutaendelea? Bila shaka! Maandiko yanatutolea sababu nzuri ili kwenda kuwaona na kuwarudilia tena watu. Hatimaye, wakati kazi ya kuhubiri itakapomalizika, Yehova atatubariki kwa kuwa tulifanya bidii kubwa katika huduma na atawabariki wale ambao, wakiwa wenye shukrani, walikubali habari njema ya Ufalme.—1 Tim. 4:16.