Je! Tunalitumia Sawasawa Neno La Mungu?
1 Yesu Kristo ni mwalimu mkuu ambaye dunia haijapata kuwa naye. Alikuwa akisema kwa namna ya kugusa mioyo ya watu, ya kuamsha hisia-moyo zao na alikuwa akiwatia moyo kutenda matendo mema. (Mt. 7:28, 29) Sikuzote alitegemeza mafundisho yake juu ya Neno la Mungu. (Lu. 24:44, 45) Alimtolea Yehova Mungu sifa ya yote aliyojua na alikuwa mwenye uwezo wa kufundisha. (Yn. 7:16) Yesu aliacha kielelezo bora kwa wanafunzi wake kwa namna yake ya kulitumia sawasawa Neno la Mungu.—2 Tim. 2:15.
2 Mtume Paulo yeye pia ni kielelezo kikubwa kwa habari ya kulitumia kwa matokeo Neno la Mungu. Hakuridhika tu na kusomea wengine Maandiko; alikuwa akifasiria yale aliyokuwa akisoma na alikuwa akifikiri juu yayo, akionyesha waziwazi kwa msaada wa Neno la Mungu kwamba Yesu alikuwa ndiye Kristo. (Mdo. 17:2-4) Vivyo hivyo, Apolo, mwanafunzi mfasaha (msemaji stadi), alikuwa “mwenye ujuzi mwingi katika Maandiko”; alikuwa akiyatumia sawasawa, akitoa kwa nguvu ukweli.—Mdo. 18:24, 28, TUM.
3 Tuwe Walimu wa Neno la Mungu: Katika siku zetu, wahubiri wa Ufalme wanapata matokeo bora wanapowafundisha watu wanyofu kwa kufikiri kutokana na Biblia na kwa kuitaja. Ndugu mmoja alitumia Ezekieli 18:4 na maandiko yaliyo na uhusiano nayo ili kumfanya kasisi mmoja na wanaparokia wake watatu wafikiri juu ya wakati ujao wa waovu na waadilifu. Mwishoni washiriki wa Kanisa walianza kujifunza, na mmoja wao alifikia kuukubali ukweli. Wakati mwingine tena, mtu mmoja mwenye kuitikia alimuomba dada mmoja afasirie mume wake mpinzani kwa nini Mashahidi wa Yehova hawaadhimishi Krismasi na sherehe za sikukuu. Dada alisoma katika kitabu Kutoa Sababu maandiko yanayoonyesha wazi nukta hiyo, na mwanamume huyo alikubali. Mke wake alikuwa mwenye furaha sana kwa kuitikia kwake hivi kwamba alisema: “Tutahudhuria kwenye mikutano yenu.” Na mume alikubali!
4 Tutumie Msaada Tunaotolewa: Huduma Yetu ya Ufalme na programu ya mkutano wa utumishi vinatutolea mashauri bora ili kutusaidia kutumia Neno la Mungu. Wahubiri wengi walionyesha shukrani yao kwa ajili ya uchaguzi wa aina ya utoaji mbalimbali unaotolewa na kuonyeshwa kwa njia ya tamasha kwa faida yetu, na zinazoonekana sana zenye kufaa na zenye matokeo. Kitabu Kutoa Sababu Kwa Kutumia Maandiko kinajaa na mawazo yanayoonyesha jinsi ya kutumia sawasawa zaidi ya vichwa vya habari vya lazima 70 vinavyohusiana na Neno la Mungu. Kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele ni muhtasari mfupi wa mafundisho yote ya Biblia ya msingi ambayo wapya wanapaswa kuelewa. Masomo ya 24 na 25 ya Kiongozi cha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi yanatuonyesha jinsi walimu stadi wanavyofanya ili kuongoza, kusoma na kutumikisha sawasawa maandiko ya Biblia. Tungepaswa kufanya matumizi mazuri ya vyombo vyote hivyo tunavyokabidhiwa.
5 Ikiwa tunalitumia sawasawa Neno la Mungu, tutatambua kwamba “liko hai na hukazia nguvu . . . na ni lenye kuweza kufahamu fikira na makusudio ya moyo” ya wale ambao tunahubiria. (Ebr. 4:12, TUM) Matokeo ambayo tutapata kwa kulitumia yatatusukuma kusema ukweli kwa uhodari tena zaidi!—Mdo. 4:31.