Tuanzishe Mafunzo ya Biblia Katika Broshua Anataka
1 Ripoti kutoka ulimwenguni pote zinaonyesha kwamba broshua Mungu Anataka Nini Kwetu? ni kifaa chenye nguvu cha kufundisha watu kweli. Maelfu ya mafunzo ya Biblia ni yenye kuanzishwa kila juma katika broshua hiyo. Je! umekuwa mwenye matokeo katika kuanzisha na kuongoza funzo la Biblia katika broshua Anataka?
2 Japo wengi huona kuwa rahisi kuangusha broshua hiyo, wengine huona kuwa vigumu kujua la kusema ili kuanzisha funzo. Ni njia gani wengine walizoziona kuwa zenye matokeo katika kuanzisha mafunzo ya Biblia kwa kutumia broshua Anataka? Madokezo yafuatayo yanaweza kuwa yenye kusaidia.
3 Tupendekeze Kufanya Onyesho la Funzo: Tunapofanya ziara ya kwanza au ziara ya kurudia, badala ya kupendekeza tu funzo la Biblia kwa msikilizaji, tunaweza kuonyesha jinsi funzo la Biblia linavyoendeshwa. Jambo hilo litaelekea kumaliza siri na wasiwasi inayofuata, siri ambayo wasikilizaji wengi huiambatanisha na neno “funzo.” Baada ya kuzoea kufanya onyesho la funzo, tutaona kwamba utangulizi mwepesi waweza kutusaidia tuingie moja kwa moja katika funzo.
4 Matayarisho Ndiyo Ufumbuzi: Shauku yetu ya kuanzisha mafunzo ya Biblia yahusiana moja kwa moja na jinsi tulivyojitayarisha vema. Matayarisho ya kimbele yanaweza kutusaidia tushinde kusita kokote tunakoweza kuwa nako tunaposhiriki katika kazi ya kuongoza mafunzo ya Biblia. Kwa kujizoeza utoaji wetu mara nyingi, tutakuwa wenye kuzungumza kwa urahisi zaidi na tutakuwa na uwezo wa kusema kama kawaida na kutumia maneno yetu wenyewe. Jambo hilo halitatuburudisha tu bali pia litamfurahisha zaidi msikilizaji wetu.
5 Unaporudilia utoaji wako, inafaa kukadiria wakati ili uweze kumjulisha msikilizaji wakati ambao utachukua ili umwonyeshe jinsi funzo linavyoendeshwa. Baada ya ndugu mmoja kujitambulisha, anasema: “Nilikutembelea ili nikuonyeshe programu yetu ya funzo la Biblia bila malipo. Inaomba dakika tano hivi. Je! unazo dakika tano?” Somo 1 la broshua Anataka laweza kuonyeshwa kwa dakika tano hivi. Bila shaka, ni maandiko yaliyochaguliwa tu yanayoweza kusomwa katika kiasi hicho cha wakati, lakini kwa kumaliza somo la kwanza kwa dakika chache, msikilizaji anaweza kuonja somo lake la kwanza. Kisha mjulishe kwamba utakaporudi kujifunza Somo 2, utachukua dakika 15 tu.
6 Utoaji Ufuatao Ulithibitika Kuwa Wenye Matokeo: “Ningependa kukuonyesha jinsi ya kuendesha funzo la Biblia lililo jepesi na lenye kukamilishwa kwa wakati mfupi kwa kutumia broshua hii Mungu Anataka Nini Kwetu? Wengi wameona kwamba katika dakika 15 tu kila juma kwa muda wa majuma 16, wanaweza kupata ufumbuzi wa Kimaandiko wenye kutosheleza wa mambo ya maana yanayopatikana katika Biblia.” Onyesha yaliyomo kwa kifupi. Kwa kugeuza ukurasa hadi Somo 1, sema: “Ikiwa unaweza kutupa dakika tano hivi, tungependa kukuonyesha namna hili linavyofanyika. Somo 1 ni lenye kichwa ‘Jinsi Unaweza Kuvumbua Kile Mungu Anataka.’ ” Kisha soma yale maulizo matatu, na ufasirie namba zilizo katika vifungo vya mraba. Soma fungu 1, na uonyeshe msikilizaji jinsi ya kupata jibu. Unaweza kumwomba msikilizaji asome fungu 2. Kisha sema: “Kwa msingi wa habari hii, unawezaje kujibu ulizo hili? [Soma tena ulizo, na uache msikilizaji ajibu.] Utaona kwamba kuna maandiko yanayoambatana na kila fungu. Hayo huelekeza uangalifu wetu kwenye jibu la Biblia la maulizo hayo. Kwa mfano, tusome 2 Timotheo 3:16, 17 na tuone ikiwa linapatana na jibu ulilotoa kuhusu mtungaji wa Biblia.” Baada ya kusoma fungu 3, kufikiria ulizo, na kusoma Yohana 17:3, vuta uangalifu wa msikilizaji juu ya ujuzi ambao amepata kwa kurudilia Somo 1. Hapo, unaweza kugeuza ukurasa hadi Soma 2 na kusoma ulizo la mwisho, “Ni njia gani mbili zinazoweza kutusaidia kujifunza juu ya Mungu?” Kisha uliza: “Ni siku gani utakapokuwa na dakika 15 hivi ili tufanye Somo 2 na kupata jibu?”
7 Ni jambo la maana kufanya mazungumzo yawe mepesi sikuzote na kumpongeza msikilizaji kila wakati inapowezekana. Unapopanga ziara nyingine, badala ya kuuliza ikiwa msikilizaji anataka kuendelea, mtie tu moyo afuate utaratibu uohuo kwenye somo linalofuata. Mjulishe kwamba unatazamia kurudi. Wahubiri fulani wamependekeza kufanya funzo kwa njia ya simu ikiwa programu ilikuwa ngumu. Unaweza pia kumtia moyo mwanafunzi aweke broshua mahali salama na penye kufaa kusudi iwe tayari kwa ajili ya ziara yenye kufuata.
8 Uwe na Nia Thabiti: Japo matayarisho ndiyo ufumbuzi, tunapaswa kuwa na nia thabiti ya kuendelea mpaka mwisho. Kufundisha somo katika dakika chache kwaweza kuwa tatizo; kwa hiyo, uwe na nia thabiti ya kujizoeza utoaji mara nyingi inavyohitajika kusudi uwe mwenye usemi rahisi unapoonyesha jinsi funzo linavyoendeshwa. Jaribu kuonyesha kila mtu unayemkuta kwenye mlango, barabarani, na unapotoa ushahidi kupitia simu jinsi funzo hilo linavyoendeshwa. Ikiwa ni tatizo kupata funzo la Biblia, usivunjike moyo. Matokeo katika kuanzisha mafunzo ya Biblia yanaomba nia thabiti na tamaa ya kweli kweli ya kuwapa wengine kweli.—Gal. 6:9.
9 Kwa kutumia madokezo haya, wewe pia waweza kuwa na pendeleo la kusaidia mtu fulani katika njia iendayo kwenye uzima, kwa kuanzisha na kuongoza funzo la Biblia katika broshua Anataka.—Mt. 7:14.