Tazamo Linalosonga Mbele Juu Ya Kazi Ya Haraka Ya Kufanya Wanafunzi
1 Kabla ya kuondoka duniani, Yesu aliamuru wafuasi wake ‘wafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote.’ Hilo liliomba kwamba waanzishe kampeni kubwa ya kuhubiri na kufundisha na kupanua utendaji wao katika dunia yote inayokaliwa. (Mt. 28:19, 20; Mdo. 1:8) Je! waliona utume wao kuwa mzigo mzito sana kuchukua? Si kulingana na mtume Yohana. Baada ya miaka 65 iliyopitishwa katika kufanya wanafunzi, yeye aliandika: “Hivi ndivyo kumpenda Mungu humaanisha, kwamba tushike amri zake; na bado amri zake si zenye kulemea.”—1 Yn. 5:3.
2 Maelezo ya Kimaandiko ya utendaji wa Wakristo wa mapema yanathibitisha kwamba walitimiza kwa bidii utume wao wa kufanya wanafunzi wa Yesu Kristo. (2 Tim. 4:1, 2) Hawakufanya hivyo kwa sababu ya wajibu tu; ni upendo uliowasukuma kumsifu Mungu na kutoa tumaini la wokovu kwa wengine. (Mdo. 13:47-49) Kwa kuwa wale wote waliokuwa wakigeuka kuwa wanafunzi walikuwa wakifanya wanafunzi wao wenyewe baadaye, kutaniko la Kikristo la karne ya kwanza lilikua kwa uharaka.—Mdo. 5:14; 6:7; 16:5.
3 Kazi ya Kufanya Wanafunzi Yazidisha Mwendo: From EnglishKazi kubwa zaidi ya kufanya wanafunzi ni yenye kutimizwa katika karne hii ya 20 kuliko wakati wowote ule! Hadi sasa, mamilioni ya watu wamekubali habari njema na kutenda kuhusiana na hiyo. (Lk. 8:15) Kwa kuwa wakati wenye kubaki wa mfumo huu wa mambo ni wenye kwenda mbio, “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” hutuandalia vifaa ambavyo vitafanya iwezekane kwa watu wanyofu kujifunza kweli haraka.—Mt. 24:45.
4 Katika 1995 tulipokea kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, kikifuatwa, katika 1996, na broshua Mungu Anataka Nini Kwetu? Kuhusu kitabu Ujuzi, Mnara wa Mlinzi wa Januari 15, 1996, ukurasa 14, ulisema: “Mafunzo ya kitabu hiki cha kurasa 192 yaweza kuchukua wakati mfupi kwa kulinganisha, na wale ‘wenye mwelekeo ufaao kwa ajili ya uhai udumuo milele’ watazamiwa kuweza kujifunza vya kutosha kupitia funzo la kitabu hicho ili wajiweke wakfu kwa Yehova na kubatizwa.”—Mdo. 13:48.
5 Nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 1996, “Jinsi ya Kufanya Wanafunzi kwa Msaada wa Kitabu Ujuzi,” ilitutolea mradi huu: “Kulingana na hali na uwezo wa akili wa mwanafunzi, labda itawezekana kuchunguza sura fulani nyingi kwa somo moja tu muda wa saa moja hivi, bila hata hivyo kwenda haraka haraka na funzo. Wanafunzi watafanya maendeleo zaidi ikiwa mwalimu na wao wenyewe wanaheshimu siku ya kukutana kwa ajili ya funzo kila juma.” Makala iliendelea kusema: “Inatazamiwa kwamba mtu anayefika mwisho wa funzo la kitabu Ujuzi awe ameonyesha waziwazi unyofu wake na tamaa yake ya kina kirefu ya kutumikia Mungu.” Kisanduku “Majibu kwa Maulizo Yenu” katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Novemba 1996 kilifasiria: “Ni jambo la akili kufikiri kwamba katika hali za kawaida, mwalimu mwenye matokeo ataweza, kwa muda mfupi, kumsaidia mwanafunzi mnyofu kufanya maendeleo ya kutosha ili kuamua kumtumikia Yehova kutokana na yale anayojua.”
