Habari hii Itamupendeza Nani?
1. Tunapaswa kufikiria nini tunaposoma Munara wa Mulinzi ao Amkeni!, na kwa sababu gani?
1 Wakati magazeti Munara wa Mulinzi na Amkeni! yanatayarishwa, mahitaji ya watu duniani pote yanafikiriwa. Kwa hiyo, magazeti hayo yanazungumuzia habari mbalimbali. Tunaposoma habari katika gazeti, tunapaswa kufikiria mutu anayeweza kupendezwa na habari hiyo, kisha hapo tutafanya mipango ili kumutolea gazeti hilo.
2. Ni habari gani zinazozungumuziwa katika magazeti yetu zinazoweza kupendeza watu?
2 Je, Munara wa Mulinzi wa hivi karibuni una habari fulani ya Biblia ambayo mulizungumuzia pamoja na mufanyakazi mwenzako? Je, kuna habari kuhusu maisha ya familia inayoweza kusaidia mutu wa familia? Je, unamufahamia mutu anayepanga kutembelea inchi fulani ambayo imezungumuziwa katika Amkeni!? Je, moja kati ya magazeti inaweza kuwavutia watu wanaotumika katika mashirika ya biashara ao ya serikali katika eneo lenu? Kwa mufano, gazeti linalozungumuzia magumu ya uzee linaweza kuwapendeza sana watu walio katika makao ya kuwatunzia wazee. Watu wanaotumika katika shirika zinazoshugulikia mambo ya sheria wanaweza kupendezwa na gazeti lililo na habari kuhusu uvunjaji wa sheria.
3. Eleza mambo ambayo wahubiri walikutana nayo yanayoonyesha faida ya kutolea magazeti watu ambao tunaona wanaweza kupendezwa na habari zilizo ndani.
3 Matokeo: Kisha kupokea Amkeni! ya Mwezi wa 10, 2011 yenye kichwa “Kuwalea Watoto Wenye Kutegemeka,” ndugu mumoja na bibi yake huko Afrika ya kusini waliita kupitia telefone wakubwa wa masomo 25 katika eneo la kutaniko lao. Wakubwa 22 kati yao walikubali magazeti na wakayagawanyia wanafunzi katika masomo yao. Ndugu mwingine na bibi yake katika inchi hiyo walifanya hivyo pia katika eneo lao na wakagawanya magazeti kwenye masomo mbalimbali. Walimu kwenye moja kati ya masomo hayo waliamua kutumia gazeti hilo katika programe yao ya masomo. Ndugu huyo na bibi yake walimuelezea mwangalizi wa muzunguko mambo hayo waliyokutana nayo. Hivyo, mwangalizi akatia moyo makutaniko ya muzunguko wake yatembelee masomo ya eneo lao. Makutaniko yaliomba tena gazeti hilo kwenye biro ya tawi hivi kwamba iliomba lichapishwe tena!
4. Sababu gani tunataka kuwatolea watu wengi zaidi magazeti kadiri iwezekanavyo?
4 Magazeti yetu yanaeleza kwa nini matukio ya leo yanatokea na mambo tunayoweza kujifunza kutokana nayo, na pia yanaelekeza uangalifu wetu juu ya Biblia na Ufalme wa Mungu. Duniani pote magazeti hayo tu ndiyo ‘yanayotangaza wokovu.’ (Isa. 52:7) Kwa hiyo, tunataka kuyatolea watu wengi zaidi kadiri iwezekanavyo. Njia nzuri ya kufanya hivyo, ni kujiuliza ulizo hili, ‘Habari hii Itamupendeza Nani?’