Mikutano Ya Utumishi Ya Desemba
Juma Toka Desemba 2
Wimbo 29
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyochaguliwa ya Huduma Yetu ya Ufalme. Eleza juu ya ripoti ya utumishi ya nchi (ikiwa inapatikana) na pia ile ya kutaniko ya mwezi wa nyuma.
Dak. 15: “Je! Tunalitumia Sawasawa Neno la Mungu?” Kwa maulizo na majibu. Toa pia maelezo fulani juu ya kitabu Kutoa Sababu, kwenye kichwa kidogo “Sababu za Kutufanya Tuichunguze Biblia,” kurasa 40-1.
Dak. 20: “Hii Yamaanisha Uhai Udumuo Milele.” (Maf. 1-5). Baada ya maneno mafupi ya utangulizi yanayotegemea fungu 1, omba wahubiri wawili wenye uwezo kutoa kwa njia ya onyesho vielelezo vya mafungu 2-5. Tia mkazo kwamba mradi ni kuanzisha mafunzo ya Biblia.
Wimbo 128 na sala ya mwisho.
Juma Toka Desemba 9
Wimbo 40
Dak. 10: Matangazo. Hali ya akaunti.
Dak. 20: Kwa Nini Kumpa Yehova? Mazungumzo kati ya wazee wawili yanayokazia nukta kubwa za makala kwenye kurasa 28-31 za Mnara wa Mlinzi wa Novemba 1, 1996. Habari hizo zinaweza pia kutolewa na mzee kama vile hotuba.
Dak. 15: “Hii Yamaanisha Uhai Udumuo Milele.” (Maf. 6-8). Zungumzia manufaa ya kutumia ufundi wa moja kwa moja ili kuanzisha mafunzo. Maonyesho ya vielelezo vinavyopatikana katika mafungu 6-7 yakifanywa na wahubiri wenye ujuzi. Alika wasikilizaji kueleza mambo yaliyoonwa ambako funzo lilianzishwa wakati tu wa kuonana kwa mara ya kwanza. Walipomtolea moja kwa moja funzo, mwanamume mmoja alijibu: “Sawa. Ingia. Ningependa kuwa na funzo.” Walianza kujifunza naye; juma lifuatalo, familia yake yote ilikuwapo, na wote walianza haraka kuhudhuria kwenye mikutano na kushiriki katika kazi ya kutoa ushuhuda [yb70 p. 241]. Tia wahudhuriaji moyo kuleta nyongeza yao ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 1996 kwenye mkutano ujao wa utumishi. Wimbo 129 na sala ya mwisho.
Juma Toka Desemba 16
Wimbo 140
Dak. 5: Matangazo.
Dak. 20: “Tunayo Kazi.” Kwa maulizo na majibu. Eleza kwa kifupi mafungu 13-16 ya Mnara wa Mlinzi wa Januari 1, 1988, kurasa 28-9.
Dak. 20: Tuongoze Mafunzo ya Biblia Yanayosonga Mbele. Hotuba itatolewa na mwangalizi wa utumishi. Ni tangu mwaka mmoja sasa tunatumia kitabu Ujuzi katika mafunzo ya Biblia. Wanafunzi bila shaka wamekwisha kukimaliza, huku wengine wameendelea vizuri katika funzo. Tulitiwa moyo kujikaza kuongoza mafunzo ya Biblia yanayowasaidia wapya kujifunza haraka ukweli, kuutumikisha katika maisha yao na kuwa washiriki wa kutaniko. Nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 1996 ilitutolea madokezo bora kabisa ili kutuwezesha kuwa walimu wenye matokeo. Chunguza upya kwa kifupi mambo fulani ambayo mtu anaweza kufanya ili kuwa mwalimu stadi katika mafundisho yake, kulingana na mafungu 3-13. Kisha kazia yale inafaa kufanya ili kuwasaidia wanafunzi kuamua kuwa upande wa ukweli, kama inavyokaziwa na mafungu 14-22. Someni mafungu 15, 17, 20-1. Chunguza mambo fulani yaliyoonwa yenye kupendeza yanayoonyesha matokeo mazuri ambayo wahubiri wa kutaniko walipata. Toa vitia moyo vitakavyochochea zaidi akina ndugu kuongoza mafunzo ya Biblia.
Wimbo 85 na sala ya mwisho.
Juma Toka Desemba 23
Wimbo 46
Dak. 5: Matangazo. Zungumzia mipango iliyochukuliwa kwa ajili ya mahubiri Desemba 25 ambayo ni siku ya sikukuu.
Dak. 15: “Kusonga Mbele Kwako Kuwe Wazi!” Hotuba itakayotolewa na mzee.
Dak. 10: Majibu kwa Maulizo Yenu. Mazungumzo na wasikilizaji.
Dak. 15: Vitabu tutakavyotolea mnamo Januari tutatolea Tafsiri ya Ulimwengu Mpya na kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? Kwa msaada wa kitabu “Kila Andiko,” kurasa 327-31, onyesha ukubwa wa Tafsiri ya Ulimwengu Mpya: inategemeza na kulitukuza jina la Mungu (maf. 1-2); tafsiri yake yenye kuchujwa inafanya maandishi kuwa yenye kueleweka zaidi (fu. 6); inaonekana kuwa chombo chenye nguvu katika huduma (maf. 22-3). Tangu mawazo ya ukurasa 189 wa kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? toleeni kielelezo cha utoaji habari na tayarisheni onyesho moja. Mipango kamili ingepaswa kuchukuliwa ili kurudi kuwaona watu walionyesha kupendezwa.
Wimbo 180 na sala ya mwisho.
Juma Toka Desemba 30
Kutaniko litatayarisha programu yalo lenyewe, kulingana na mahitaji ya mahali.