Je, Unatetea Neno la Mungu?
1 Katika ulimwengu wa watu ambao mara nyingi wanasema vibaya kuhusu Biblia, Wakristo wa kweli wanatetea kwa bidii Neno la Mungu. Kwa kuwa tunaamini kabisa kwamba “andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu,” tunakubaliana hivyo na Yesu, ambaye katika sala kwa Yehova alishuhudia hivi: “Neno lako ni kweli.” (2 Tim. 3:16; Yoh. 17:17) Namna gani tunaweza kutetea (défendre) Neno la Mungu kwa matokeo zaidi?
2 Jifunze Maandiko: Bila shaka, Yesu alijifunza Neno la Mungu kwa bidii. Hilo lilimwezesha kufundisha mambo yenye kutoka katika Maandiko alipokuwa akihubiri. (Luka 4:16-21; 24:44-46) Tunaweza kufanya nini ili kuchunga maandiko mengi sana akilini mwetu? Tunafanya hivyo kwa kusoma Biblia kila siku na kisha kufikiri sana juu ya andiko ambalo tunaona kuwa ni lenye kutia moyo au linaloweza kusaidia zaidi katika kazi ya kuhubiri. Tunapotayarisha mikutano, tunapaswa kutafuta na kusoma moja kwa moja katika Biblia maandiko yanayotajwa na labda kutayarisha maelezo fulani kuhusu maandiko hayo. Tunapohuzuria mikutano, tunapaswa kufuata katika Biblia zetu wenyewe msemaji anaposoma maandiko. Kujifunza maandiko ya Biblia kutatutayarisha ili ‘tutumie sawasawa neno la kweli.’—2 Tim. 2:15.
3 Acha Biblia Iseme: Tunapohuburi, tunapaswa kuacha Biblia iseme. Kwa mfano, ikiwa hali zinaruhusu, tunapaswa kusoma andiko na kulizungumzia pamoja na msikilizaji. Ikiwa anauliza ulizo au anapinga wazo fulani, ni vizuri kutumia Biblia ili kutoa jibu. Wakati msikilizaji wetu ana kazi nyingi, tunaweza kukazia wazo fulani la Biblia kwa kusema hivi: “Mbele niende, uniruhusu nikusomee andiko hili.” Inapowezekana, soma andiko moja kwa moja katika Biblia, umwonyeshe msikilizaji andiko hilo unapolisoma, yaani asome pamoja nawe.
4 Msikilizaji mmoja alipoonyeshwa maandiko yenye kupinga Utatu, alisema: “Nimekwenda kanisani muda wote wa maisha yangu, hata hivyo sikujua kwamba Biblia inasema hivi!” Mara moja alikubali funzo la Biblia. Yesu alisema kwamba kondoo wake watasikiliza sauti yake. (Yoh. 10:16, 27) Njia nzuri ya kusaidia watu wanyoofu watambue kweli ni kuiona moja kwa moja katika Maandiko. Acheni basi tutetee Neno la Mungu la kweli!