Majibu Kwa Maulizo Yenu
◼ Ni kwa muda gani tungepaswa kujifunza na mtu kitabu Ujuzi?
Yehova anabariki leo watu wake. Tuna ushuhuda wa hilo kila mwaka wakati maelfu ya wapya wanasimama upande wa ukweli. Mambo ya kweli yanaonyesha kwamba kitabu Ujuzi ni chombo chenye matokeo ili kufundisha ukweli. Mnara wa Mlinzi, katika namba ya Januari 15, 1996, ulivutia uangalifu wetu juu ya jambo la kwamba kitabu hicho kimechapwa ili kusaidia mwanafunzi wa Biblia kufanya maendeleo haraka vya kutosha; labda miezi fulani itatosha ili afikie ubatizo.
Ni kwa sababu hiyo namba hiyo hiyo ya Mnara wa Mlinzi ilikazia kwenye ukurasa 17: “Baada ya mtu kumaliza funzo lake la Biblia katika kitabu Ujuzi naye amebatizwa, huenda lisiwe jambo la lazima kuongoza funzo la rasmi pamoja naye katika kitabu cha pili.”
Tutafanya nini ikiwa kitabu Ujuzi kinamalizika na kwamba mwanafunzi si tayari kwa ajili ya ubatizo? Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 1996, ukurasa 6, fungu 23, ilikumbusha shauri la Mnara wa Mlinzi kutojifunza kitabu cha pili kisha kitabu Ujuzi. Je! hilo humaanisha kwamba tunapaswa kusimamisha kumsaidia mwanafunzi kufanya maendeleo? Hapana. Tunapenda kwamba watu wapata ujuzi wa msingi wa ukweli. Hata hivyo, ni jambo la akili kufikiri kwamba katika hali za kawaida, mwalimu mwenye matokeo ataweza, kwa muda mfupi, kumsaidia mwanafunzi mnyofu kufanya maendeleo ya kutosha ili kuamua kumtumikia Yehova kutokana na yale anayojua. Inawezekana kwamba kulingana na hali zao wanafunzi fulani wanaweze kujifunza mara nyingi kwa juma.
Inafaa kukubali kwamba wanafunzi fulani hawafanyi maendeleo ya haraka kama wengine. Lakini ikiwa kisha funzo la kitabu Ujuzi, ambalo katika hali fulani linaweza kuwa kwa kiasi ndefu, mtu mpaka sasa hajaamua kujiunga na kutaniko, mhubiri atafanya vema kuzungumza swala hilo pamoja na mzee mmoja wa halmashauri ya utumishi. Ikiwa hali za pekee zinaomba hivyo, msaada wa ziada utaweza kutolewa, kulingana na kanuni inayoonyeshwa katika Mnara wa Mlinzi wa Januari 15, 1996, ukurasa 17, mafungu 11-12.
Mwanafunzi ambaye alisaidiwa kujua ukweli, hata ikiwa alifundishwa nukta kubwa tu, angepaswa kujisikia mwenye kusukumwa, kwa shukrani, kuhudhuria kwenye mikutano ya Kikristo. Hilo litamwongoza labda kuonyesha waziwazi kwamba anatamani kumtumikia Yehova. Ikiwa, baada ya kujifunza kwa muda mrefu kitabu Ujuzi, mwanafunzi haonyeshi kwamba anathamini mambo ya kiroho, inaweza kuwa vizuri kusimamisha funzo.