Ujitayarishe Vizuri Ili Kufundisha
1. Tunapoongoza funzo la Biblia, kwa nini tunapaswa kujikaza kumsaidia mwanafunzi apendezwe na mambo anayojifunza?
1 Tunapoongoza funzo la Biblia, tunapaswa kujitayarisha vizuri ikiwa tunataka kumchochea mwanafunzi amtumikie Yehova. Tutapata matokeo mazuri ikiwa tunajikaza ili kumsaidia mwanafunzi apendezwe na mambo anayojifunza katika Biblia. Hilo litamchochea kabisa. (Kum. 6:5; Met. 4:23; 1 Kor. 9:26) Tunaweza kumsaidia namna gani?
2. Jinsi gani sala inaweza kutusaidia kujitayarisha vizuri kwa ajili ya funzo?
2 Tusali Tunapotayarisha Funzo: Kwa kuwa ni Yehova ndiye anayefanya mbegu ya kweli ikomae katika moyo wa mwanafunzi, ni jambo lenye kufaa kusali kwanza kwa ajili ya mwanafunzi na mahitaji yake ya pekee tunapotayarisha funzo. (1 Kor. 3:6; Yak. 1:5) Sala hiyo inaweza kutusaidia pia tujue kile tunachoweza kufanya zaidi ili kumsaidia mwanafunzi ajaze moyo wake ‘na ujuzi sahihi’ wa mapenzi ya Yehova.—Kol. 1:9, 10.
3. Namna gani tunaweza kufikiria mwanafunzi wetu tunapojitayarisha kwa ajili ya funzo?
3 Fikiria Mwanafunzi: Yesu alijua kwamba ili kufundisha vizuri inaomba kufikiria wasikilizaji. Yesu aliulizwa mara mbili ulizo lilelile, aliulizwa hivi: “Nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?” Yesu alijibia ulizo hilo kwa njia tofauti. (Luka 10:25-28; 18:18-20) Tunapaswa kufikiria mambo ambayo mwanafunzi anahitaji kujifunza tunapojitayarisha. Ni maandiko gani yanayotajwa ambayo tutasoma pamoja naye? Ni vifungo vingapi ambavyo tutajifunza naye? Ni mambo gani ambayo mwanafunzi anaweza kuwa na magumu ya kuelewa na kukubali? Ikiwa tunafikiria mbele ya wakati maulizo fulani ambayo mwanafunzi anaweza kuuliza, tutakuwa tayari kumtolea majibu yanayofaa.
4. Kujitayarisha vizuri kunatia ndani nini?
4 Rudilia Habari: Hata ikiwa tumejifunza habari mara nyingi kadiri gani, itakuwa mara ya kwanza kujifunza habari hiyo pamoja na mwanafunzi huyo. Ikiwa tunataka kugusa moyo wake, ni jambo la maana kujitayarisha vizuri kwa ajili ya kila funzo. Hilo linamaanisha kwamba tunapomtia moyo mwanafunzi kutayarisha funzo, sisi wenyewe pia tunapaswa kujitayarisha kwa ajili ya funzo. Chunguza habari, kutia ndani maandiko yanayotajwa ukifikiria mwanafunzi, na labda piga kistari chini ya mambo makuu.—Rom. 2:21, 22.
5. Namna gani tunaweza kumwiga Yehova?
5 Yehova anapendezwa sana na maendeleo ya kila mwanafunzi wa Biblia. (2 Pet. 3:9) Ikiwa tunachukua wakati wa kujitayarisha kwa ajili ya kila funzo la Biblia, tutaonyesha kwamba tunahangaikia kwa upendo mwanafunzi wa Biblia.