Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/96 uku. 8
  • Tutayarishe Utoaji Wetu Wenyewe Wa Magazeti

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tutayarishe Utoaji Wetu Wenyewe Wa Magazeti
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kutayarisha Namna ya Kutolea Mtu Gazeti
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Tolea Watu Magazeti Yanayotoa Ushahidi Juu ya Ile Kweli
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Je, Unatimiza Huduma
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Onyesha Kupendezwa Kibinafsi na Wengine—Kwa Kuwa Mwenye Kujitayarisha
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 11/96 uku. 8

Tutayarishe Utoaji Wetu Wenyewe Wa Magazeti

1 Tunathamini Mnara wa Mlinzi na Amkeni! kwa ajili ya makala yazo zinazotokea kwa wakati ufaao na zenye kuelimisha, zinazozungumzia habari zote, maswala yanayovuma hadi “mambo yenye kina kirefu ya Mungu.” (1 Kor. 2:​10, NW) Kila mmoja wetu anakumbuka hesabu ya mambo mapya na yenye kujenga aliyosoma katika magazeti hayo, ambayo Yehova anatumia ili kufunua hatua kwa hatua ukweli. (Mit. 4:18) Na sisi hakika ni wenye kufurahia kuyagawanya kwa uwingi iwezekanavyo.

2 Tuchunguze Eneo Letu: Ni watu wa aina gani wanaoishi katika ujirani wetu? Ikiwa watu wanaishi maisha ya pirika-pirika (yenye shughuli nyingi), itafaa bila shaka tutayarishe utoaji wa haraka unaoonyesha moja kwa moja kusudi. Kinyume na hilo, ikiwa wakaaji wa eneo letu wana hali ya maisha yenye utulivu zaidi, tutaweza labda kuzungumza kwa urefu zaidi. Mahali ambapo watu walio wengi wanatumika wakati wa mchana, bila shaka tutapata mafanikio zaidi ikiwa tunapita makwao mwishoni mwa kisha-mchana au mapema mwanzoni mwa jioni. Wakati wa mchana, tutaweza kuwakuta wamoja kwa kuhubiri barabarani au duka kwa duka. Wahubiri wamoja wanapata matokeo mazuri kwa kuwakaribia watu kwenye nafasi za kuegeshea magari na katika mabustani ya watu wote.

3 Tuyajue Vizuri Magazeti Yetu: Tusome kila namba tangu tu kuipokea. Tuchague makala ambazo tunajua zinaweza kupendeza wakaaji wa eneo letu. Ni habari gani zinazowashughulisha? Katika makala ambayo tunatayarisha kukazia, tutafute andiko kamili ambalo tutaweza kutaja. Tutafute ulizo la kuuliza ili kuchochea kupendezwa kwa msikilizaji wetu. Tuchague andiko moja lenye kulingana ambalo tutakalomsomea ikiwa tunaweza kufanya hivyo. Mwishowe, tufikiri juu ya jinsi tungeweza kutaja sababu ambayo tunaomba mchango mdogo na kutokeza mawazo kwa ajili ya ziara ya kurudia.

4 Tutayarishe Maneno Yetu ya Utangulizi: Tuchague kwa makini maneno ya kwanza ambayo tutasema ili kujitambulisha na kuanzisha mazungumzo. Wamoja wanapata matokeo mazuri kwa kusema: “Nilisoma makala moja yenye kuvutia sana katika gazeti hili, na ninapenda kuijulisha kwa wengine.” Wengi wanaanza kwa ulizo moja litakaloongoza kwenye mazungumzo juu ya wazo ambalo walikusudia kuzungumzia. Kwa mfano:

5 Ikiwa tunatolea makala juu ya ongezeko la uuaji, tunaweza kuuliza:

◼ “Itaomba kufanya nini ili hatimaye tuweze kulala kwa usalama, bila kuhofu kuibiwa au kushambuliwa?” Tufasirie kwamba tuna habari juu ya suluhisho la tatizo hilo, kwa msaada walo fujo za kijamii za kila aina zitatoweka hivi karibuni. Tutaje sentensi moja ya gazeti inayotoa sababu ya kutumainia badiliko hilo. Utakaporudi, unaweza kuvutia uangalifu wa mtu juu ya sura 1 ya kitabu Ujuzi.

6 Tunapotolea makala juu ya maisha ya familia, tunaweza kusema:

◼ “Wazazi wengi wanatambua kwamba si jambo rahisi kulea familia katika siku zetu. Vitabu vingi viliandikwa juu ya habari hiyo, lakini hata wataalamu hawakubaliani kati yao. Je! kuna mtu fulani anayeweza kututolea mashauri ya kweli-kweli?” Taja sentensi moja ya gazeti inayoonyesha ni mashauri gani yenye hekima yanayopatikana katika Biblia. Tunaporudi kumwona mtu, tuzungumze pamoja naye mawazo ya Biblia kuhusu malezi ya watoto, yanayotolewa kwenye kurasa 145-8 za kitabu Ujuzi.

7  Ili kutolea makala inayozungumzia tatizo fulani la kijamii, tunaweza kusema:

◼ “Watu wengi wanajisikia wakiwa chini ya mikazo kwa sababu ya kipindi chenye kuogofya tunamoishi. Je! unafikiri kwamba Mungu alikuwa anatukusudia kuishi hivi?” Tutolee makala inayoonyesha jinsi ya kumaliza matatizo ya leo au makala inayotoa sababu za kungoja wakati ujao ulio huru na woga wowote. Wakati wa ziara yetu ijayo, tuzungumzie picha na maelezo yake yanayofuata kwenye kurasa 4-5 za kitabu Ujuzi, kisha tuanze moja kwa moja funzo la Biblia.

8 Tujue Kujiambatanisha na Msikilizaji Wetu: Watu ambao tunakutana nao wanatoka katika sehemu mbalimbali na kila mmoja wao ana mapendezi yake. Tutayarishe utoaji wa msingi ambao tutaambatanisha na kila msikilizaji. Tufikirie mapema yale tutakayosema iwe tunakutana na mwanamume, mwanamke, mtu mzee-mzee au kijana tutakayekutana naye. Hakuna kanuni kwa habari hiyo. Tutumie utoaji mbalimbali tunaojua vizuri na ambao tunapata matokeo mazuri nao. Katika hali zote, tuwe wenye shauku, tuseme na moyo wetu na tujue kusikiliza. Wale walio katika “mwelekeo ufaao” wataona unyofu wetu na wataitikia vizuri.—Mdo. 13:48.

9 Tusaidiane: Kwa kubadilishana mawazo na wengine, tutatajirisha namna yetu ya kusema. Tutajipatia ujuzi na kuwa wenye uhakika ikiwa tunarudia-rudia utoaji wetu mbalimbali pamoja na washiriki wenzetu. (Mit. 27:17) Tutajisikia hivyo wenye kustarehe zaidi kwenye milango. Ni muhimu kwamba wazazi wachukue wakati wa kuwasaidia watoto wao kujitayarisha, wawasikilize wakati wanapojizoeza utoaji wao na wawatolee mashauri ili kuuboresha. Kuhusu wapya, mahubiri pamoja na wahubiri wenye ujuzi zaidi yatawafaidisha sana.

10 Kutayarisha utoaji wetu wenyewe wa magazeti hakungepaswa kuwa na matatizo. Inaomba tu kuwa akilini na jambo fulani kamili la kusema na kufanya baadaye utoaji kwa namna yenye kuvutia. Pamoja na juhudi kidogo na kwa kufikiria mambo, tunaweza kutayarisha utoaji bora kabisa utakaochochea kuitikia kuzuri.

11 Ugawaji wa magazeti ni mojawapo ya njia za muhimu kupitia hizo tunatawanya ujumbe wa Ufalme ulimwenguni. Ikiwa tunaweza kuweka Mnara wa Mlinzi na Amkeni! katika mikono ya watu wanyofu, magazeti yataweza kusema yenyewe. Tukumbuke sikuzote thamani yayo, na kwamba ujumbe uliomo unaweza kuokoa uhai. Namna hiyo ya “kutenda mema na kule kushiriki vitu pamoja na wengine” hakika kunampendeza Yehova.​—Ebr. 13:​16, NW.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine