Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 6/96 uku. 7
  • Majibu kwa Maulizo Yenu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Majibu kwa Maulizo Yenu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jinsi Ya Kufanya Wanafunzi Kwa Msaada Wa Kitabu Ujuzi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Majibu Kwa Maulizo Yenu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Tazamo Linalosonga Mbele Juu Ya Kazi Ya Haraka Ya Kufanya Wanafunzi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Jinsi ya Kutumia Kitabu “Upendo wa Mungu” Ili Kuongoza Mafunzo ya Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 6/96 uku. 7

Majibu kwa Maulizo Yenu

◼ Kwa kuwa sasa tuna kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, ni kwa muda gani funzo la Biblia la nyumbani litaweza kuongozwa?

Huduma Yetu ya Ufalme ya Septemba 1993 ilipendekeza kuendelea na funzo la Biblia la nyumbani pamoja na mtu mpya mpaka pale vitabu viwili vitakapomalizika. Kwa kuwa sasa tunacho kitabu Ujuzi, inaonekana kuwa jambo la hekima kubadili namna hiyo ya kufanya, kulingana na yale Mnara wa Mlinzi wa Januari 15, 1996 unaonyesha kwenye kurasa 13 na 14.

Kitabu Ujuzi kimekusudiwa ili kuwasaidia wale walio katika “mwelekeo ufaao kwa ajili ya uhai udumuo milele” kujifunza yale wanayohitaji ili kujitoa wakfu kwa Yehova na kubatizwa. (Mdo. 13:​48, NW) Kwa hiyo, baada tu ya kumaliza kitabu kipya, haingekuwa lazima kujifunza kitabu cha pili. Kwa kadiri wanafunzi wetu wanavyozingatia ukweli, tunaweza hatua kwa hatua kuwatia moyo kuongeza ujuzi wao kwa kuhudhuria mikutano ya Mashahidi wa Yehova pia kwa kusoma Biblia na vichapo mbalimbali vya Kikristo.

Ingekuwa lazima sana kwamba tufahamiane kabisa na maulizo ya kurasa 175 mpaka 218 ya kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu. Hata ikiwa hatungetaja maulizo hayo au kuyachunguza pamoja na mwanafunzi, ingekuwa vizuri kwamba tukazie katika kitabu Ujuzi nukta ambazo zitamwezesha kuonyesha akili yake nzuri ya kweli za msingi za Biblia wakati wazee watakapochunguza pamoja naye maulizo kwa ajili ya ubatizo wake.

Hakuna lazima ya kuongeza juu ya habari za kitabu Ujuzi kwa kutaja habari nyingine za nje au hoja za ziada ili kukazia mafundisho ya Biblia au ili kutupilia mbali mafundisho ya uongo. Hilo lingerefusha tu funzo. Badala yake ingekuwa vizuri kwamba kitabu kimalizwe haraka, labda katika miezi sita tu. Jambo ambalo ni la muhimu kwetu kujifunza mapema na kwa undani habari, ili kuweza kuyatolea waziwazi na kwa uhakika. Mwanafunzi angepaswa pia kutiwa moyo kujitayarisha, kusoma maandiko yanayotolewa na kujikaza kuelewa yale kila sura inayofundisha.

Mnara wa Mlinzi ulitia mkazo juu ya ulazima kwa Mashahidi wa Yehova kuongoza mafunzo ya Biblia zaidi yenye matokeo kwa wakati mfupi. (Ona Isaya 60:22.) Kwa kufanya matumizi mazuri ya kitabu Ujuzi, tutaweza kuwasaidia wapya kupata ujuzi uongozao kwenye uhai udumuo milele na kushikamana nao.—Yn. 17:3.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine