Sisi Ni Mashahidi Nyakati Zote
1. Tunaweza kujifunza nini kutokana na habari inayoeleza jinsi Yesu alivyomhubiria mwanamke kwenye kisima?
1 Yesu alikuwa ametembea kwa muda wa saa nyingi. Alikuwa amechoka na mwenye kiu. Wanafunzi wake walipokwenda kununua chakula, alikaa kwenye kisima cha maji inje ya mji wa Samaria ili kupumzika. Yesu hakuja Samaria ili kuhubiri, alipitia tu huko akijielekeza Galilaya ili kuendelea na kazi yake ya kuhubiri. Hata hivyo, alichukua nafasi ya kumhubiria mwanamke aliyekuja kwenye kisima ili kushota maji. (Yoh. 4:5-14) Kwa nini? Nyakati zote, Yesu aliendelea kuwa “shahidi mwaminifu na wa kweli” wa Yehova. (Ufu. 3:14) Tunamwiga Yesu kwa kuendelea kuwa Mashahidi wa Yehova nyakati zote.—1 Pet. 2:21.
2. Namna gani tunaweza kujitayarisha ili kuhubiria watu wakati hatukupanga kufanya hivyo?
2 Namna ya Kujitayarisha: Tunaweza kuwa tayari kuhubiria watu wakati hatukupanga kufanya hivyo kwa kuwa na vichapo kila wakati. Wahubiri wengi wanachukua trakti na kuzitolea watu wanaotumika kwenye maduka (magazins), kwenye vituo (stations) vya essence, na wengine ambao wanakutana nao muda wa siku. (Mhu. 11:6) Dada mmoja anayesafiri mara nyingi anatia Biblia yake ndogo na kitabu Biblia Inafundisha katika mfuko wake mdogo wa mkononi, na anajikaza kuanzisha mazungumzo na wale wanaokaa karibu naye.
3. Namna gani tunaweza kuanzisha mazungumzo?
3 Namna ya Kuanzisha Mazungumzo: Tunapohubiria watu wakati hatukupanga kufanya hivyo, si lazima kuanzisha mazungumzo kwa kutumia habari ya Maandiko. Alipoanzisha mazungumzo pamoja na mwanamke kwenye kisima, Yesu hakujitambulisha kuwa Masihi. Alimwomba tu maji ya kunywa, na hilo likamfanya apendezwe. (Yoh. 4:7-9) Dada mmoja aliona kwamba kutumia njia hiyo kunamsaidia kuanzisha mazungumzo anapoulizwa ikiwa alifurahia kuazimisha sikukuu fulani. Kuliko kujibu kwamba hakuazimisha sikukuu kwa kuwa yeye ni Shahidi wa Yehova, anasema tu hivi: “Niliamua kutokuazimisha sikukuu hiyo.” Mara nyingi, yule mwenye kuuliza ulizo anataka kujua kwa nini, na hivyo dada anapata nafasi ya kumtolea ushahidi.
4. Kwa nini andiko la Mathayo 28:18-20 linakuchochea?
4 Hata ikiwa Yesu alimaliza utumishi wake aliofanya kwa bidii duniani, yeye anaendelea kupendezwa sana na kazi ya kuhubiri inayoendelea kutimizwa kwa bidii kama alivyofanya. (Mt. 28:18-20) Kwa hiyo, kama Yesu Mfano wetu, sisi ni Mashahidi walio tayari kutoa ushahidi waziwazi kuhusu imani yetu.—Ebr. 10:23.