6 Kitabu Ujuzi Chatoa Matokeo: Wakati wa ubatizo wake, mwanamke mmoja kijana alieleza jinsi alivyohisi kuhusu kujifunza kitabu Ujuzi. Kwa wakati fulani alikuwa akijifunza kitabu Kuishi Milele. Wakati kitabu Ujuzi kilipotokea, dada aliyekuwa akiongoza funzo alikitumia badala ya kile kingine. Punde si punde, mwanafunzi aliona kwamba hilo lingemwongoza kuchukua uamuzi, naye alichochewa kufanya maendeleo ya haraka tangu hapo. Msichana huyo, ambaye sasa ni dada yetu, anasema: “Kitabu Kuishi Milele kilinisaidia kumpenda Yehova, lakini kitabu Ujuzi kilinisaidia nichukue uamuzi wa kumtumikia.”
7 Acheni tuone kwa uharaka gani mwanamke mwingine alijifunza kweli. Baada ya funzo la pili, alihudhuria mkutano uliofanywa kwenye Jumba la Ufalme wakati wa ziara ya mwangalizi wa mzunguko. Juma hilo, kwenye funzo lake la tatu, alimjulisha mwangalizi kwamba alikuwa amejiweka wakfu kwa Yehova na kwamba alitaka kuwa mhubiri asiyebatizwa. Baada ya kuzungumza naye, wazee walitoa kibali chao na juma lililofuata akaanza kuhubiri. Alipendezwa sana na funzo lake la Biblia hivi kwamba aliomba likizo la pekee ili kujifunza mara mbili au tatu kwa juma na kupitisha wakati mwingi zaidi katika mahubiri. Mara kwa mara, walijifunza sura mbili au tatu wakati wa funzo. Mwanamke huyo akaanza kutumikisha yote aliyojifunza katika sehemu zote za maisha yake, akamaliza kitabu Ujuzi kwa majuma manne na akaendelea hadi ubatizo!
8 Mume wa dada mmoja alijieleza mwenyewe kuwa alikuwa “kielelezo chenyewe cha mwenzi asiyeamini.” Siku moja, ndugu mmoja akamtolea funzo la Biblia katika kitabu Ujuzi, akimweleza mtu huyo kwamba angeweza kuacha funzo baada ya mazungumzo ya kwanza au wakati mwingine wowote. Mume huyo akakubali kujaribu, ingawa hakuwa mwanafunzi mzuri katika ujana wake na ingawa, kwa muda wa miaka 20, hakujifunza kichapo chochote cha kidini. Aliitikiaje funzo la kitabu Ujuzi? Alisema: “Ilikuwa furaha kwelikweli kuona kwamba katika kitabu hicho kinachosaidia kujifunza Biblia mmeandikwa mambo rahisi kama hayo. Mafundisho yalitolewa waziwazi na kwa akili hivi kwamba, baada ya wakati kidogo, nilitazamia funzo letu lenye kufuata kwa hamu. Mwalimu wangu alifuata kwa ustadi njia za kufanya wanafunzi zinazopendekezwa na Sosaiti, na kwa msaada wa roho takatifu, nilibatizwa miezi minne baada ya hapo. Ninaweza kusema kwamba ikiwa tunasitawisha upendo wa kufanya wanafunzi, ikiwa tunaendelea kutafuta watu wenye unyofu katika huduma, ikiwa tunatumia kitabu Ujuzi na vichapo vingine vinavyosaidia kujifunza Biblia vinavyoandaliwa na Sosaiti, na jambo la maana zaidi, ikiwa tunatafuta mwongozo wa Yehova katika sala, tunaweza kuwa na pendeleo la pekee la kusaidia kufanya wanafunzi.” Mambo hayo yaliyoonwa ni ya pekee. Wengi wa wanafunzi tunaojifunza nao hawaji kwenye kweli kwa uharaka kama huo.
9 Wanafunzi Hufanya Maendeleo kwa Miendo Tofauti: Inafaa kutambua kwamba uwezo wa walimu na wa wanafunzi wa Neno la Mungu unaweza kutofautiana kwa kiasi kikubwa. Ukuzi wa kiroho waweza kuwa wa polepole au wa haraka. Watu fulani hufanya, katika miezi michache, maendeleo ambayo yataomba wakati mrefu zaidi kwa wengine. Mwendo wa maendeleo ya mtu hutegemea elimu yake, uthamini wake wa mambo ya kiroho na kina cha ushikamano??? wake na Yehova. Watu wote tunaojifunza nao hawachunguzi Maandiko kila siku kwa “hamu ya akili iliyo kubwa zaidi,” kama walivyofanya watu wa Beroya waliogeuka kuwa waamini.—Mdo. 17:11, 12.
10 Hiyo ndiyo sababu nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Mei 1998, yenye kichwa “Mafunzo ya Biblia Zaidi Yanatakwa,” inatoa mwongozo ufuatao wenye kusema kweli: “Kwa kweli, si wanafunzi wote wa Biblia wanaofanya maendeleo kwa mwendo uleule. Wamoja hawapendezwi kiroho kama vile wengine wala kuwa haraka kuelewa mambo wanayojifunza. Wengine wanaishi maisha yenye shughuli sana na hawawezi kutoa wakati unaohitajika ili kumaliza sura moja kila juma. Hivyo, katika hali fulani linaweza kuwa jambo la lazima kuchukua zaidi ya kipindi kimoja cha funzo ili kumaliza sura fulani fulani na miezi ya ziada ili kumaliza kitabu.”[2]
11 Wale Wanaofanya Wanafunzi Huwa na Maoni Yenye Usawaziko: Inatubidi kukadiria mwendo wa funzo kulingana na hali na uwezo wa mtu tunayejifunza naye. Kwa kuwa tunatiwa moyo kuanza mafunzo kwa msaada wa broshua Anataka, labda itachukua miezi miwili au mitatu ili kuimaliza kabla ya kuingia katika kitabu Ujuzi. Ikiwa tunatumia madokezo yote yaliyotolewa katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 1996, itawezekana kwamba tuhitaji miezi mingine sita au tisa ili kumaliza kitabu hicho. Wengine walikuwa wameanzisha funzo katika kitabu Ujuzi, wakalikatiza ili kutumia broshua Anataka na hivyo wasaidie mtu ajifunze kweli za msingi za Biblia haraka zaidi. Kisha, wakarudilia funzo la kitabu Ujuzi. Ikiwa funzo lilianzishwa katika kitabu Ujuzi na linaendelea vizuri, linaweza kuwa jambo la akili kujifunza broshua Anataka baadaye. Jambo hilo litafanya iwezekane kurudilia haraka kweli za msingi. Katika hali zote hizo, hatupendi kupoteza uelewevu mzuri wa mwanafunzi kwa ajili ya kwenda haraka. Kila mtu anayejifunza anahitaji imani yake mpya katika Neno la Mungu ijengwe juu ya msingi imara.
12 Kwa sababu tumefika mbali katika kupita kwa wakati, ni jambo la haraka zaidi kuliko wakati mwingine wowote kusaidia wengine wajifunze kweli. Huku tukisali bila kukoma ili kuanzisha mafunzo mapya ya Biblia, acheni tusali pia kwa ajili ya wale ambao tayari tunajifunza nao. Hivyo, tutakuwa wenye furaha kuendelea kubatiza wanafunzi “siku zote hadi umalizio wa mfumo wa mambo.”—Mt. 28:20.