Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 9/96 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Ya Septemba

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mikutano Ya Utumishi Ya Septemba
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 9/96 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Ya Septemba

Juma Toka Septemba 9

Wimbo 56

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa ya Huduma Yetu ya Ufalme.

Dak. 20: “Tutangaze Bila Kuacha Habari Njema.” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Taja mawazo fulani kutoka kitabu Auxiliaire pour une meilleure intelligence de la Bible, ukurasa 1216, fu. 7.

Dak. 15: “Tutangaze Habari Njema ya Ufalme kwa Msaada wa Broshua.” (maf. 1-5) Tumia fungu la kwanza kwa ajili ya utangulizi. Toa maelezo yenye kujenga juu ya manufaa ya broshua Kuishi Milele Katika Furaha na “Tazama!” katika mahubiri. Tayarisha maonyesho manne yaliyorudiliwa vizuri yanayoonyesha jinsi tunaweza kutumia broshua hizo wakati wa kuonana kwa mara ya kwanza au wa ziara ya kurudia. Maonyesho juu ya broshua Kuishi Milele Katika Furaha yatafanywa na mhubiri kijana, akishindikizwa na baba yake au mama yake. Wahubiri watapendelea labda kutolea broshua nyingine kwa kufuata vielelezo vinavyodokezwa.

Wimbo 136 na sala ya mwisho.

Juma Toka Septemba 16

Wimbo 192

Dak. 15: Matangazo. Hali ya akaunti. Toa maelezo yenye kutia moyo juu ya “Namna Mbalimbali za Kutoa,” kwa kutumia Mnara wa Mlinzi wa Desemba 1, 1993, kurasa 29-31.

Dak. 15: “Tutangaze Habari Njema ya Ufalme kwa Msaada wa Broshua.” (maf. 6-8) Toa maelezo mafupi ya yaliyomo katika broshua Serikali. Maonyesho pamoja na vielelezo vinavyopendekezwa kwa mazungumzo ya kwanza na ziara ya kurudia. Tia kila mhubiri moyo kurudi kuwaona wale waliokubali vichapo.

Dak. 15: “Michango kwa Ajili ya Kazi ya Ulimwenguni Pote ya Sosaiti Inategemeza Mpanuko.” Hotuba changamfu inayotolewa na mzee. Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Agosti 1996. Kwa msaada wa Kitabu-Mwaka, toa hesabu fulani zinazohakikisha maendeleo ya kazi ya Ufalme katika nchi fulani zinazowakilishwa.

Wimbo 9 na sala ya mwisho.

Juma Toka Septemba 23

Wimbo 174

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Chunguza kisanduku “Majibu kwa Maulizo Yenu.”

Dak. 15: “Nani Anayestahili Kuhubiri?” Mzee anazungumzia makala pamoja na wahubiri wawili au watatu. Tia mkazo juu ya wazo la kwamba tunapokea mazoezi bora kuliko, ambayo yanatutolea vifaa kikamili ili kuwa wahudumu wa Mungu. Hatuna sababu yoyote ya kujisikia kwamba hatustahili kuhubiri.

Dak. 20: “Jinsi ya Kufanya Wanafunzi kwa Msaada wa Kitabu Ujuzi.” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji ya mafungu 17-26 ya nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 1996. Panga wakati mchache ili kuzungumzia mambo fulani yaliyoonwa ya mahali penu kuhusu wahubiri wanaoongoza mafunzo kwa msaada wa kitabu Ujuzi. Wanaweza kufasiria kwa namna yenye kutia moyo jinsi walivyotumikisha madokezo yaliyomo katika nyongeza na katika njia gani hilo liliwasaidia kuongoza mafunzo ya Biblia yanayofanya maendeleo zaidi. Tia wahubiri wote moyo kulinda nyongeza hiyo na kuichunguza upya kibinafsi kila mara wanapoanzisha funzo lipya.

Wimbo 189 na sala ya mwisho.

Juma Toka Septemba 30

Wimbo 104

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Chunguza kisanduku “Kusanyiko Lipya la Pekee la Siku Moja.” Tangaza mipango iliyochukuliwa kwa ajili ya mahubiri mwishoni mwa juma.

Dak. 20: Pendezweni na Shule ya Watoto Wenu. Hotuba inayotolewa na mzee. Chunguza mawazo yaliyo katika broshua Mashahidi wa Yehova na Elimu, kurasa 2-5, yanayoonyesha kwamba tunashukuru kwa mazoezi yenye manufaa zaidi ambayo yanatolewa na shule. Onyesha jinsi ya kufasiria walimu kwa busara sababu kwa nini tunafuatia kwanza miradi ya kiroho badala ya kazi-maisha ya kiufundi. Rudilia mawazo ya “Umalizio,” ukurasa 31. Tia wazazi moyo kutumikisha madokezo yanayotolewa na Amkeni! ya Septemba 8, 1988, ukurasa 11.

Dak. 15: Kichapo tutakachotolea mnamo Oktoba. Tutatumia kitabu La vie : comment est-elle apparue ? Évolution ou création ? Onyesha kwamba kitabu hicho kinazungumzia habari mbalimbali. Sura 1-15 zinachambua kwa undani ubishi kuhusu kutokea kwa uhai duniani; sura 16 inatokeza ulizo linaloacha kila mtu bumbuazi. “Kwa Nini Mungu Angeruhusu Mateso?”; sura 17-18 zinajenga imani katika Biblia kama vile Neno la Mungu lililoongozwa na lenye kustahili kutumainiwa; sura 19-20 zinavutia uangalifu juu habari njema ya Ufalme kuhusu uhai kwenye dunia ya kiparadiso na zinafasiria jinsi ya kuupata. Onyesho: mhubiri mmoja mwenye uwezo atatumia mojawapo ya mawazo hayo ili kutolea kwa kifupi kitabu Création. Tutaweza kutolea vitabu Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha na Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani ikiwa kutaniko linavyo ndani ya stoki.

Wimbo 113 na sala ya mwisho.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine