Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/05 uku. 8
  • Tumia Magazeti Katika Huduma Yako

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tumia Magazeti Katika Huduma Yako
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Magazeti Huutangaza Ufalme
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Chagua Makala Kwa Kulenga Kupendezwa Kwa Watu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Je! Unalo Ombi la Kawaida?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
Huduma Yetu ya Ufalme—2005
km 2/05 uku. 8

Tumia Magazeti Katika Huduma Yako

1 “Ni yenye kupendeza, yenye kufika pa wakati, na yenye kutia moyo.” “Hayo ni magazeti yenye kutia moyo zaidi ambayo sijawahi kusoma.” Maelezo hayo yanaonyesha vizuri jinsi wasomaji ulimwenguni pote wanavyojisikia kuhusu Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Kwa kweli, magazeti yetu yameonekana kuwa vyombo vya thamani sana katika kutolea “watu wa namna zote” habari njema. —1 Tim. 2:4.

2 Mwanaume mwenye kufuatia sana kazi-maisha alipokea gazeti Amkeni! iliyokuwa na habari iliyompendeza. Baadaye, akasoma toleo la Mnara wa Mlinzi alilopokea pamoja na Amkeni! hiyo, lililokuwa na makala ambayo ilimchochea kuchunguza kwa makini imani aliyokuwa nayo kwa muda mrefu kuhusu Utatu. Jambo hilo liliamsha kupendezwa kwake. Miezi sita baadaye akabatizwa. Mwanamume mwengine alikuwa akipokea kwa ukawaida magazeti lakini hakuwa akiyasoma. Kwa upande mwingine, mke wake aliyekuwa akiepuka Mashahidi alikuwa akiyasoma magazeti waliokuwa wakimwachia mume wake. Moyo wake ukaguswa na ahadi ya Biblia ya dunia paradiso itakayojazwa na watu waadilifu. Baadaye, yeye, mwana wake, na dada yake wakawa watumishi wa Yehova.

3 Yatoe Yakiwa Pamoja: Kama mifano iliyo hapo juu inavyoonyesha, hatuwezi kujua kwa hakika nani atakayesoma magazeti yetu au habari gani inayoweza kuamsha kupendezwa kwao. (Mhu. 11:6) Kwa hiyo, ni jambo lenye faida kutolea Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yakiwa pamoja, hata ikiwa kwa kawaida tutakazia gazeti moja katika utoaji wetu. Katika hali fulani, linaweza kuwa jambo lenye kufaa kutolea watu matoleo mbalimbali ya magazeti yetu kwenye ziara moja.

4 Ni jambo lenye faida kupanga siku moja katika juma ili kushiriki katika kazi ya kutoa magazeti. Kwenye Kalenda ya Mashahidi wa Yehova ya 2005, kila Siku ya Posho inapendekezwa kuwa “Siku ya Magazeti.” Bila shaka, kwa kuwa hali za mahali na za kibinafsi zinatofautiana, ndugu wengine wanaweza kupangia siku nyingine ili kutolea watu magazeti yetu. Je, hii ni sehemu ya programu yako ya kila juma?

5 Ujiwekee Mradi wa Kibinafsi: Kujiwekea mradi wa kibinafsi kila mwezi kuhusu uwingi wa magazeti ya kutolea watu, kunaweza kutusaidia tufikirie zaidi jambo la kutolea watu magazeti. Je, una watu ambao unaachia magazeti kwa ukawaida? Je, unatoa magazeti kwa wale ambao unakutana nao katika huduma? Je, unaweza kutolea watu magazeti katika utumishi wa barabarani, katika eneo la biashara, na katika mahali pa watu wote? Je, unachukua magazeti unaposafiri, unapokwenda kununua vitu dukani, na unapokwenda kuonana na mtu fulani? Tumia vizuri kila nafasi inayopatikana ili kusaidia wengine wafaidike kutokana na Mnara wa Mlinzi na Amkeni!

6 Tunapaswa kufanya pia iwe mradi wetu kutoa magazeti ya zamani tuliyo nayo. Hata ikiwa magazeti hayakutolewa mnamo mwezi moja au miwili, bado habari iliyomo ni yenye thamani. Uwatolee watu wanaopendezwa. Kwa mamilioni ya watu, Mnara wa Mlinzi na Amkeni! imekuwa “neno . . . kwa wakati unaofaa.” (Met. 25:11) Na tuyatumie ili kusaidia mamilioni ya watu zaidi ili wamjue na kumtumikia Yehova.

[Maulizo ya Funzo]

1, 2. Namna gani Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yanagusa maisha za watu?

3. Kuna faida gani ya kutoa magazeti yakiwa pamoja?

4. Namna gani tunaweza kupangia kazi ya magazeti?

5. Ni nafasi gani tunazopaswa kufikiria ili kutolea watu magazeti, na ni nini itakayotusaidia kufanya hivyo?

6. Namna gani tunaweza kufanya matumizi mazuri ya magazeti ya zamani?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine