Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 9/05 uku. 3-6
  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Vichapo Vinavyopendekezwa
  • Jinsi ya Kujitayarisha
  • Patanisha Somo na Mahitaji ya Mwanafunzi
  • Fundisha Mambo Yanayotoka Katika Neno la Mungu
  • Kupiga Kistari Chini ya Majibu na Kuandika Maelezo Pembeni
  • Mwono wa Jumla na Kurudilia
  • Jenga Imani Thabiti
  • Tumia Ufahamu
  • Uwe Mwenye Kiasi
  • Jinsi ya Kuanza Funzo kwa Sala
  • Mambo ya Kutia Katika Sala
  • Mikutano ya Kutaniko
  • Tumia Vidio Ili Kuongeza Uthamini Wao
  • Uwatie Moyo Watoe Ushahidi
  • Wazoeze Waelezee Wengine
  • Kutayarisha Pamoja
  • Kuhubiri Pamoja
  • Kujitayarisha kwa Ajili ya Kurudia
  • Kufuatia Kupendezwa kwa Bidii
  • Kutolea Watu Funzo la Biblia
  • Kuzoeza Wanafunzi Kuwa Walimu
  • Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Kwanza
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Saidia Mwanafunzi Wako wa Biblia Afikie Kubatizwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Pili
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Ujitayarishe Vizuri Ili Kufundisha
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2005
km 9/05 uku. 3-6

Ichungwe

Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo

Nyongeza hii ni mkusanyo wa mambo makuu kutoka mfululizo wa makala kuhusu Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo ambayo yametokea katika Huduma Yetu ya Ufalme. Sote tunatiwa moyo kuchunga nyongeza hii na kuichunguza tunapoongoza mafunzo ya Biblia. Kwa kuongezea, mambo kutoka nyongeza hii yanaweza kukaziwa mnamo mikutano kwa ajili ya utumishi wa shambani, na waangalizi wa utumishi wanaweza kuyatumia kuwa msingi wa hotuba wanazofanya wakati wanapotembelea vikundi vya funzo la kitabu.

Sehemu 1: Funzo la Biblia Ni Nini?

Ikiwa una mazungumzo, hata mafupi, ya Biblia pamoja na mtu mwenye kupendezwa, na ikiwa unazungumzia kwa ukawaida na kwa utaratibu habari fulani ukitumia Biblia na kimoja cha vichapo vinavyopendekezwa, unaongoza funzo la Biblia. Hilo ni kweli hata ikiwa funzo linafanyika mlangoni au kwa njia ya simu. Funzo linaweza kuripotiwa ikiwa limeongozwa mara mbili baada ya kumwonyesha mtu jinsi ya kujifunza na ikiwa kuna sababu inayosadikisha kwamba funzo hilo halitakatizwa.—km 7/04 uku. 1.

Vichapo Vinavyopendekezwa

◼ Mungu Anataka Nini Kwetu?

◼ Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele

◼ Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli

◼ Broshua Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu! inaweza kutumiwa ili kujifunza pamoja na watu walio na ujuzi mdogo au uwezo mdogo wa kusoma.

Sehemu 2: Kujitayarisha Ili Kuongoza Funzo

Tunapaswa kutoa habari kwa namna inayogusa moyo wa mwanafunzi. Hilo linaomba kujitayarisha kabisa tukifikiria mahitaji ya mwanafunzi.—km 8/04 uku. 1.

Jinsi ya Kujitayarisha

◼ Chunguza kichwa cha habari, vichwa vidogo, na picha za sura au somo.

◼ Pata kutambua majibu ya maulizo yenye kuchapishwa, ukitia alama maneno makuu tu na pia fungu la maneno.

◼ Amua ni maandiko gani utakayosoma wakati wa funzo. Andika maelezo mafupi kandokando ya maandishi katika kichapo cha funzo.

◼ Tayarisha kurudilia kwa kifupi mambo makuu.

Patanisha Somo na Mahitaji ya Mwanafunzi

◼ Sali kwa ajili ya mwanafunzi na mahitaji yake.

◼ Fikiria kimbele mambo ambayo yanaweza kuwa vigumu kwa mwanafunzi kuelewa au kukubali.

◼ Fikiria: Ni jambo gani anahitaji kuelewa au kutengeneza katika maisha yake ili kufanya maendeleo ya kiroho? Ninawezaje kufikia moyo wake?

◼ Inapohitajiwa, tayarisha mfano, elezo fulani, au mfululizo wa maulizo ili kusaidia mwanafunzi aelewe maana ya jambo au andiko fulani.

Sehemu 3: Matumizi Yenye Matokeo ya Maandiko

Tunapoongoza mafunzo ya Biblia mradi wetu ni “kufanya wanafunzi” kwa kusaidia watu waelewe na kukubali mafundisho ya Neno la Mungu na kuyatumia katika maisha zao. (Mt. 28:19, 20; 1 The. 2:13) Kwa hiyo, funzo linapaswa kutegemea Maandiko.—km 11/04 uku. 4.

Fundisha Mambo Yanayotoka Katika Neno la Mungu

◼ Onyesha mwanafunzi jinsi ya kupata maandiko kamili katika nakala yake mwenyewe ya Biblia.

◼ Tafuta na mzungumzie maandiko ya Biblia yanayoonyesha msingi wa Kimaandiko wa mambo tunayoamini.

◼ Tumia maulizo. Badala ya kufafanulia mwanafunzi maandiko ya Biblia, mwombe yeye akufafanulie maandiko hayo.

◼ Fanya andiko liwe rahisi. Usijaribu kueleza kila sehemu ya andiko. Tia ndani tu mambo yanayohitajiwa ili kufanya habari mnayojifunza ieleweke.

◼ Fanya matumizi yanayofaa. Saidia mwanafunzi kuona jinsi maandiko ya Biblia yanavyomhusu kibinafsi.

Sehemu 4: Kuzoeza Wanafunzi Kutayarisha Funzo

Mwanafunzi anayesoma kimbele somo litakalochunguzwa, anayepiga kistari chini ya majibu, na anayefikiri jinsi ya kujibu katika maneno yake mwenyewe anafanya maendeleo ya kiroho kwa haraka. Kwa hiyo, mara tu funzo la kawaida litakapokuwa limeanzishwa, tayarisha somo pamoja na mwanafunzi ili kumwonyesha jinsi ya kutayarisha. Kuhusu wanafunzi wengi, litakuwa jambo lenye kusaidia kutayarisha sura au somo nzima pamoja.—km 12/04 uku. 1.

Kupiga Kistari Chini ya Majibu na Kuandika Maelezo Pembeni

◼ Umueleze jinsi ya kupata majibu ya moja kwa moja ya maulizo yenye kuchapishwa.

◼ Onyesha mwanafunzi kichapo chako cha funzo ambamo umepiga kistari chini ya maneno makuu au fungu la maneno.

◼ Umsaidie aone kwamba kila andiko linaloonyeshwa na ambalo halitajwi moja kwa moja linategemeza jambo fulani katika fungu, na kumwonyesha jinsi ya kuandika maelezo kwa kifupi pembeni katika kichapo chake cha funzo.

Mwono wa Jumla na Kurudilia

◼ Onyesha mwanafunzi jinsi ya kuchunguza kichwa cha sura au cha somo, vichwa vidogo, na picha kabla ya kuanza kutayarisha habari ya funzo kwa undani.

◼ Tia mwanafunzi moyo kurudilia mambo makuu akimaliza kujitayarisha.

Sehemu 5: Kukadiria Kiasi cha Habari ya Kujifunza

Kiasi cha habari ya kujifunza kitategemea uwezo na hali za mwalimu na mwanafunzi.—km 1/05 uku. 1.

Jenga Imani Thabiti

◼ Ni jambo la maana sana kusaidia mwanafunzi aelewe habari waziwazi kuliko kujifunza habari nyingi kwa wakati mfupi.

◼ Pitisha wakati wowote unaohitajiwa ili kusaidia mwanafunzi kuelewa na kukubali mambo anayojifunza.

◼ Chukua wakati wa kutosha ili kuchunguza maandiko ya msingi ambayo yanategemeza mafundisho.

Kushikamana na Habari Mnayojifunza

◼ Ikiwa mwanafunzi anaelekea kusemea sana mambo yake ya kibinafsi, unaweza kufanya mpango ili kuzungumzia mambo hayo baada ya funzo.

◼ Epuka kusema sana wakati wa funzo. Epuka kuzungumzia zaidi mambo madogo na yale yaliyoonwa ili kwamba yasizuie mwanafunzi kutwaa ujuzi sahihi wa mafundisho ya Biblia ya msingi.

Sehemu 6: Wakati Mwanafunzi Anapotokeza Ulizo

Wakati funzo la Biblia linapoanzishwa vizuri, kwa kawaida ni vizuri zaidi kuchunguza mafundisho ya Biblia katika njia yenye utaratibu badala ya kurukaruka habari. Hilo linasaidia mwanafunzi ajenge msingi wa ujuzi sahihi na kuendelea kiroho.—km 2/05 uku. 6.

Tumia Ufahamu

◼ Maulizo yanayohusiana na habari mnayojifunza yanaweza kujibiwa hapohapo.

◼ Maulizo yasiyohusiana na mambo mnayojifunza au yanayoomba kufanya utafiti yanaweza kuchunguzwa wakati mwingine. Litakuwa jambo lenye kusaidia kuandika maulizo kama hayo.

◼ Ikiwa mwanafunzi ana magumu ya kukubali mafundisho fulani, chunguza habari ya ziada ambayo inazungumzia kikamili jambo hilo.

◼ Ikiwa bado mwanafunzi hasadiki, mnaweza kuacha jambo hilo pembeni ili kulizungumzia wakati mwingine na hivyo kuendelea na funzo lenu.

Uwe Mwenye Kiasi

◼ Ikiwa haujui jibu la ulizo, usijaribu kutoa maoni yako.

◼ Fundisha mwanafunzi hatua kwa hatua jinsi ya kufanya utafiti.

Sehemu 7: Kutoa Sala Kwenye Funzo

Ili wanafunzi wa Biblia wafanye maendeleo ya kiroho, baraka ya Yehova inahitajiwa. Kwa hiyo, ni jambo lenye kufaa kuanza na kumaliza funzo kwa sala.—km 3/05 uku. 6.

Jinsi ya Kuanza Funzo kwa Sala

◼ Kwa wale walio na mwelekeo wa kidini, mara nyingi sala inaweza kutolewa kwenye funzo la kwanza kabisa.

◼ Kwa wengine, tunahitaji kuwa na utambuzi ili kujua wakati unaofaa wa kuanza funzo kwa sala.

◼ Maandiko ya Zaburi 25:4, 5 na 1 Yohana 5:14 yanaweza kutumiwa ili kueleza kwa nini sala inatolewa.

◼ Andiko la Yohana 15:16 linaweza kutumiwa ili kuonyesha kwamba tunapaswa kusali kwa Yehova kupitia Yesu Kristo.

Mambo ya Kutia Katika Sala

◼ Ni jambo lenye kufaa kutoa sifa kwa Yehova akiwa Chanzo cha mafundisho.

◼ Onyesha kwamba unapendezwa kikweli na mwanafunzi.

◼ Onyesha kwamba unathamini tengenezo ambalo Yehova anatumia.

◼ Omba Yehova abariki jitihada za mwanafunzi ili kutumia katika maisha yale anayojifunza.

Sehemu 8: Kuongoza Wanafunzi Kwenye Tengenezo

Mradi wetu tunapoongoza mafunzo ya Biblia si kufundisha tu mafundisho yanayohusu imani lakini pia kusaidia wanafunzi wawe sehemu ya kutaniko la Kikristo. Kila juma kwenye funzo la Biblia chukua dakika chache ili mjifunze jambo moja kuhusu tengenezo la Yehova.—km 4/05 uku. 8.

Mikutano ya Kutaniko

◼ Zungumzia mkutano mmoja mmoja. Kuanzia funzo la kwanza, uwaalike kuhudhuria.

◼ Shiriki pamoja nao mambo makuu yaliyotolewa kwenye mikutano.

◼ Ongeza shauku yao kuhusu Ukumbusho, mikusanyiko, na ziara ya mwangalizi wa mzunguko.

◼ Tumia picha katika vichapo vyetu ili kuwasaidia wawe na picha akilini ya mambo yaliyotokea.

◼ Uwatie moyo kusoma broshua Mashahidi wa Yehova, Wao Ni Nani, Wanaamini Nini?

Tumia Vidio Ili Kuongeza Uthamini Wao

◼ Les Témoins de Jéhovah : un nom, une organisation

◼ Toute la communauté des frères

◼ Unis grâce à l’enseignement divin

◼ Jusqu’aux extrémités de la terre

Sehemu 9: Kutayarisha Wanafunzi Kutoa Ushahidi wa Vivi Hivi

Wanafunzi wa Biblia wanapoanza kuamini mambo wanayojifunza, wanachochewa kusema kuhusu hayo.—km 5/05 uku. 1.

Uwatie Moyo Watoe Ushahidi

◼ Je, kuna marafiki na washiriki wa familia ambao anaweza kualika ili wahudhurie funzo lake?

◼ Je, kuna yeyote wa wafanyakazi wenzake, wanashule wenzake, au watu anaofahamiana nao wanaoonyesha kupendezwa?

Wazoeze Waelezee Wengine

Mambo Wanayoamini

◼ Mnapofikia kwenye mambo fulani uliyochagua wakati wa funzo lenu, uliza mwanafunzi, “Unawezaje kutumia Biblia ili kufafanua kweli hii kwa familia yako?”

◼ Saidia mwanafunzi kuelewa uhitaji wa kuwa mwenye adabu na fadhili anapozungumza na wengine kuhusu Mungu na makusudi yake.

◼ Broshua Mashahidi wa Yehova—Wao Ni Nani? Wanaamini Nini? Inaweza kutumiwa na wanafunzi ili kusaidia rafiki na washiriki wa familia waelewe mambo ya msingi ya Biblia tunayoamini na pia utendaji wetu mbalimbali.

Sehemu 10: Kuzoeza Wanafunzi Katika Huduma ya Nyumba kwa Nyumba

Wakati ambapo wazee wanaamua kwamba mwanafunzi wa Biblia anastahili kuwa mhubiri asiyebatizwa, anaweza kuanza kushiriki pamoja na kutaniko katika kazi ya kuhubiri waziwazi.—km 6/05 uku. 1.

Kutayarisha Pamoja

◼ Umwonyeshe mhubiri mpya mahali anapoweza kupata utoaji uliopendekezwa.

◼ Umsaidie kuchagua utangulizi ulio rahisi na wenye kufaa eneo lenu.

◼ Umtie moyo kukazia Biblia katika huduma yake.

◼ Mjizoeze pamoja. Umwonyeshe jinsi ya kushughulikia kwa busara hali mbalimbali ambazo ni za kawaida katika eneo.

Kuhubiri Pamoja

◼ Acha mwanafunzi atazame jinsi unavyotoa utangulizi ambao ninyi wawili mlitayarisha pamoja.

◼ Ufikirie utu na uwezo wa mwanafunzi. Katika visa fulani, lingekuwa jambo bora kumwomba ahubiri tu kidogo akitumia sehemu ya utoaji.

◼ Umsaidie mhubiri mpya kufanya programu ya kawaida ili kushiriki katika huduma.

Sehemu 11: Kusaidia Wanafunzi Kufanya Ziara za Kurudia

Kujitayarisha kwa ajili ya ziara ya kurudia kunaanza wakati wa ziara ya kwanza. Mtie moyo mwanafunzi apendezwe kwa unyofu na wale anaozungumza nao. Hatua kwa hatua umzoeze mhubiri mpya kuomba watu anaozungumza nao watoe mawazo yao, asikilize maelezo yao, na kutambua mambo yanayowahangaisha.—km 7/05 uku. 1.

Kujitayarisha kwa Ajili ya Kurudia

◼ Chunguza maandishi ya ziara ya kwanza, na usaidie mwanafunzi kuchagua habari itakayovutia mwenye nyumba.

◼ Tayarisheni pamoja utoaji mfupi unaokazia andiko moja la Biblia pamoja na fungu moja katika kichapo cha funzo.

◼ Tayarisha ulizo moja linaloweza kutokezwa wakati wa umalizio wa mazungumzo.

Kufuatia Kupendezwa kwa Bidii

◼ Mtie moyo mwanafunzi kurudilia bila kukawia watu wote wanaoonyesha kupendezwa.

◼ Saidia mwanafunzi kuona uhitaji wa kudumu katika kujaribu kufikia wale ambao ni vigumu kuwapata.

◼ Mwonyeshe mhubiri mpya jinsi ya kufanya mipango ili kurudilia tena watu, na kumsaidia aelewe uhitaji wa kurudi kama ilivyoahidiwa.

Sehemu 12: Kusaidia Wanafunzi Kuanzisha na Kuongoza Mafunzo ya Biblia

Kumwiga Yesu kwa kuweka mfano unaofaa katika huduma yako ni jambo la maana. Mwanafunzi anapotazama mfano wako katika huduma, ataelewa kwamba mradi katika kufanya ziara za kurudia ni kuanzisha mafunzo ya Biblia.—km 8/05 uku. 1.

Kutolea Watu Funzo la Biblia

◼ Mwelezee mwanafunzi kwamba kwa kawaida si lazima kueleza mpango wa funzo kwa kirefu.

◼ Mara nyingi ni jambo bora kuonyesha tu jinsi ya kuongoza funzo kwa kutumia labda fungu moja au mafungu mawili kutoka kitabu cha funzo.

◼ Rudilieni na mfanye mazoezi ya mapendekezo kwa ajili ya kuanzisha mafunzo ya Biblia.—km 8/05 uku. 8; km 1/02 uku. 6.

Kuzoeza Wanafunzi Kuwa Walimu

◼ Uwatie wanafunzi moyo wajiandikishe kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi.

◼ Fanya mpango ili wahubiri wapya waandamane nawe kwenye mafunzo mengine ya Biblia ambapo wanaweza kushiriki kwa kiasi kidogo katika mafundisho.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine