Jinsi Ya Kufanya Wanafunzi Kwa Msaada Wa Kitabu Ujuzi
1 Wakristo wote wana mradi wenye kusifika wa kufundisha ukweli kwa wengine na wa kufanya wanafunzi wale walio katika “mwelekeo ufaao kwa ajili ya uhai udumuo milele.” (Mdo. 13:48 ; Mt. 28:19, 20) Ili kutusaidia kufikia mradi huo, tengenezo la Yehova limetupatia chombo kizuri kabisa: kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Kichwa cha habari cha kitabu hicho kinaonyesha umuhimu wa pekee wa mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Kwa hiyo, ili kupata uhai udumuo milele, inafaa kujifunza kumjua Yehova, Mungu pekee wa kweli, na Mwana wake, Yesu Kristo.—Yn. 17:3.
2 Kwa sasa, kitabu Ujuzi ndicho kitabu cha kwanza cha Sosaiti cha kutumia wakati wa mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Kwa msaada wacho, tunaweza kufundisha ukweli kwa urahisi, waziwazi na kwa ufupi. Hilo litatusaidia kugusa moyo wa wale ambao tunafundisha. (Lk. 24:32) Bila shaka, ni jambo la lazima kwamba yule anayeongoza funzo atumie ufundi mzuri mbalimbali wa kufundisha. Ni kwa sababu hiyo nyongeza hii imetayarishwa katika kusudi la kutolea madokezo na vikumbusho kuhusu ufundi wa kufundisha ambao ulionekana kuwa wenye matokeo. Kwa utambuzi na kulingana na hali yetu, tunaweza bila shaka kutumikisha hatua kwa hatua mamoja ya madokezo hayo, hata yote. Tulinde nyongeza hii na tuichunguze mara kwa mara. Ina nukta mbalimbali ambazo zitakuwa zenye matokeo zaidi wakati tutakapotumia kitabu Ujuzi ili kufanya wanafunzi.
3 Tuongoze Funzo la Biblia Hatua kwa Hatua: Tupendezwe kibinafsi na kwa unyofu na mwanafunzi, tukimwona kama mwanafunzi Mkristo na kama ndugu au dada wa wakati ujao. Tuwe wenye shauku, wenye urafiki na wenye furaha. Ikiwa sisi ni wasikiaji wenye makini, tutafikia kumjua mtu—wakati wake uliopita na hali yake ya maisha—jambo ambalo litatusaidia kutambua ni nini namna iliyo bora zaidi ya kumsaidia kiroho. Tuwe tayari kujitoa wenyewe kwa faida ya mwanafunzi.—1 Thes. 2:8.
4 Funzo likiisha kusitawi vizuri, ni vema kuchunguza sura za kitabu Ujuzi kwa kufuata utaratibu wa mpangilio wa sura. Hivyo mwanafunzi ataweza kupata uelewevu wa ukweli hatua kwa hatua, kwani kitabu kinazungumzia habari za kibiblia kwa namna iliyo sawa iwezekanavyo. Fanya kwamba funzo libaki rahisi na lenye kupendeza, ili liwe hai na kwamba liendelee. (Rum. 12:11) Kulingana na hali na uwezo wa akili wa mwanafunzi, labda itawezekana kuchunguza sura fulani nyingi kwa somo moja tu muda wa saa moja hivi, bila hata hivyo kwenda haraka haraka na funzo. Wanafunzi watafanya maendeleo zaidi ikiwa mwalimu na wao wenyewe wanaheshimu siku ya kukutana kwa ajili ya funzo kila juma. Labda itawezekana, kujifunza na watu wengine sura 19 za kitabu muda wa miezi 6 hivi.
5 Anza kila somo kwa maelezo mafupi yatakayoamsha kupendezwa kwa ajili ya habari. Utaona kwamba kila sura inafanyiza kichwa cha habari kinachopaswa kuzungumziwa kwa urefu. Kila kichwa kidogo cha habari kinazungumzia kipekee nukta fulani kubwa, jambo ambalo linakusaidia kulinda akilini kichwa cha sura. Uwe mwangalifu kwamba usiseme-seme sana. Badala yake ujikaze kumfanya mwanafunzi aseme. Kwa kuuliza mwanafunzi maulizo kamili yenye kuonyesha majibu unayotaka kulingana na yale tayari anajua, utamsaidia kufikiri na kufikia maamuzi mazuri. (Mt. 17:24-26; Lk. 10:25-37; ona Kiongozi cha Shule, uku. 51 fu. 10.) Fuatia kwa ukaribu habari zinazopatikana katika kitabu Ujuzi. Ikiwa unaingiza maelezo ya ziada, utakwenda pembeni ya mawazo makuu au utayavuruga, jambo ambalo litarefusha funzo. (Yn. 16:12) Ikiwa ulizo ambalo halina uhusiano na habari inayofunzwa linatokezwa, mara nyingi utaweza kulijibu mwishoni mwa funzo. Hilo litakuwezesha kuendelea na somo la juma bila wewe kuwa mwenye kugawanyika. Mwambie mwanafunzi kwamba siku nenda atapata jibu kwa mengi ya maulizo yake muda wa funzo.—Ona Kiongozi cha Shule, uku. 94 fu. 14.
6 Ikiwa mwanafunzi anaamini kwelikweli katika Utatu, kutokufa kwa nafsi, helo ya moto au mafundisho mengine ya uongo na kwamba mafasirio ya kitabu Ujuzi hayamtoshi, unaweza kumtolea kitabu Kutoa Sababu au kichapo kingine kinachozungumzia habari hiyo. Umwambie kwamba utazungumza naye kisha yeye kufikiri kwa yale atakayosoma.
7 Kwa kuanza na kwa kumaliza funzo kwa sala ili kutafuta uongozi wa Yehova, tutatoa staha kwa wakati, na tutatia kila mtu katika hali ya akili yenye kuheshimika, huku tukimtanguliza Yehova mbele kama vile Mwalimu wa kweli. (Yn. 6:45) Ikiwa mwanafunzi anavuta bado tumbaku, labda itakuwa lazima kumwomba kutovuta wakati wa funzo.—Mdo. 24:16; Yk. 4:3.
8 Tufundishe kwa Matokeo kwa Njia ya Maandiko, Mifano na Maulizo ya Kujikumbusha: Haidhuru iwe ni mara ngapi tumekwisha kujifunza habari: mwalimu stadi atachunguza upya mapema kila somo, akifikiria mwanafunzi kwa kibinafsi. Hilo litamsaidia kufikiria mapema mojawapo ya maulizo yake. Ili kufundisha kwa matokeo, uwe na uelewevu ulio wazi wa nukta kuu za sura. Tafuta maandiko ili kuona ni katika njia gani yanaambatana na habari na amua yale yatakayosomwa wakati wa funzo. Fikiri vizuri kwa namna unaweza kufundisha kwa msaada wa mifano na maulizo ya kujikumbusha yaliyo mwishoni mwa sura.
9 Kwa kutumia kwa matokeo Maandiko, utamsaidia mwanafunzi kutambua kwamba anajifunza kabisa kabisa Biblia. (Mdo. 17:11) Tumikisha kisanduku “Tumia Biblia Yako Vizuri”, kwenye ukurasa 14 wa kitabu Ujuzi, ili kumfundisha kujua nafasi maandiko hupatikana. Mwonyeshe jinsi ya kutambua maandiko yanayonukuliwa katika somo. Ikiwa wakati unaruhusu, tafuteni na someni yale yanayoonyeshwa lakini hayanukuliwi. Omba mwanafunzi afasirie ni katika upande gani maandiko hayo yanategemeza au kuonyesha wazi yale fungu linavyosema. Tilia mkazo juu ya sehemu za muhimu za maandiko ili kwamba mwanafunzi aelewe sababu ya kuwa ya nukta kubwa ya somo. (Neh. 8:8) Kwa ujumla, si lazima mwalimu kuongeza tena maandiko mengine zaidi ya yale yanayopatikana katika kitabu. Fasiria umuhimu wa kuyajua majina na mpangilio wa vitabu vya Biblia. Litakuwa labda jambo la lazima kwa mwanafunzi kusoma Mnara wa Mlinzi wa Juni 15, 1991, kurasa 27-30. Inapopatana, tia moyo matumizi ya Traduction du monde nouveau. Unaweza kuonyesha hatua kwa hatua jinsi ya kutumikisha sehemu zayo mbalimbali, kama vile mitajo ya pembizoni na fahirisi ya maneno ya kibiblia.
10 Somo 34 la Kiongozi cha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi linaonyesha kwamba vielelezo au mifano inamsha kufikiri na inawezesha kuelewa kwa vyepesi zaidi mawazo mapya. Inaunganisha pia mvuto wa akili pamoja na mkazo wa moyoni, hivi kwamba ule ujumbe unafikishwa akilini kwa mkazo usiowezekana mara nyingi kutolewa tu maelezo mepesi ya jambo la hakika. (Mt. 13:34) Kitabu Ujuzi kina mifano mingi inayokusudiwa kufundisha, iliyo rahisi lakini yenye nguvu. Hivyo, tunakuta katika fungu la 17 mfano unaotusukuma kuwa wenye shukrani kwa namna Yehova anavyotutolea, kwa upande wa kiroho, chakula, mavazi na ulinzi kwa njia ya kutaniko la Kikristo. Picha nzuri za rangi za kitabu Ujuzi zinaweza kutumiwa kwa matokeo ili kuamsha hisia-moyo. Kwa kuchunguza kichwa kidogo cha habari “Ufufuo Wenye Shangwe” kwenye ukurasa 185, fungu 18 kitakuwa na uvutano mzuri juu ya mwanafunzi ikiwa anaangalia picha ya ukurasa 86. Hilo litamsukuma labda kuona katika ufufuo ukweli wa Ufalme wa Mungu.
11 Inafaa kwamba wanafunzi wa Biblia wafanye maendeleo ya kiroho kwa kila somo. Ni kwa sababu hiyo usisahau kuuliza maulizo ya kujikumbusha yaliyomo katika kisanduku “Tahini Ujuzi Wako” yanayopatikana mwishoni mwa kila sura. Tumaini kwamba yale yaliyofunzwa yalikuwa zaidi kuliko utoaji habari kiakili tu. Mojawapo ya maulizo hayo yana kusudi la kuchochea jibu la kibinafsi linalotoka moyoni. Kwa mfano, ona ukurasa 31, mahali wanapomwuliza mwanafunzi: “Ni sifa zipi za Yehova Mungu ambazo hasa hukuvutia wewe?”—2 Kor. 13:5.
12 Funza Wanafunzi Kujitayarisha kwa Ajili ya Funzo: Mwanafunzi anayesoma somo mapema, anaandika maulizo na anafikiri juu ya namna anavyoweza kuyasema katika maneno yake mwenyewe atafanya maendeleo haraka kwa upande wa kiroho. Kupitia mfano wako na vitia-moyo vyako, unaweza kumfundisha kujitayarisha kwa ajili ya funzo. Umwonyeshe kitabu chako, juu yacho ulipanga au kupiga mistari semi na maneno makuu. Umwonyeshe jinsi ya kupata moja kwa moja majibu kwa maulizo yaliyochapwa. Utaweza kumsaidia mwanafunzi kwa kutayarisha sura moja pamoja naye. Umtie moyo kusema katika maneno yake mwenyewe. Ndiyo njia moja ya kutambua ikiwa anaelewa hakika mafundisho. Ikiwa anasoma jibu ndani ya kitabu, unaweza kuamsha uwezo wake wa kufikiri kwa kumuuliza jinsi gani angeweza kufasiria wazo hilo kwa mtu mwingine katika maneno yake mwenyewe.
13 Mtie mwanafunzi moyo kutafuta maandiko yasiyotajwa wakati wa kutayarisha kwake kila juma, kwani hamtapata labda wakati wa kuyasoma yote muda wa funzo. Mpongeze kwa ajili ya bidii anayofanya kwa kutayarisha mafunzo yake. (2 Pt. 1:5; ona Mnara wa Mlinzi wa Agosti 15, 1993, kur. 13-14, ambamo tunapata madokezo mengine juu ya yale yanayoweza kufanyika iwe na mwalimu kama vile na mwanafunzi ili kwamba ajifunze vizuri zaidi wakati wa funzo la Biblia.) Katika njia hiyo, mwanafunzi anajifunza kujitayarisha kwa ajili ya mikutano ya kutaniko na kutoa maelezo mazuri. Anajifunza jinsi ya kupata mazoea mazuri ya funzo la kibinafsi; atakuwa hivyo tayari ili kuendelea kufanya maendeleo katika ukweli funzo lake la Biblia litakapomalizika juu ya kitabu Ujuzi.—1 Tim. 4:15; 1 Pt. 2:2.
14 Tuongoze Wanafunzi Kwenye Tengenezo la Yehova: Wale wanaofanya wanafunzi wana daraka la kuongoza wanafunzi kwenye tengenezo la Yehova. Mwanafunzi atasonga mbele zaidi kwenye ukomavu wa kiroho ikiwa anajua na anathamini tengenezo la Mungu na ikiwa anatambua umuhimu wa kuwa sehemu yalo. Tunatamani afurahie kushirikiana na watumishi wa Mungu na awe na tamaa ya kuwa pamoja nasi kwenye Jumba la Ufalme, ambako atapokea tegemezo la kiroho na la kiakili kutoka kutaniko la Kikristo.—1 Tim. 3:15.
15 Broshua Mashahidi wa Yehova—Wanafanya Mapenzi ya Mungu kwa Umoja Ulimwenguni Pote inatangazwa ili kuwezesha watu kufahamiana na tengenezo moja ambalo Yehova anatumia katika siku zetu ili kutimiza mapenzi yake. Funzo litakapokuwa limesitawi vizuri, kwa nini kutotoa nakala moja kwa mwanafunzi? Tangu tu mwanzoni, alika kwa ukawaida mwanafunzi kwenye mikutano. Umwambie jinsi inavyoendeshwa. Unaweza kumtolea kichwa cha hotuba ijayo na kumwonyesha nakala itakayochunguzwa wakati wa funzo la Mnara wa Mlinzi. Labda itawezekana kwako kumwonyesha Jumba la Ufalme wakati hakuna mikutano, ili kupunguza woga wake iwezekanavyo wa kwenda mahali papya kwa mara ya kwanza. Bila shaka utaweza kumpendekezea kumpeleka kwenye mikutano. Anapokuja, umstareheshe ili ajisikie mwenye kukaribishwa. (Mt. 7:12) Umwonyeshe kwa Mashahidi wengine, kutia na wazee. Tunatumaini kwamba ataanza kuona kutaniko kama familia ya kiroho. (Mt. 12:49, 50; Mk. 10:29, 30) Ungeweza kumwekea mradi wa kufikia hatua kwa hatua, kama vile kuhudhuria kwenye mkutano kila juma.—Ebr. 10:24, 25.
16 Huku funzo linapoendelea katika kitabu Ujuzi, tia mkazo juu ya sehemu zinazoonyesha ulazima wa kushirikiana kikawaida na kutaniko wakati wa mikutano. Kazia hasa kurasa 52, 115, 137-9, 159, pia na sura 17. Onyesha hisia-moyo za kina kirefu za shukrani unazohisi mwenyewe kuelekea tengenezo la Yehova. (Mt. 24:45-47) Sema katika maneno ya kusifu kutaniko lenu na ya yale mnayojifunza kwenye mikutano. (Zab. 84:10; 133:1-3) Ingekuwa vizuri mwanafunzi aweze kuona kasetivideo za Sosaiti, kwa kuanza na Les Témoins de Jéhovah — Un nom, une organisation. Utapata mawazo ya ziada juu ya namna ya kuongoza watu kwenye tengenezo katika Mnara wa Mlinzi wa Aprili 1, 1985, kur. 8-12, na katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Agosti 1993.
17 Tia Wanafunzi Moyo Kutoa Ushuhuda kwa Wengine: Tunapojifunza pamoja na watu, mradi wetu ni kuwafanya wanafunzi watakaoshuhudia kwa ajili ya Yehova. (Is. 43:10-12) Hilo humaanisha kwamba mwalimu anapaswa kumtia mwanafunzi moyo kuzungumzia wengine yale anayojifunza katika Biblia. Tunaweza kufanya hivyo kwa namna iliyo rahisi kwa kuuliza: “Jinsi gani ungeweza kufasiria kweli hii kwa familia yako?” au “Ni maandiko gani ungetumia ili kuonyesha hilo kwa rafiki?” Toa maandiko ya muhimu ya kitabu Ujuzi yanayotia moyo ushuhuda, kama kwenye kurasa 22, 93-5, 105-6, na pia katika sura 18. Ikiwa ni yenye kupatana, inawezekana kumpa mwanafunzi trakti fulani fulani ambazo atatumia kwa kutoa ushuhuda wa vivi hivi. Umwombe aalike washiriki wa familia yake kuhudhuria kwenye funzo. Je! ana marafiki ambao wangependa pia kujifunza Biblia? Umwambie akujulishe wale ambao hilo linapendeza.
18 Kwa kuhudhuria kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na kwenye mkutano wa utumishi, atakayekuwa mfuasi atapata mazoezi na vitia moyo vya ziada vitakavyomsaidia kuwa mhubiri wa habari njema. Ikiwa anaonyesha nia ya kujiandikisha kwenye shule au kuwa mhubiri asiyebatizwa, inastahili kufuata kanuni zinazotolewa katika kitabu Huduma Yetu, kurasa 97-99. Ikiwa hatimizi matakwa yanayoombwa katika sehemu fulani ya maisha yake, mnaweza kutafuta katika vichapo vya Sosaiti mawazo ya lazima yanayozungumzia ulizo hilo na kumjulisha hilo. Kwa mfano, inawezekana kwamba mwanafunzi ana magumu ya kuachana na hali ya kuwa chini ya utumwa wa tumbaku au dawa nyingine za kulevya. Kitabu Kutoa Sababu kinaonyesha sababu imara za kibiblia kupitia hizo Wakristo wanapaswa kuachana na mazoea hayo mabaya na kinaonyesha kwenye ukurasa 62 ufundi ambao ulionekana wenye matokeo ili kuachana na dawa za kulevya. Sali pamoja naye kuhusu tatizo hilo na umfundishe kumtegemea zaidi na zaidi Yehova ili kupokea msaada.—Yak. 4:8.
19 Utaratibu wa kufuata ili kujua ikiwa mtu anatimiza matakwa yanayoombwa ili kushiriki katika huduma ya peupe unaonyeshwa katika Mnara wa Mlinzi wa Januari 15, 1996, uku. 16 fu. 6. Mwanafunzi anapotimiza matakwa yanayoombwa, ni jambo lenye kupatana kufanya kipindi cha mazoezi ili kumtayarisha kwa siku yake ya kwanza ya mahubiri. Kwa namna yenye kujenga, zungumzia jinsi mbalimbali ya kuitikia na vizuia-mazungumzo vya kawaida kwa watu wa eneo lenu. Kwanza kabisa, anza naye na mahubiri ya mlango kwa mlango kwa kadiri iwezekanavyo, na umzoeze baadaye hatua kwa hatua katika aina nyingine za huduma. Ikiwa utoaji wako habari unabaki mfupi na mwepesi, itakuwa rahisi kwake kukuiga. Uwe mwenye kujenga na mwenye kutia moyo, onyesha shangwe katika mahubiri; ataweza hivyo kutambua hali yako ya akili na kuionyesha. (Mdo. 18:25) Mfuasi mpya angepaswa kuwa na mradi wa kuwa mhubiri aliye kawaida na mwenye bidii ya habari njema. Unaweza bila shaka kumsaidia kupanga programu nzuri ya mahubiri. Ili kumsaidia kufanya maendeleo katika namna yake ya kutoa ushuhuda, unaweza kumdokezea (kumshauri) kusoma makala ya Mnara wa Mlinzi wa Januari 15, 1985, kur. 12-17; Julai 15, 1988, kur. 9-20; Januari 15, 1991, kur. 15-20 na Januari 1, 1994, 20-5.
20 Tia Wanafunzi Moyo Kujiweka Wakfu kwa Mungu na Kubatizwa: Mwanafunzi mnyofu angepaswa kuweza kujifunza mengi wakati wa funzo la kitabu Ujuzi ili kujiweka wakfu kwa Mungu na kutimiza matakwa yanayoombwa kwa ajili ya ubatizo. (Ona Matendo 8:27-39; 16:25-34.) Hata hivyo, kabla mtu fulani awe na nia ya kujiweka wakfu kwa Mungu, anapaswa kuwa amekomaza ushikamanifu wa kina kirefu kwa Yehova. (Zab. 73:25-28) Muda wote wa funzo, tafuta nafasi za kujenga shukrani kuelekea Yehova kwa ajili ya sifa zake. Onyesha hisia-moyo za kina kirefu unazohisi kuelekea Mungu. Saidia mwanafunzi kufikiri kwa namna ambayo, anaweza kukomaza uhusiano wa kibinafsi na wenye shauku pamoja na Yehova. Ikiwa anafikia kwelikweli kumjua na kumpenda Mungu, atamtumikia hivyo kwa uaminifu, kwani ushikamanifu kwa Mungu unahusiana na namna ambayo tunaona utu wa Yehova.—1 Tim. 4:7, 8; ona Kiongozi cha Shule, uku. 76 fu. 11.
21 Jikaze kugusa moyo wa mwanafunzi. (Zab. 119:11; Mdo. 16:14; Rum. 10:10) Ni jambo la lazima kwamba aone ni katika njia gani ukweli unamgusa kibinafsi na kwamba anaamua jinsi anaweza kutumia yale aliyojifunza. (Rum. 12:2) Je! anauamini kabisa ukweli anaotolewa juma baada ya juma (1 Thess. 2:13)? Ili kujua hilo, unaweza kumuuliza maulizo ya maoni yenye akili, kama haya: Wewe unafikiri nini? Jinsi gani unaweza kutumikisha hilo katika maisha yako? Kwa msaada wa maelezo hayo, utaweza kutambua hali ndani yazo ungepaswa kumsaidia zaidi ili kugusa moyo wake. (Lk. 8:15; ona Kiongozi cha Shule, uku. 52 fu. 11) Maandishi ya picha za kurasa 172 na 174 za kitabu Ujuzi yanauliza: “Je, umejiweka wakfu kwa Mungu katika sala?” na “Nini kinachokuzuia usibatizwe?” Maulizo hayo yanaweza kumsukuma mwanafunzi kutenda.
22 Namna ya kutenda wakati mhubiri anapotamani kubatizwa inaelezwa katika Mnara wa Mlinzi wa Januari 15, 1996, uku. 17 fu. 9. Kitabu Ujuzi kilitayarishwa kwa kusudi la kuwezesha mtu kujibu kwenye “Maswali ya Kuuliza Wanaotaka Kubatizwa”. Maulizo hayo, ambayo wazee watachunguza pamoja naye, yanapatikana katika nyongeza ya kitabu Huduma Yetu. Ikiwa uliweka mkazo juu ya maulizo yanayochapwa katika kitabu Ujuzi, mwanafunzi atakuwa tayari kwa ajili ya mazungumzo mbalimbali atakayokuwa nayo pamoja na wazee kwa ajili ya ubatizo.
23 Tuwasaidie Wale Waliomaliza Funzo lao la Biblia: Inatazamiwa kwamba mtu anayefika mwisho wa funzo la kitabu Ujuzi awe ameonyesha waziwazi unyofu wake na tamaa yake ya kina kirefu ya kutumikia Mungu. (Mt. 13:23) Ni kwa sababu hiyo kichwa kidogo cha habari kinachomalizia kitabu kinatokeza ulizo hili: “Utafanya Nini?” Mafungu ya mwisho-mwisho yanatia mwanafunzi moyo kufikiria uhusiano ambao angepaswa kuwa amekuza pamoja na Mungu, kwa ulazima wa kutumikisha ujuzi anaopata na kwa umuhimu wa kutenda bila kuchelewa ili kuonyesha upendo wake kwa Yehova. Haikusudiwi kwamba tujifunze vitabu vingine pamoja na watu wanaomaliza kitabu Ujuzi. Ikiwa mwanafunzi haitikii kwa ujuzi wa Mungu, umueleweshe kwa upole na waziwazi yale anapaswa kufanya ili aendelee kiroho. Utaweza kumwona tena mara kwa mara, ukimwachia hivyo mlango wazi ili apige hatua zitakazomwongoza kwenye uhai udumuo milele.—Mh. 12:13.
24 Mfuasi mpya anayekubali ukweli na kubatizwa atapaswa tena kukomaa katika ujuzi na katika uelewevu kabla ya kusitawi kabisa kabisa katika imani. (Kol. 2:6, 7) Baada ya kumaliza kitabu Ujuzi, badala ya kuendelea na funzo lake la Biblia la nyumbani, unaweza kuwa tayari kumtolea msaada wa kibinafsi ambao labda atahitaji ili kupata ukomavu wa kiroho. (Gal. 6:10 ; Ebr. 6:1) Kwa upande wake, anaweza kuongeza uelewevu wake kwa kusoma Biblia kila siku, kwa kujifunza kibinafsi Mnara wa Mlinzi na vichapo vingine vya ‘mtumwa mwaminifu’, kwa kujitayarisha kwa ajili ya mikutano na kwa kuihudhuria, na kwa kuzungumza ukweli pamoja na washiriki wenzake katika imani. (Mt. 24:45-47; Zab. 1:2; Mdo. 2:41, 42; Kol. 1:9, 10) Ili apange mambo yake vizuri kwa kusudi la kutimiza kikamilifu huduma yake kwa namna ya kitheokrasi, itakuwa lazima kwamba asome kitabu Huduma Yetu na kwamba afuate mapendekezo yake.—2 Tim. 2:2 ; 4:5.
25 Tukuze Ufundi wa Kufundisha: Tulipokea kazi ya ‘kufanya wanafunzi, na kuwafundisha’. (Mt. 28:19, 20.) Kwa kuwa ufundi wa kufundisha ni wa lazima ili kufanya wanafunzi, tunataka tujikaze ili kuwa walimu bora kabisa. (1 Tim. 4:16; 2 Tim. 4:2) Kwa madokezo mengine juu ya namna ya kukomaza ufundi wa kufundisha, labda utatamani kusoma: “Kusitawisha Ustadi wa Kufundisha” na “Kuufikia Moyo wa Wasikilizaji Wako” katika kitabu Kiongozi cha Shule, masomo 10 na 15; “Enseignant, enseignement” (Mwalimu, mafundisho) katika Auxiliaire; na makala ya Mnara wa Mlinzi: “Kujenga kwa Vitu Visivyoweza Kuchomwa na Moto” na “Unapofundisha, Fikia Moyo”, Januari 1, 1985; “Je! Wewe Ni Mwenye Matokeo Katika Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko?”, Machi 1, 1986; na ‘Wanapata Shangwe kwa Kufanya Wanafunzi’, Februari 15, 1996.
26 Huku mnapojikaza kufanya wanafunzi kwa msaada wa kitabu Ujuzi, salini Yehova kwa kuendelea, Yeye “anayekomaza”, ili kwamba abariki bidii ambayo mnafanya ili kugusa mioyo kwa njia ya habari njema ya Ufalme. (1 Kor. 3:5-7) Basi na mpate shangwe ambayo mtu hujipatia kwa kufundisha wengine kuelewa ujuzi uongozao kwenye uhai udumuo milele, na pia kutambua thamani yake na kutenda kupatana na ujuzi huo!