Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/09 uku. 6-7
  • Sisi Ni Mashahidi Nyakati Zote

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Sisi Ni Mashahidi Nyakati Zote
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2009
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Unaweza Kutoa Ushahidi Wakati Haukupanga Kufanya hivyo!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kuanzisha Mazungumuzo ili Kuhubiri Wakati Hatukupanga Kufanya Hivyo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Yesu anazungumuza na mwanamuke Musamaria kwenye kisima
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2018
  • Sifuni Yehova kwa Kutoa Ushahidi wa Vivi Hivi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2009
km 11/09 uku. 6-7

Sisi Ni Mashahidi Nyakati Zote

1. Tunaweza kujifunza nini kutokana na habari inayoeleza jinsi Yesu alivyomhubiria mwanamke kwenye kisima?

1 Yesu alikuwa ametembea kwa muda wa saa nyingi. Alikuwa amechoka na mwenye kiu. Wanafunzi wake walipokwenda kununua chakula, alikaa kwenye kisima cha maji inje ya mji wa Samaria ili kupumzika. Yesu hakuja Samaria ili kuhubiri, alipitia tu huko akijielekeza Galilaya ili kuendelea na kazi yake ya kuhubiri. Hata hivyo, alichukua nafasi ya kumhubiria mwanamke aliyekuja kwenye kisima ili kushota maji. (Yoh. 4:5-14) Kwa nini? Nyakati zote, Yesu aliendelea kuwa “shahidi mwaminifu na wa kweli” wa Yehova. (Ufu. 3:14) Tunamwiga Yesu kwa kuendelea kuwa Mashahidi wa Yehova nyakati zote.—1 Pet. 2:21.

2. Namna gani tunaweza kujitayarisha ili kuhubiria watu wakati hatukupanga kufanya hivyo?

2 Namna ya Kujitayarisha: Tunaweza kuwa tayari kuhubiria watu wakati hatukupanga kufanya hivyo kwa kuwa na vichapo kila wakati. Wahubiri wengi wanachukua trakti na kuzitolea watu wanaotumika kwenye maduka (magazins), kwenye vituo (stations) vya essence, na wengine ambao wanakutana nao muda wa siku. (Mhu. 11:6) Dada mmoja anayesafiri mara nyingi anatia Biblia yake ndogo na kitabu Biblia Inafundisha katika mfuko wake mdogo wa mkononi, na anajikaza kuanzisha mazungumzo na wale wanaokaa karibu naye.

3. Namna gani tunaweza kuanzisha mazungumzo?

3 Namna ya Kuanzisha Mazungumzo: Tunapohubiria watu wakati hatukupanga kufanya hivyo, si lazima kuanzisha mazungumzo kwa kutumia habari ya Maandiko. Alipoanzisha mazungumzo pamoja na mwanamke kwenye kisima, Yesu hakujitambulisha kuwa Masihi. Alimwomba tu maji ya kunywa, na hilo likamfanya apendezwe. (Yoh. 4:7-9) Dada mmoja aliona kwamba kutumia njia hiyo kunamsaidia kuanzisha mazungumzo anapoulizwa ikiwa alifurahia kuazimisha sikukuu fulani. Kuliko kujibu kwamba hakuazimisha sikukuu kwa kuwa yeye ni Shahidi wa Yehova, anasema tu hivi: “Niliamua kutokuazimisha sikukuu hiyo.” Mara nyingi, yule mwenye kuuliza ulizo anataka kujua kwa nini, na hivyo dada anapata nafasi ya kumtolea ushahidi.

4. Kwa nini andiko la Mathayo 28:18-20 linakuchochea?

4 Hata ikiwa Yesu alimaliza utumishi wake aliofanya kwa bidii duniani, yeye anaendelea kupendezwa sana na kazi ya kuhubiri inayoendelea kutimizwa kwa bidii kama alivyofanya. (Mt. 28:18-20) Kwa hiyo, kama Yesu Mfano wetu, sisi ni Mashahidi walio tayari kutoa ushahidi waziwazi kuhusu imani yetu.—Ebr. 10:23.  

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine