Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lmd somo 2
  • Kuzungumuza kwa Njia ya Kawaida

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kuzungumuza kwa Njia ya Kawaida
  • Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mambo Yenye Filipo Alifanya
  • Mufano wa Filipo Unatufundisha Nini?
  • Umuige Filipo
  • Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kuanzisha Mazungumuzo ili Kuhubiri Wakati Hatukupanga Kufanya Hivyo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Kupendezwa na Watu
    Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
  • Kutangaza “Habari Njema juu ya Yesu”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kuanzisha Mazungumuzo Yenye Itatutolea Nafasi ya Kuhubiri
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2018
Ona Habari Zaidi
Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
lmd somo 2

KUANZISHA MAZUNGUMUZO

Filipo mweneza-injili iko nazungumuza na mwanaume Muetiopia mwenye anaikala mu gari ya kukokotwa na iko nasoma kitabu ya kukunjwa.

Mdo. 8:30, 31

SOMO YA 2

Kuzungumuza kwa Njia ya Kawaida

Kanuni: “Neno lenye kusemwa wakati wenye kufaa​—ni la muzuri sana!”​—Mez. 15:23.

Mambo Yenye Filipo Alifanya

Filipo mweneza-injili iko nazungumuza na mwanaume Muetiopia mwenye anaikala mu gari ya kukokotwa na iko nasoma kitabu ya kukunjwa.

VIDEO: Filipo Anamuhubiria Towashi Muetiopia

1. Angalia VIDEO, ao usome Matendo 8:30, 31. Kisha ufikirie maulizo yenye kufuata:

  1. Namna gani Filipo alianzisha mazungumuzo?

  2. Nini njo inaonyesha kama Filipo alianzisha mazungumuzo na kumufundisha ule mwanaume kweli ya Biblia mu njia ya kawaida?

Mufano wa Filipo Unatufundisha Nini?

2. Kama tunazungumuza na mutu mu njia ya kawaida, ile itafanya ule mutu akuwe mwenye kutulia na afurahie kutusikiliza.

Umuige Filipo

3. Ukuwe muangalifu. Namna mutu anaonekana inaweza kutusaidia kujua mambo ya mingi juu yake. Vile unamuona ule mutu, iko tayari kuongea na weye? Pengine unaweza kuzungumuza naye habari fulani ya Biblia kwa kumuuliza tu “Unajuaka kama . . . ?” Usilazimishe mutu aongee na weye kama hapendi.

4. Ukuwe muvumilivu. Usiwaze kama wakati unaanza tu kuongea na mutu unapaswa kumuambia palepale kweli fulani ya Biblia. Muendelee tu na mazungumuzo; kuko saa nafasi itajitokeza, yenye unaweza kuingiza wazo fulani ya Biblia mu njia ya kawaida. Wakati fulani inaweza kuomba ungoye mupaka wakati mutazungumuza tena na ule mutu.

5. Ujipatanishe na hali. Wakati fulani musikilizaji anaweza kusema mambo yenye haukutazamia. Kama ni vile, unapaswa kuzungumuzia naye habari fulani yenye itapatana na mambo yenye alisema, hata kama ile habari haiko njo yenye ulipanga kuzungumza naye.

ONA PIA

Muh. 3:1, 7; 1 Ko. 9:22; 2 Ko. 2:17; Kol. 4:6

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine