Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • bt sura 7 uku. 52-59
  • Kutangaza “Habari Njema juu ya Yesu”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kutangaza “Habari Njema juu ya Yesu”
  • “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Wale Wenye Walikuwa Wametawanywa” (Mdo. 8:4-8)
  • “Munipatie Mimi Pia Mamlaka Hii” (Mdo. 8:9-25)
  • “Kweli Unajua Mambo Yenye Unasoma?” (Mdo. 8:26-40)
  • Onyesha Roho ya Upainia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Ulijua?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Kuzungumuza kwa Njia ya Kawaida
    Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
  • “Ningewezaje . . . nisipoongozwa na mtu?”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
Ona Habari Zaidi
“Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
bt sura 7 uku. 52-59

SURA YA 7

Kutangaza “Habari Njema Juu ya Yesu”

Filipo mweneza-injili alituwekea mufano muzuri

Inategemea Matendo 8:4-40

1, 2. Kujaribu kuzuia Wakristo kuhubiri habari njema kulikuwa na matokeo gani yenye haikutazamiwa?

MVUA ya mateso inaanza, na Sauli anaanza “kushambulia” kutaniko; mu luga ya kwanza-kwanza neno kushambulia iko na maana ya kutendea mutu kwa ukali sana. (Mdo. 8:3) Wanafunzi wanakimbia, na inaonekana kama kusudi ya Sauli ya kumaliza kabisa Wakristo itatimia. Lakini, kutawanyika kwa Wakristo kunatokeza jambo fulani yenye haitazamiwe. Kunatokeza nini?

2 Wale wenye wametawanyika wanaanza ‘kutangaza habari njema ya lile neno’ mu maeneo kwenye walikimbilia. (Mdo. 8:4) Waza kidogo! Ile mateso inashindwa kuzuia Wakristo waache kutangaza habari njema, na zaidi ya ile inasaidia habari njema ifike fasi za mingi! Kwa kutawanya wanafunzi, bila kupenda wapinzani wao wamesaidia habari njema ya Ufalme ifike mu maeneo ya mbali. Sawa vile tutaona, jambo ya vile imetokea pia mu wakati wetu.

“Wale Wenye Walikuwa Wametawanywa” (Mdo. 8:4-8)

3. (a) Filipo alikuwa nani? (b) Samaria haikukuwa imehubiriwa sana, lakini Yesu alitabiri nini juu ya Samaria?

3 Filipo alikuwa kati ya “wale wenye walikuwa wametawanywa.”a (Mdo. 8:4; ona kisanduku “Filipo ‘Mweneza-injili.’”) Alienda Samaria, kwenye watu wengi hawakukuwa wamehubiriwa juu wakati fulani Yesu alipatiaka mitume wake hii maagizo: “Musiingie katika muji wowote wa Wasamaria; lakini tofauti na hilo, muende tu kwa kondoo wenye kupotea wa nyumba ya Israeli.” (Mt. 10:5, 6) Lakini, Yesu alijua kama, kuko wakati wenye habari njema ingehubiriwa sana mu Samaria, juu mbele apande mbinguni, alisema hivi: “Mutakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, katika Yudea yote na Samaria, na mupaka kwenye sehemu ya mbali zaidi ya dunia.”​—Mdo. 1:8.

4. Wasamaria walitenda namna gani wakati Filipo aliwahubiria, na pengine juu ya nini walitenda vile?

4 Filipo aliona kama Samaria ilikuwa ‘mweupe kwa ajili ya kuvunwa.’ (Yoh. 4:35) Ujumbe wake ulikuwa kitulizo kwa watu wenye kuishi Samaria, na ile inaeleweka. Juu ya nini? Wayahudi hawakukuwa wanajiunga na Wasamaria, na hata walionyesha kama wanawachukia. Lakini, Wasamaria waliona kama ujumbe wa habari njema ulitolea watu wote tumaini bila ubaguzi, na ile ilikuwa tofauti kabisa na mawazo ya Wafarisayo wenye ubaguzi. Juu Filipo aliwahubiria Wasamaria kwa bidii bila ubaguzi, ile ilionyesha kama hakukuwa na ubaguzi sawa vile watu wenye walikuwa nawachukia. Njo maana, haishangaze kuona kama Wasamaria wengi sana walimusikiliza Filipo “kwa umoja.”​—Mdo. 8:6.

5-7. Leta mifano yenye kuonyesha namna kutawanyika kwa Wakristo kulisaidia habari njema ifike fasi mingi.

5 Sawa vile mu karne ya kwanza, leo pia mateso haiyafanya watu wa Mungu waache kuhubiri. Mara kwa mara, wakati Wakristo wanalazimishwa kuenda fasi ingine sawa vile mu gereza ao mu inchi ingine, ile inawapatia nafasi ya kuhubiria watu wa kule habari njema ya Ufalme. Kwa mufano, wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu, Mashahidi wa Yehova walipata nafasi ya kuhubiria wengine mu kambi za mateso za Wanazi. Muyahudi fulani mwenye alikutana na Mashahidi wa Yehova mu kambi ya mateso alisema hivi: “Musimamo wa wafungwa Mashahidi wa Yehova ulinisadikisha kama imani yao ilitegemea Maandiko, na miye nikafikia kuwa Shahidi wa Yehova.”

6 Mu hali fulani, hata wale wenye walikuwa natesa Mashahidi walisikia habari njema na wakaikubali. Kwa mufano, wakati Shahidi mwenye kuitwa Franz alipelekwa mu kambi ya mateso ya Gusen mu inchi ya Austria, aliweza kujifunza Biblia na ofisa fulani wa SS. Wazia furaha ya wale wanaume wawili wakati walikutana ku mukusanyiko wa Mashahidi wa Yehova na wote wawili walikuwa wahubiri wa habari njema!

7 Jambo ya vile ilitokea wakati mateso ilifanya Wakristo wakimbilie mu inchi zingine. Kwa mufano, mu miaka ya 1970, ushahidi mukubwa ulitolewa Mozambique wakati Mashahidi wa Malawi walilazimika kukimbilia kule. Hata wakati upinzani ulitokea Mozambique, kazi ya kuhubiri iliendelea. Francisco Coana anasema hivi: “Ni kweli kwamba, wamoja kati yetu walikamatwa mara mingi juu ya kazi ya kuhubiri. Lakini, wakati tuliona namna watu wengi walikuwa nakubali habari njema ya Ufalme, tulikuwa hakika kama Mungu alikuwa natusaidia sawa vile alisaidiaka Wakristo wa kwanza-kwanza.”

8. Matatizo ya kupata feza na mabadiliko mu mambo ya politike imekuwa na matokeo gani juu ya kazi ya kuhubiri?

8 Lakini, haiko mateso tu njo ilisaidia habari njema ifike mu maeneo ya mingi. Mu miaka yenye imepita, matatizo ya kupata makuta na mabadiliko mu mambo ya politike imefanya watu wenye kuzungumuza luga mbalimbali na wenye kutoka mu inchi mbalimbali wapate nafasi ya kusikiliza habari njema ya Ufalme. Vita na matatizo ya kupata makuta imefanya watu fulani wahamie mu inchi zingine kwenye kuwa maisha ya muzuri zaidi, na kule wameanza kujifunza Biblia. Pia tumepata nafasi ya kuhubiri mu luga zingine mu maeneo yenye kuwa na wakimbizi wengi. Uko najikaza kuhubiria watu “kutoka mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na luga” mu eneo yenu?​—Ufu. 7:9.

“Munipatie Mimi Pia Mamlaka Hii” (Mdo. 8:9-25)

Simoni mwenye alikuwa muchawi zamani anakarbia mutume na makuta. Ule mutume iko naweka mikono yake ku mabega ya mwanaume fulani Mukristo. Nyuma, mwanaume mwingine Mukristo iko naponyesha kijina mwanamuke kilema na watu wenye kuangalia wanafurahi.

“Sasa wakati Simoni aliona kwamba watu walikuwa wanapokea roho wakati mitume walikuwa wanaweka mikono juu yao, akawapatia feza.”​—Matendo 8:18

9. Simoni alikuwa nani, na nini njo ilifanya apendezwe na Filipo?

9 Filipo alifanya miujiza ya mingi Samaria. Kwa mufano, aliponyesha watu wenye walikuwa na ulemavu na alifukuza pepo wachafu. (Mdo. 8:6-8) Mutu fulani alishangazwa sana na uwezo wa kufanya miujiza wenye Filipo alikuwa nao. Ule mutu aliitwa Simoni, mwanaume mwenye kufanya uchawi mwenye aliheshimiwa sana mupaka watu walikuwa nasema hivi juu yake: “Mutu huyu ndiye Nguvu za Mungu.” Lakini sasa Simoni alijionea nguvu za kweli za Mungu kupitia miujiza yenye Filipo alifanya. Kwa hiyo Simoni akakuwa Mukristo. (Mdo. 8:9-13) Lakini, kisha wakati fulani jambo fulani ilitokea yenye ingeonyesha sababu yenye pengine ilimuchochea kuwa Mukristo. Ni jambo gani?

10. (a) Petro na Yohana walifanya nini mu Samaria ? (b) Simoni alifanya nini wakati aliona wanafunzi wapya wanapata roho takatifu wakati Petro na Yohana waliweka mikono juu yao?

10 Wakati mitume walisikia juu ya ongezeko yenye ilikuwa kule Samaria, walituma Petro na Yohana. (Ona kisanduku “Petro Anatumia ‘Funguo za Ufalme.’”) Wakati wale mitume wawili walifika Samaria, waliweka mikono yao juu ya wale wanafunzi wapya, na kila mumoja wao akapokea roho takatifu.b Wakati Simoni aliona vile, akabakia kinywa wazi. Akaambia mitume hivi: “Munipatie mimi pia mamlaka hii, ili mutu yeyote mwenye nitaweka mikono juu yake apokee roho takatifu.” Na hata aliwaambia kama atawapatia makuta. Aliwaza kama anaweza kuuza ule uwezo wenye ulitoka kwa Mungu!​—Mdo. 8:14-19.

11. Petro alishauria Simoni afanye nini, na Simoni alitenda namna gani?

11 Bila kuenda huku na huku Petro alijibia Simoni hivi: “Feza zako ziangamie pamoja na wewe, kwa sababu uliwaza kama unaweza kupata zawadi ya bure ya Mungu kupitia feza. Wewe hauna sehemu ao fungu katika jambo hili, kwa maana moyo wako hauko wenye kunyooka mbele ya macho ya Mungu.” Kisha Petro akamushauria Simoni atubu na kusali ili Yehova amusamehe. Alimuambia hivi: “Umulilie Yehova, ili ikiwezekana, usamehewe nia mubaya ya moyo wako.” Inaonekana Simoni hakukuwa mutu mubaya; alipenda kufanya mambo ya muzuri, lakini hakukuwa naelewa mambo muzuri. Kwa hiyo, aliwaambia mitume hivi: “Mumulilie Yehova kwa ajili yangu ili nisipatwe na jambo hata moja kati ya mambo yenye mulisema.”​—Mdo. 8:20-24.

12. Tabia ya kuuza na kuuzisha vyeo imeenea kwa kadiri gani kati ya Wakristo wa uongo?

12 Karipio yenye Petro alipatia Simoni ni onyo kwa Wakristo leo. Mu luga za mingi, neno yenye kutumiwa ili kuzungumuzia tabia ya kuuza na kuuzisha vyeo, zaidi sana mu mambo ya dini, inatokana na jina “Simoni.” Mu historia ya Wakristo wa uongo muko mifano mingi ya ile tabia ya kuuza na kuuzisha vyeo. Na hata toleo ya kenda ya kitabu Encyclopædia Britannica (1878) inasema hivi: “Wakati tunachunguza historia ya uchaguzi wa Mapapa, inaonekana wazi kama mu kila uchaguzi munakuwaka ile tabia ya kuuza na kuuzisha vyeo, tena wanaifanyaka bila haya na waziwazi.”

13. Ni njia gani mbalimbali za kuuza na kuuzisha madaraka zenye Wakristo wanapaswa kuepuka?

13 Wakristo wanapaswa kuepuka ile zambi ya kuuza na kuuzisha vyeo. Kwa mufano, haupaswe kujaribu kujipendekeza kwa wale wenye kuwa na madaraka kwa kuwapatia zawadi ao kwa kuwasifu-sifu ili tu upewe mapendeleo fulani. Na wale wenye kuwa na madaraka wanapaswa kuepuka kupendelea wale wenye kuwa matajiri. Mu zile hali zote kufanya vile ni kutafuta kuuza ao kuuzisha madaraka. Kweli, watumishi wote wa Mungu wanapaswa kujiendesha kama ‘wadogo zaidi,’ na kungojea roho takatifu ya Yehova njo iwachague ili watumikie mapendeleo fulani. (Lu. 9:48) Mu tengenezo ya Yehova hamuna fasi kwa ajili ya watu wenye wanajaribu ‘kujitafutia utukufu wao wenyewe.’​—Mez. 25:27.

PETRO ANATUMIA “FUNGUO ZA UFALME”

Yesu alimuambia hivi Petro: “Nitakupatia funguo za Ufalme wa mbinguni.” (Mt. 16:19) Yesu alimaanisha nini? Wakati alizungumuzia “funguo,” alipenda kumaanisha kama Petro angefungulia vikundi mbalimbali vya watu nafasi ya kupata ujuzi na kuingia mu Ufalme wa Kimasiya. Petro alitumia zile funguo wakati gani?

  • Petro alitumia funguo ya kwanza ku Pentekoste ya mwaka wa 33 K.K.Y. wakati aliomba Wayahudi na wageuzwa-imani watubu na kubatizwa. Watu 3000 walifanya vile na wakakuwa na tumaini ya kutawala katika Ufalme.​—Mdo. 2:1-41.

  • Petro alitumia funguo ya pili muda mufupi kisha Stefano kuuawa kwa sababu ya imani yake. Mu ile wakati, Petro na Yohana waliweka mikono juu ya Wasamaria wenye walitoka kubatizwa, kisha pale wale waamini wapya wakapokea roho takatifu.​— Mdo. 8:14-17.

  • Petro alitumia funguo ya tatu mu 36 K.K.Y. Mu ile mwaka, alisaidia Watu wa Mataifa wenye walikuwa hawatahiriwe wakuwe na tumaini ya kutawala mbinguni. Alifanya vile wakati alitolea ushahidi Kornelio, Mutu wa Mataifa wa kwanza mwenye hatahiriwe mwenye alifikia kuwa Mukristo.​—Mdo. 10:1-48.

“Kweli Unajua Mambo Yenye Unasoma?” (Mdo. 8:26-40)

14, 15. (a) “Towashi Mwetiopia” alikuwa nani, na Filipo alimupata namna gani? (b) Ule Mwetiopia alitenda namna gani wakati alisikia ujumbe wa Filipo, na juu ya nini hatuwezi kusema kama alibatizwa haraka bila kufikiri? (Ona maelezo ya chini.)

