Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 12/96 uku. 1-5
  • Tunayo Kazi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tunayo Kazi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Namna Yehova Anatusaidia Kutimiza Kazi Yetu ya Kuhubiri
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Sababu gani Mashahidi wa Yehova wanahubiri nyumba kwa nyumba?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Habari Njema Iko Nahubiriwa Namna Gani?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • “Muende, na Mufanye Wanafunzi”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 12/96 uku. 1-5

Tunayo Kazi

1 Yesu aliomba kwa wale wanaomfuata kufanya “wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote.” (Mt. 28:​19, TUM) Zaidi ya milioni tano ya waabudu wa Yehova Mungu ni ushuhuda ulio hai wa utimizo wa amri hiyo katika nchi na visiwa 232. Lakini namna gani sisi hasa? Je! tunachukua kwa uzito kazi ya kuhubiri?

2 Wajibu wa Kiadili: Kazi ni “daraka linalokabidhiwa mtu kwenda kutimiza jambo fulani.” Kristo alitutolea amri ya kuhubiri. (Mdo. 10:42) Mtume Paulo alitambua kwamba aliwekewa, kwa amri hiyo, sharti, au wajibu wa kiadili, wa kutangaza habari njema. (1 Kor. 9:16) Tutoe mfano wa hilo: Fikiri kwamba wewe ni mwanamaji juu ya mashua inayozama polepole. Kapteni anakuamuru kuarifu wasafiri na kuwaongoza kwenye mashua ndogo ya kuokolea. Je! utapuuza amri hiyo na kuhangaikia tu kuokoa uhai wako? Bila shaka hapana. Kupona au kufa kwa watu wengine ni katika mikono yako. Uhai wao ni hatarini. Uko katika wajibu wa kiadili wa kutimiza kazi yako inayohusu kuwasaidia.

3 Tulipokea kazi ya kimungu ya kutoa onyo. Hivi karibuni Yehova atakomesha mfumo wote mwovu wa mambo ya sasa. Kufa au kupona kwa mamilioni ya watu hakujulikani. Je! lingekuwa jambo lenye kufaa kwamba tusijali hatari yoyote ambayo majirani zetu wanakabiliana nayo huku tukishughulikia tu wokovu wetu wenyewe? Bila shaka hapana. Tunao wajibu wa kiadili wa kusaidia jirani yetu kuokoa uhai wake.—1 Tim. 4:16.

4 Vielelezo vya Uaminifu vya Kuigwa: Nabii Ezekieli alikuwa akiona kwamba alikuwa na wajibu wa kutoa ujumbe wenye onyo kwa Waisraeli wasio waaminifu. Yehova alimuonya waziwazi yale ambayo yangetukia ikiwa hangetimiza daraka lake: “Kama nikimwambia mwovu: ‘Hakika utakufa’; nawe humupi maonyo . . . , yule mwovu atakufa katika uovu wake; lakini damu yake nitataka mukononi mwako.” (Ezek. 3:18) Ezekieli alitimiza kiaminifu kazi yake, hata mbele ya upinzani mkubwa. Hata hivyo, aliweza kufurahi wakati hukumu za Yehova ziliweza kutekelezwa.

5 Karne nyingi baadaye, mtume Paulo alizungumzia daraka lake la kuhubiri. Alisema: “Mimi ni safi kutokana na damu ya watu wote, kwa maana sikuepuka kuwaambia nyingi shauri lote la Mungu.” Paulo alihubiri hadharani na nyumba kwa nyumba kwani alitambua kwamba kwa kuwa mpuuzi kwa upande huo angejitwika deni ya damu mbele za Mungu.​—Mdo. 20:​20, 26, 27, TUM.

6 Je! sisi ni mwenye bidii kama vile Ezekieli? Je! tunajisikia kusukumwa kuhubiri kwa mfano wa Paulo? Kazi yetu ni ileile. Tunapaswa kuendelea kutimiza daraka letu la kuonya majirani zetu ingawa hali yao ya uzembe, ubariki na upinzani. Inawezekana kwamba maelfu ya watu wakubali tena ujumbe wa Ufalme na kusema: “Tutakwenda pamoja nanyi, kwa maana tumesikia ya kuwa Mungu ni pamoja nanyi.” (Zek. 8:23) Basi na upendo wetu kwa Mungu na kwa jirani yetu utusukume kutoacha! Tunayo kazi: kuhubiri!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine