Tolea Watu Magazeti Yanayotoa Ushahidi Juu ya Ile Kweli
1 Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova na Amkeni! ni magazeti yanayotimiza kazi kubwa katika kazi ya kuhubiri Ufalme na kufanya wanafunzi. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Tunaposhiriki katika aina mbalimbali ya kazi ya kuhubiri Ufalme tunafurahi kutolea watu kwa ukawaida magazeti hayo yanayotolewa kwa wakati unaofaa.
2 Miaka iliyopita tumeona mabadiliko yakifanyika kuhusu ukubwa na mambo yaliyo katika magazeti pia katika njia tulizotumia ili kutolea watu magazeti. Mabadiliko hayo yamefanywa ili magazeti hayo yavutie sana na yawe na matokeo mazuri na pia ili ujumbe wa Ufalme uguse mioyo ya ‘watu wa namna zote ili waokolewa na kupata ujuzi sahihi wa kweli.’—1 Tim. 2:4.
3 Tangu mwezi wa 1, 2006, tumepata ufundi wa kutolea watu Amkeni! moja kila mwezi kwa kutumia utoaji mbalimbali. Sasa katika mahubiri tutatolea vilevile watu moja kati ya matoleo mawili ya Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova. Maneno tunayoweza kusema ili kutolea watu magazeti yanapatikana kwenye ukurasa wa mwisho wa Huduma Yetu ya Ufalme. Kwa kawaida maneno hayo yanakazia habari za mwanzo-mwanzo za gazeti, lakini huenda wakati mwingine tutakazia habari zingine ambazo zinavutia sana watu. Maneno hayo yenye kupendekezwa yanaweza kuwa na matokeo mazuri ikiwa tunajua vizuri habari za gazeti zinazopaswa kukaziwa na ikiwa tunatumia maneno yetu wenyewe ili kufanya mahubiri yetu yapatane na hali ya eneo letu.
4 Ijapokuwa Huduma Yetu ya Ufalme inapendekeza namna mbili ya kutolea watu kila gazeti, kila mhubiri iko huru kutumia namna nyingine iliyo tofauti na vile inavyoonyeshwa kwenye Huduma Yetu ya Ufalme. Sababu moja ya kufanya hivyo ni kwamba habari nyingine katika gazeti zaidi ya ile iliyopendekezwa inaweza kuvutia sana watu katika eneo lako. Ao labda unaona kwamba unaweza kutumia kwa matokeo zaidi habari fulani inayokupendeza sana.
5 Jinsi ya Kujitayarisha: Jambo la kwanza, ni lazima kujua vizuri habari unayotaka kukazia katika gazeti. Hauwezi kila mara kujua vizuri kila habari inayopatikana katika gazeti mbele ya kuitumia katika mahubiri. Hata hivyo, unapochagua habari unazotaka kukazia, unapaswa kuwa mwenye uchangamfu na mwenye usadikisho unapozungumzia habari hizo. Unaweza kuwa hivyo ikiwa tu unajua vizuri habari unayotaka kutolea watu.
6 Jambo la pili, unapotayarisha maneno ya utangulizi, fikiria akilini hali mbalimbali zinazoweza kujitokeza na kuwa hivyo mwenye kubadilika kulingana na hali hizo. Ili kuanzisha mazungumzo unaweza kutumia ulizo linaloamsha kupendezwa linalopatana na habari. Siku zote tegemea nguvu ya Neno la Mungu ili kugusa moyo. (Ebr. 4:12) Chagua andiko linalofaa linalozungumzia habari unayomtolea mtu, ingekuwa vizuri zaidi kuchagua andiko linalotajwa katika habari unayozungumzia. Fikiria jinsi ya kuambatanisha andiko lile na habari.
7 Kila Mara Nafasi Inapojitokeza: Tusipotumia mambo tuliyotayarisha, hayatakuwa na faida yoyote. Jiunge na kutaniko Siku ya Posho katika mahubiri ya kuachia watu magazeti. Tolea magazeti watu ambao hapo mbele walikubali vitabu vingine. Kila mara tolea magazeti watu unaojifunza nao Biblia na watu wengine unaokuta hapo unaporudilia wale waliopendezwa. Unaweza kutolea magazeti watu unaozungumza nao unapokwenda kununua vitu, unaposafiri, au unapongojea daktari. Mara kwa mara tengeneza vizuri maneno utakayowaambia watu, kwa kuwa utawatolea magazeti yaleyale katika mwezi mzima.
8 Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ni tofauti kabisa na magazeti mengine. Magazeti hayo yanamtukuza Yehova akiwa Mwenye enzi kuu ya ulimwengu. (Mdo. 4:24) Yanafariji watu kupitia habari njema ya Ufalme wa Mungu na kuwatia moyo wawe na imani katika Yesu Kristo. (Mt. 24:14; Mdo. 10:43) Zaidi ya hilo, yanaendelea kufuatilia matukio ya ulimwengu ili kuona namna yanavyotimiza unabii wa Biblia. (Mt. 25:13) Saidia watu katika eneo lako wafaidike na magazeti hayo. Unaweza kufanya hivyo ikiwa unajitayarisha kwa kusudi la kuwatolea magazeti kila mara nafasi inapojitokeza!
9 Unapokuwa na matokeo mazuri katika kutolea watu magazeti, au hata ikiwa una mazungumzo tu ya kirafiki kuhusu mambo ya dini pamoja na mtu, uwe tayari kutokeza ulizo au wazo litakalomsaidia afikiri na litakalofanya iwezekane umurudilie ili kuendelea na mazungumzo ya Biblia. Ikiwa tuna bidii ya kupanda mbegu ya ukweli, tunaweza kuwa hakika kwamba Yehova atafungua mioyo ya wale ambao wanapenda kwelikweli kumjua na kumtumikia Yeye.—1 Kor. 3:6.
[Maulizo ya Funzo]
1. Magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yanatimiza kazi gani katika kazi yetu ya kuhubiri?
2. Ni mabadiliko gani ambayo yamefanywa katika Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, na kwa nini?
3. Namna gani tutatumia magazeti yetu katika mahubiri?
4. Kwa nini linaweza kuwa jambo lenye kufaa kutumia maneno tofauti na yale yanayopendekezwa katika Huduma Yetu ya Ufalme wakati wa kutolea mtu gazeti?
5. Kabla ya kutayarisha habari ya gazeti linalopendekezwa, unapaswa kufanya nini?
6. Namna gani tunaweza kujitayarisha ili kutolea watu magazeti?
7. Namna gani tunaweza kutengeneza vizuri zaidi namna yetu ya kutolea watu magazeti?
8. Ni katika njia gani Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ni tofauti na magazeti mengine?
9. Namna gani tunaweza kuweka msingi kwa ajili ya kurudilia wale waliopendezwa?