14 Sasa malaika wa Yehova anaambia Filipo aende kwenye barabara yenye kutoka Yerusalemu kuenda Gaza. Pengine Filipo alijiuliza juu ya nini, lakini bila kukawia anapata jibu wakati anakutana na towashi Mwetiopia mwenye alikuwa ‘anasoma kwa sauti kubwa nabii Isaya.’ (Ona kisanduku “‘Towashi’ mu Maana Gani?”) Roho takatifu ya Yehova ilimuongoza Filipo akaribie gari ya ule mwanaume. Na wakati alikuwa anakimbia pembeni-pembeni ya ile gari alimuuliza hivi ule mwanaume Mwetiopia: “Je, kweli unajua mambo yenye unasoma?” Na ule mwanaume Mwetiopia akajibia hivi: “Ninaweza kujua namna gani kama mutu fulani haniongoze?”​—Mdo. 8:26-31.

15 Ule mwanaume akamuomba Filipo apande mu gari yake. Bila shaka walikuwa na mazungumuzo yenye kufurahisha! Kwa miaka mingi watu hawakujua ikiwa “kondoo,” ao “mutumishi” mwenye kuzungumuziwa mu unabii wa Isaya ni nani. (Isa. 53:1-12) Lakini, wakati Filipo alikuwa nasafiri na towashi Mwetiopia alimufasiria kama ni Yesu Kristo njo alitimiza ule unabii. Sawa tu wale wenye walibatizwa ku Pentekoste ya mwaka wa 33 K.K.Y., ule Mwetiopia, mwenye tayari alikuwa mugeuzwa-imani, alijua palepale jambo yenye alipaswa kufanya. Aliambia hivi Filipo: “Angalia! Hapa kuko maji; ni kitu gani kinanizuia nisibatizwe?” Bila kukawia Filipo akamubatiza ule Mwetiopia!c (Ona kisanduku “Kubatizwa ‘Katika Maji.’”) Kisha pale, roho ya Mungu iliongoza Filipo mu mugao ingine kule Ashdodi, kwenye aliendelea kutangaza habari njema.​—Mdo. 8:32-40.

“TOWASHI” MU MAANA GANI?

Neno ya Kigiriki eu·nouʹkhos, yenye inatafsiriwa “towashi,” inaweza kumaanisha mwanaume mwenye hana uwezo wa kuzaa ao mutu mwenye iko na mamlaka mu nyumba ya mufalme. Inawezekana maofisa wenye walisimamia nyumba ya bibi za mufalme waliharibiwa viungo vyao vya uzazi, lakini haikukuwa lazima kufanya vile maofisa wengine wa mufalme, sawa vile ofisa mwenye kuletea mufalme divai ao mwenye kuchunga hazina zake. Inaonekana towashi Mwetiopia mwenye Filipo alibatiza alikuwa na cheo ya vile juu alikuwa nasimamia hazina mu nyumba ya kifalme. Ni kusema, alikuwa waziri wa mambo ya feza.

Ule Mwetiopia alikuwa pia mugeuzwa-imani, ni kusema mutu wa mataifa mwenye alikuwa anamuabudu Yehova. Na hata, alikuwa anatoka Yerusalemu ili kuabudu. (Mdo. 8:27) Kwa kufikiria ile mambo yote, tunaweza kusema kama ule Mwetiopia hakukuwa towashi kimwili, juu Sheria ya Musa ilikataza mwanaume mwenye alifanywa kuwa towashi kuingia katika kutaniko la Israeli.​—Kum. 23:1.

KUBATIZWA “KATIKA MAJI”

Ubatizo wa Kikristo unafanywa namna gani? Watu fulani wanawaza kama inatosha tu kumwangia mutu maji kidogo ku kichwa. Lakini towashi Mwetiopia alibatizwa ndani ya “maji.” Kitabu ya Matendo inasema hivi: “Wote wawili Filipo na towashi wakaingia ndani ya maji.” (Mdo. 8:36, 38) Kama ilitosha kumwangia mutu maji kidogo tu ku kichwa, haingeomba ule towashi asimamishe gari yake kwenye kuko maji. Hata maji kidogo, kwa mufano yenye kuwa mu chupa, ingetosha. Inawezekana alikuwa na chupa ya maji, juu alikuwa anasafiri mu “barabara yenye kupita katika jangwa.”​—Mdo. 8:26.

Kulingana na kitabu A Greek-English Lexicon, yenye ilitolewa na Liddell na Scott, neno ya Kigiriki ba·ptiʹzo yenye inatafsiriwa katika Kiswahili “ubatizo” inamaanisha “kutumbukiza, kuingiza ndani.” Mambo yenye Biblia inasema juu ya ubatizo inapatana na ile mafasirio. Yohana 3:23 inasema kama Yohana “alikuwa anabatiza kule Ainoni karibu na Salimu, kwa sababu kule kulikuwa maji mengi.” Vilevile, Biblia inasema hivi kuhusu ubatizo wa Yesu: “Wakati alipanda kutoka katika maji [Yesu] akaona mbingu zikifunguka.” (Mk. 1:9, 10) Kwa hiyo, Wakristo wa kweli wanabatizwa kwa kutumbukizwa kabisa ndani ya maji.

16, 17. Namna gani malaika wako wanaongoza kazi ya kuhubiri leo?

16 Leo Wakristo wako na pendeleo ya kufanya kazi ya kuhubiri sawa Filipo. Mara mingi, wanahubiriaka watu wenye wanakutana nao wakati wowote, kwa mufano wakati wako wanasafiri. Na kwa ukawaida, wanakutana na watu wenye moyo muzuri kwa sababu wanaongozwa na malaika. Biblia inaonyesha kama malaika wako wanaongoza kazi ya kuhubiri juu ujumbe wa Ufalme ufikie “kila taifa na kabila na luga na watu.” (Ufu. 14:6) Yesu alitabiri waziwazi kama malaika wangeongoza kazi ya kuhubiri. Mu mufano wake wa ngano na magugu, Yesu alisema kama mu kipindi ya mavuno, ni kusema mu siku za mwisho, “wavunaji ni malaika.” Alisema pia kama malaika “watakusanya kutoka katika Ufalme wake vitu vyote vyenye vinafanya watu wakwazike na pia watu wenye matendo ya kuvunja sheria.” (Mt. 13:37-41) Wakati uleule, malaika wangekusanya wale wenye watatawala mu Ufalme mbinguni, na kisha wangekusanya “kundi kubwa” ya “kondoo wengine” wenye Yehova anapenda kuvuta mu tengenezo yake.​—Ufu. 7:9; Yoh. 6:44, 65; 10:16.

17 Watu wengi wenye tunakutana nao mu kazi ya kuhubiri wamesema kama walikuwa nasali ili Mungu awasaidie. Ile inaonyesha kama malaika wako naongoza kazi ya kuhubiri. Kwa mufano, siku moya wahubiri wawili walikuwa mu mahubiri na mutoto mudogo. Wakati wale wahubiri walitaka kumaliza mahubiri yao ya asubui, ule mutoto alipenda sana kuenda ku nyumba ya kufuata, na hata alienda yeye peke na kugonga ku mulango! Wakati kijana mwanamuke alifungula mulango, wale Mashahidi wawili walimukaribia na kuzungumuza naye. Na walishangala wakati ule mwanamuke aliwaambia kama alikuwa anasali na kuomba mutu fulani akuye kumutembelea na kumusaidia kuelewa Biblia. Kisha ule mwanamuke akaanza kujifunza Biblia!

Mu mahubiri bibi na bwana wako napiga kengele ya mulango ya nyumba ya mwanamuke fulani wakati ule mwanamuke iko nasali.

“Mungu, kama unakuwaka kabisa, tafazali nisaidie”

18. Juu ya nini hatupaswe kuzarau hata kidogo kazi yetu ya kuhubiri?

18 Juu uko mu kutaniko ya Kikristo, uko na pendeleo ya kutumika pamoya na malaika mu kazi kubwa ya kuhubiri yenye iko nafanyika leo mu namna yenye haiyafanyikaka. Usizarau hata kidogo ile pendeleo. Kama unaendelea kujikaza utapata furaha kubwa wakati unaendelea kutangaza “habari njema juu ya Yesu.”​—Mdo. 8:35.

FILIPO “MWENEZA-INJILI”

Wakati wafuasi wa Yesu walitawanyika kwa sababu ya mateso, Filipo alienda Samaria. Ni wazi kwamba alitumika kwa ukaribu na baraza yenye kuongoza ya karne ya kwanza, juu “wakati mitume katika Yerusalemu walisikia kwamba Samaria ilikuwa imekubali neno la Mungu, wakatuma kwao Petro na Yohana.” Matokeo ilikuwa nini? Waamini wapya wenye walikuwa kule walipokea zawadi ya bure ya roho takatifu.​—Mdo. 8:14-17.

Filipo anaikala mugari pamoya na Toashi Mwetiopia.

Kisha matukio yenye kuzungumuziwa mu Matendo sura ya 8, Filipo anazungumuziwa tena mara moya tu. Miaka 20 hivi kisha mahubiri ya kwanza ya Filipo, mutume Paulo na wenzake walikuwa nasafiri kuenda Yerusalemu ku mwisho wa safari ya tatu ya umisionere ya Paulo. Paulo na wenzake walisimama Tolemai. Luka anaeleza hivi: “Siku yenye ilifuata tukatoka na kufika Kaisaria, na tukaingia katika nyumba ya Filipo mweneza-injili, mwenye alikuwa mumoja wa wale wanaume saba (7), na tukakaa pamoja naye. Mutu huyo alikuwa na mabinti ine (4) wenye walikuwa hawajaolewa, na walikuwa wanatoa unabii.”​—Mdo. 21:8, 9.

Inaonekana kama, Filipo alibakia mu eneo yenye alipewa ili kuhubiri na sasa alikuwa na familia. Kuona kama Luka anamuita “mweneza-injili,” inatufundisha jambo ya maana juu yake. Maandiko inatumia ile neno ili kuzungumuzia watu wenye wanaacha nyumba zao ili kuenda kuhubiri habari njema mu maeneo yenye haiyahubiriwa. Bila shaka, Filipo alikuwa angali na bidii sana kwa ajili ya mahubiri. Na juu watoto wake ine wanamuke walikuwa natoa unabii, ile inaonyesha waziwazi kama Filipo alifundisha familia yake kumupenda na kumutumikia Yehova.

a Filipo mwenye kuzungumuziwa hapa haiko mutume Filipo. Lakini ni Filipo mwenye, sawa vile Sura ya 5 ya hii kitabu inaonyesha, alikuwa kati ya wale ‘wanaume saba (7) wenye walijulikana kuwa na sifa za muzuri,’ wenye waliwekwa ili kusimamia kazi ya kugabulia chakula wale wajane wenye walikuwa nazungumuza Kigiriki na wenye walikuwa nazungumuza Kiebrania katika Yerusalemu.​—Mdo. 6:1-6.

b Inaonekana kwamba, ile wakati kwa kawaida wanafunzi wapya walikuwa wanapokea roho takatifu wakati wanabatizwa. Ile ilikuwa nawapatia tumaini ya kutawala wakiwa wafalme na makuhani pamoja na Yesu kule mbinguni. (2 Ko. 1:21, 22; Ufu. 5:9, 10; 20:6) Lakini, mu hii hali wanafunzi hawakupokea roho takatifu wakati walibatizwa. Ni kisha tu Petro na Yohana kuweka mikono juu ya wale wanafunzi wapya njo walipokea roho takatifu na uwezo wa kufanya miujiza wenye ulitokana na roho takatifu.

c Ule haukukuwa ubatizo wa haraka-haraka na wa bila kufikiri. Juu ule Mwetiopia alikuwa mugeuzwa-imani, alikuwa najua muzuri Maandiko, kutia ndani maunabii mbalimbali juu ya Masiya. Na juu sasa alikuwa ameelewa daraka ya Yesu katika kusudi ya Mungu, angeweza kubatizwa bila kukawia.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine