Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kuanzisha Mazungumuzo ili Kuhubiri Wakati Hatukupanga Kufanya Hivyo
Sababu Gani ni Lazima Kufanya Hivyo: Tunapohubiri nyumba kwa nyumba, mara nyingi tunakuta watu wengi hawako nyumbani. Lakini, tunaweza kukutana nao tunaposafiri pamoja na watu wengi, tunapongojea muganga kwenye hopitali, wakati wa mapumuziko kwenye masomo ao kwenye kazi, na wakati mwengine wowote. Yehova anataka kila mutu apate nafasi ya kusikiliza ujumbe wa Ufalme. (1 Tim. 2:3, 4) Kwa hiyo, kila mara tunapaswa kuwa tayari kuanzisha mazungumuzo ili kuhubiri.
Tumikisha Shauri Hili Katika Mwezi:
Kila juma ujikaze kuanzisha mazungumuzo ukiwa na muradi wa kuhubiri hata kama haukupanga kufanya hivyo.