Chagua Makala Kwa Kulenga Kupendezwa Kwa Watu
1 Kama vile wapiga-upinde wanaolenga kwa uangalifu kwa mishale yao kabla ya kuirusha, wahubiri na mapainia wengi wa kutaniko ni wenye kupata matokeo bora kwa kutumia makala ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yaliyochaguliwa kwa kulenga kupendezwa kwa watu katika eneo lao. Wanaamua ni nani zaidi yaelekea watapendezwa kusoma makala fulani za magazeti. Wanafanyaje hivyo?
2 Kwanza, wanasoma kila toleo toka jalada hadi jalada. Baadaye, wao hujiuliza wenyewe, Ni aina gani ya watu ambao kila makala ingependeza? Ndipo jitihada hufanywa ili kutembelea watu ambao yaelekea wangeweza kupendezwa kusoma makala hayo. Wanapofikiri kimbele kwamba toleo la pekee lingeweza kukubaliwa kwa wingi katika eneo lao, wanafanya ombi la ziada.
3 Magazeti Yetu Yanathaminiwa Sana: Mmoja wa waandikishaji wetu anayetumikia gazeti la kimataifa la Nigeria lisomwalo kuliko mengine yote aliandika kuhusu Amkeni!: “Pongezi kwa gazeti la upendezi wa ujumla lililo bora zaidi ulimwenguni.” Msomaji mwenye bidii wa magazeti yetu anaeleza: “Hizo ni johari nzuri kama nini za hekima ya bei kubwa ajabu! Ni kama hakuna habari yoyote inipendezayo nisiyoipata imezungumzwa mahali fulani katika kurasa za mojapo mabuku haya.”
4 Magazeti yanazungumzia habari mbalimbali, kutia ndani Biblia, matukio ya ulimwengu, mambo ya familia, matatizo ya kijamii, historia, sayansi, maisha ya wanyama na mimea, kwa kutaja hayo tu. Bila shaka, mtu anaelekea kusoma kitu fulani kinachohusiana na mahitaji yake, hali yake au kazi yake. Kwa kuwa tunasimulia na watu tofauti tofauti, kila mmoja akiwa na mapendezi na matatizo yake kibinafsi, kuchagua makala kwa kulenga mambo yanayowapendeza ni kwenye matokeo sana.
5 Ona kile kilichotukia wakati Mashahidi wawili walipopendekeza toleo la Amkeni! la Septemba 8, 1996 kwa mwandikaji-gazeti mmoja. Yeye aliandika: “Kabla ya mimi kupata nafasi ya kusema kwamba sikupendezwa, mmoja wao akaongeza: ‘Kuna makala juu ya Wahindi wa Amerika. Tunajua kwamba umekuwa ukiandika mengi juu ya jambo hilo.’ ” Akachukua gazeti, na wakati wa mlo wa asubuhi alisoma habari juu ya Wahindi. Alikubali baadaye kwamba “ilikuwa bora” na “yenye unyofu sana.”
6 Ni Nini Kinachopendeza Watu Katika Eneo Lako? Ulisoma nini katika magazeti ya karibuni kinachoweza kupendeza wauza-bidhaa (wachuuzi) au wafanya kazi katika eneo lako au kwa majirani zako, wafanya kazi wenzako na wanashule wenzako? Ni nini lingekuwa la kupendeza kipekee kwa wanasheria, walimu, washauri wa familia na shule, washauri wa vijana, watumishi wa jamii, na madaktari wa afya? Kuwa na watu unaowahubiri akilini unapofikiria kila toleo kutakupa njia bora za kueneza neno la kweli.
7 Wakati mtu fulani anapopendezwa kipekee na makala moja ya Mnara wa Mlinzi au Amkeni! na anakubali gazeti, tunaweza kusema: “Wakati ujao nitakaposoma makala ambayo yaelekea itakupendeza, nitakuwa mwenye furaha kukuletea yenyewe.” Hivyo labda tutaongeza mtu mmoja kwenye njia yetu ya magazeti kwa kurudi mara nyingi iwezekanavyo kumtolea namba za karibuni. Hilo linafanana na lile tunalofanya wakati tunaporuhusiwa kurudi kuona wale ambao walipendezwa na aina fulani za makala. Makala ya namna hiyo ni mengi katika magazeti yetu ya zamani. Tunaweza kuyachagua na kuwapelekea hayo. Tukifanya hivyo, tunaweza hata kumaliza stoki ya magazeti ya zamani.
8 Uwe na Mradi wa Kiroho: Miaka michache iliyopita, mwanamume mmoja mwenye kufikiria kazi yake ya maisha tu alipokea gazeti Amkeni! lililompendeza. Hata hivyo, mwanamume huyo wa kidini alisoma pia toleo la Mnara wa Mlinzi alilopokea wakati uohuo. Makala moja yalimwongoza kuchunguza imani yake ya maisha yote katika utatu. Miezi sita baadaye alibatizwa! Kwa hiyo, usisite kuanzisha mazungumzo pamoja na wasomaji wa magazeti yetu. Unaweza kuwatolea broshua Mungu Anataka Nini Kwetu? na kupendekeza kuchukua dakika chache tu kuchunguza somo moja kwa kila ziara wakati unaporudi na aina mpya ya magazeti.
9 Fikiria kwa uangalifu ni nani, kati ya ziara zako za kurudia na mahusiano yako ya kibiashara angependa kupata namba za karibuni za Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Kisha fanya jitihada ya kweli kuwafikia. Tembelea watu wengi iwezekanavyo ukiwa na mabuku haya ya thamani. Na usisahau kamwe kwamba kwa kadiri unavyojitahidi kusaidia watu wengi zaidi kusoma magazeti yetu, wewe ni mwenye ‘kutupa chakula chako juu ya maji.’ Hatimaye, unaweza kuwa na matokeo katika kupata wanafunzi wapya wa wakati ujao.—Mhu. 11:1, 6.