Tuhubiri Ufalme
1 Katika Waebrania 10:23, tunahimizwa ‘kushika sana lile tangazo la hadharani la tumaini,’ ambalo msingi walo ni juu ya Ufalme wa Mungu. Yesu aliamuru waziwazi kwamba habari njema ya Ufalme ihubiriwe katika mataifa yote. (Mk. 13:10) Ni jambo la muhimu kwamba tuchunge hilo akilini wakati tunaposhiriki katika huduma.
2 Tunapokutana na watu, tunajaribu kuanzisha mazungumzo juu ya habari fulani inayowapendeza au inayowahusu. Mara nyingi, tunataja hali ambazo wanajua vizuri, kama vile mauaji katika ujirani, matatizo yanayogusa vijana, hangaiko la kuweza kutosheleza mahitaji yao au kuharibika kwa uchumi. Kwa kuwa watu wengi wanakazia akili juu ya “mahangaiko ya maisha,” wanatujulisha mara nyingi kile kinachowasumbua wakati tunapoonyesha kwamba tunapendezwa nao na kwamba tunawaelewa. (Lk. 21:34) Hilo linaweza kutuwezesha baadaye kutangaza tumaini letu.
3 Hata hivyo, ikiwa sisi si wangalifu, mazungumzo yanaweza kuwa juu ya mawazo yasiyojenga kwa kiasi kutofikia kusudi la ziara yetu: kuhuburi ujumbe wa Ufalme. Ikiwa ni kweli kwamba tunachochea watu watende juu ya hali mbaya zilizo chanzo cha matatizo mengi, kusudi letu ni kuongoza uangalifu wao juu ya Ufalme, tumaini pekee la wanadamu. Bila shaka, tunalo tumaini nzuri ajabu ambalo watake wasitake watu wana lazima ya kulijua. Hivyo, hata ikiwa tunaanza kwa kutaja hali fulani za “nyakati za hatari, zilizo ngumu kushughulika nazo”, tuongoze haraka mazungumzo yetu kwanza juu ya kiini cha ujumbe wetu, “habari njema ya milele.” Kwa kufanya hivyo, tutatimiza kikamilifu huduma yetu.—2 Tim. 3:1; 4:5; Ufu. 14:6, NW.