Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 6/00 uku. 4
  • “Ningewezaje . . . nisipoongozwa na mtu?”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Ningewezaje . . . nisipoongozwa na mtu?”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tazamo Linalosonga Mbele Juu Ya Kazi Ya Haraka Ya Kufanya Wanafunzi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Jinsi Ya Kufanya Wanafunzi Kwa Msaada Wa Kitabu Ujuzi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Pili
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Kwanza
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 6/00 uku. 4

“Ningewezaje . . . nisipoongozwa na mtu?”

1 Wakati mweneza-evanjeli Filipo alipomwuliza towashi Mwethiopia ikiwa alielewa yale aliyokuwa akisoma kutoka katika Neno la Mungu, mwanamume huyo alijibu: “Ningewezaje kusikia, nisipoongozwa na mtu?” Kwa furaha, Filipo alimsaidia kuelewa habari njema kuhusu Yesu; tokeo lilikuwa kubatizwa kwa mara moja kwa mwanamume huyo. (Mdo. 8:26-38, Agano Jipya) Filipo alikuwa akitii amri ya Kristo ya ‘kufanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, kuwabatiza na kuwafundisha.’—Mt. 28:19, 20.

2 Tunapaswa kutii amri ya kufanya wanafunzi, kama vile tu alivyofanya Filipo. Hata hivyo, aina ya maendeleo ya kiroho ya haraka aliyofanya towashi Mwethiopia mara nyingi hayaonekani kwa watu tunaojifunza Biblia pamoja nao. Mwanamume huyo, mwongofu wa dini ya Kiyahudi aliyejua sana Maandiko, alikuwa na moyo wenye kuitikia vizuri, naye alihitaji tu kukubali kwamba Yesu alikuwa ndiye Masiya aliyeahidiwa. Ni tatizo ikiwa wale tunaojifunza nao hawajui Biblia, ikiwa wamedanganywa na mafundisho ya kidini ya uwongo, au ikiwa wanalemewa na matatizo mazito ya kibinafsi. Ni nini litakalotusaidia kuwa wenye matokeo katika kuongoza wanafunzi wa Biblia kwenye wakfu na ubatizo?

3 Tambua mahitaji ya kiroho ya mwanafunzi wa Biblia: Nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Septemba 1998 ilizungumzia urefu wa wakati tunaopaswa kufanya tunapojifunza na watu, tukitumia broshua Anataka na kitabu Ujuzi. Ilitoa mwongozo ufuatao: “Inatubidi kukadiria mwendo wa funzo kulingana na hali na uwezo wa mtu tunayejifunza naye. . . . Hatupendi kupoteza uelewevu mzuri wa mwanafunzi kwa ajili ya kwenda haraka. Kila mtu anayejifunza anahitaji imani yake mpya katika Neno la Mungu ijengwe juu ya msingi imara.” Kwa hiyo, ni vizuri kutoenda haraka-haraka na habari katika kitabu Ujuzi kwa sababu ya wazo la kujaribu kumaliza kitabu kwa muda wa miezi sita. Huenda ikaomba zaidi ya miezi sita ili kusaidia watu fulani kufanya maendeleo kufikia ubatizo. Kadiri unavyoongoza funzo juma baada ya juma, tumia wakati wowote unaohitajiwa ili kusaidia mwanafunzi aelewe na kukubali yale anayojifunza kutoka katika Neno la Mungu. Katika hali fulani, huenda majuma mawili au matatu yakahitajiwa ili kumaliza sura moja katika kitabu Ujuzi. Hilo litafanya kuwe na wakati wa kusoma na kueleza maandiko mengi yanayotajwa.—Rom. 12:2.

4 Hata hivyo, namna gani ikiwa baada ya kumaliza kitabu Ujuzi, unatambua kwamba uelewevu wa kweli wa mwanafunzi unahitaji kukamilishwa au kwamba hajachochewa kikamili kuchukua msimamo kwa ajili ya kweli na kuweka maisha yake wakfu kwa Mungu? (1 Kor. 14:20) Ni jambo gani lingine unaloweza kufanya ili kumwongoza kwenye njia iongozayo kwenye uhai?—Mt. 7:14.

5 Tosheleza mahitaji ya kiroho ya mwanafunzi wa Biblia: Ikiwa ni wazi kwamba mtu anafanya maendeleo, ingawa ni ya polepole, na kwamba ni mwenye kukomaza uthamini kwa yale anayojifunza, basi endelea na funzo la Biblia katika kitabu cha pili baada ya kumaliza broshua Anataka na kitabu Ujuzi. Huenda hilo lisiwe jambo la lazima katika kila hali, lakini inapohitajika, endelea na funzo katika kitabu Amani ya Kweli, kitabu Wenye Umoja Katika Ibada, au kitabu Neno la Mungu. Wahubiri wengi wana nakala zao binafsi za vitabu hivyo wanazoweza kutumia ikiwa kutaniko halina navyo. Kitabu Neno la Mungu tu ndicho kinaweza kuagizwa. Kwa vyovyote, funzo linapaswa kufanywa kwanza katika broshua Anataka na kitabu Ujuzi. Funzo la Biblia, ziara za kurudia, na wakati unaopitishwa ili kuendeleza funzo vingepaswa kuhesabiwa na kuripotiwa, hata ikiwa mwanafunzi anabatizwa mbele ya kumaliza kitabu cha pili.

6 Je, hilo linamaanisha kwamba wale ambao walibatizwa juzi-juzi lakini ambao walijifunza tu kitabu kimoja wanapaswa sasa kupokea msaada unaorudiliwa upya ili kujifunza kitabu cha pili? Si lazima. Hata hivyo, huenda ikawa wamekuwa wasiotenda au kwamba hawakufanya maendeleo katika kweli, na huenda wakaona kwamba wanahitaji msaada wa kibinafsi ili kufanya matumizi makubwa zaidi ya kweli katika maisha zao. Mwangalizi wa utumishi anapaswa kuulizwa mbele ya funzo kuanzishwa upya pamoja na mhubiri aliyebatizwa. Hata hivyo, ikiwa mnajua watu fulani ambao walijifunza kitabu Ujuzi wakati uliopita lakini hawakufanya maendeleo kufikia wakfu na ubatizo, mnaweza kutaka kufanya hatua ya kwanza ili kuona ikiwa wanaweza kurudilia tena funzo lao la Biblia.

7 Ni alama ya upendo wa Kikristo kutoa uangalifu wa karibu na wa kibinafsi kwa kila mtu mwenye kupendezwa tunayejifunza naye. Mradi wetu ni kusaidia mwanafunzi apate ufahamu mkubwa zaidi wa kweli ya Neno la Mungu. Ndipo anaweza kuchukua msimamo kamili na wenye ujuzi kwa ajili ya kweli na kuweka maisha yake wakfu kwa Yehova, akionyesha wakfu huo kupitia ubatizo wa maji.—Zab. 40:8; Efe. 3:17-19.

8 Je, unakumbuka lililotukia baada ya yule towashi Mwethiopia kubatizwa? “Akaongeza safari yake kwa furaha” akiwa mwanafunzi mpya wa Yesu Kristo. (Mdo. 8:39, 40; AJ) Acheni sisi na wale tunaoongoza kwa matokeo katika njia ya kweli tupate furaha kubwa katika kumtumikia Yehova Mungu—sasa na milele!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine