Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lmd somo 1
  • Kupendezwa na Watu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kupendezwa na Watu
  • Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mambo Yenye Yesu Alifanya
  • Mufano wa Yesu Unatufundisha Nini?
  • Umuige Yesu
  • Kuzungumuza kwa Njia ya Kawaida
    Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
  • Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kuanzisha Mazungumuzo Yenye Itatutolea Nafasi ya Kuhubiri
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2018
  • Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kuanzisha Mazungumuzo ili Kuhubiri Wakati Hatukupanga Kufanya Hivyo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Fazili
    Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
lmd somo 1

KUANZISHA MAZUNGUMUZO

Yesu iko nazungumuza na mwanamuke ku.

Yoh. 4:6-9

SOMO YA 1

Kupendezwa na Watu

Kanuni: “Upendo . . . hautafute faida zake wenyewe.”​—1 Ko. 13:4, 5.

Mambo Yenye Yesu Alifanya

Yesu iko nazungumuza na mwanamuke ku.

VIDEO: Yesu na Mwanamuke ku Kisima

1. Angalia VIDEO, ao usome Yohana 4:6-9. Kisha ufikirie maulizo yenye kufuata:

  1. Yesu alitambua nini juu ya ule mwanamuke mbele ya kuanza kuzungumuza naye?

  2. Yesu alisema: “Nipatie maji nikunywe.” Juu ya nini ile ilikuwa njia ya muzuri ya kuanzisha mazungumuzo?

Mufano wa Yesu Unatufundisha Nini?

2. Mazungumzo yetu itakuwa ya muzuri kama tunaanza na habari yenye inafurahisha musikilizaji.

Umuige Yesu

3. Ujipatanishe na hali. Usianze mazungumzo vile tu weye ulipanga mu akili. Uanze na habari ya sasa yenye wengine wako wanafikiria. Ujiulize hivi:

  1. ‘Kuko habari gani za sasa?’

  2. ‘Ni habari gani njo majirani wangu, wafanyakazi wenzangu, na wanafunzi wenzangu wako nazungumuzia?’

4. Ukuwe muangalifu. Ujiulize hivi:

  1. ‘Huyu mutu iko nafanya nini? Pengine iko nawaza nini?’

  2. ‘Namna alishavala, namna anaonekana, na pia nyumba yake vinaonyesha nini juu ya imani yake na desturi yake?’

  3. ‘Itakuwa muzuri kama naongea naye hii saa?’

5. Usikilize.

  1. Usiseme mambo mingi.

  2. Umusaidie mwenye uko naongea naye ajisikie huru kusema mawazo yake. Kama ni muzuri umuulize maulizo.

ONA PIA

Mt. 7:12; 1 Ko. 9:20-23; Flp. 2:4; Yak. 1:19

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine