Saidia Musikilizaji Wako Afikiri
1. Ni ufundi gani wa kuhubiri ulio na matokeo mazuri zaidi?
1 Ni ufundi gani wa kuhubiri ulio na matokeo mazuri zaidi? Je, unawaza ni vizuri kushikilia tu wazo lako bila kufikiria maoni ya musikilizaji wako ao ni vizuri kumusaidia afikiri na kisha yeye mwenyewe aone ukweli kuhusu jambo munalozungumuzia? Mutume Paulo alitumia ufundi wa kufikiri pamoja na wasikilizaji wake Wayahudi huko Thesalonike, na ‘wengi kati yao wakawa waamini.’ (Mdo. 17:2-4) Kufikiri pamoja na wengine kunaomba nini?
2. Namna gani tunaweza kuiga mufano wa Paulo tunapohubiria watu habari njema?
2 Fikiria Maoni na Malezi ya Wasikilizaji Wako: Ili kusaidia watu wa eneo lenu wafikiri, unapaswa kufikiria maoni yao. Katika Areopago, Paulo alitolea Wagiriki wasioamini hotuba. Kwa kuwa alifikiria maoni yao, yeye alianza hotuba hiyo kwa kutaja mambo ambayo labda walijua na kuamini. (Mdo. 17:22-31) Kwa hiyo, unapotayarisha jinsi ya kuhubiria watu katika eneo lenu, fikiria maoni yao na mambo wanayoamini. (1 Kor. 9:19-22) Ikiwa musikilizaji anatokeza kizuia-mazungumzo, fikiria mambo ambayo hayatatokeza ubishi, na muzungumuzie mambo hayo.
3. Kwa kutumia maulizo kwa ufundi, namna gani tunaweza kufikiri na wengine kwa matokeo mazuri zaidi?
3 Tumia Maulizo kwa Ufundi: Ili kumutolea mutu anayesafiri maelezo ya kumusaidia afike mahali anapokwenda, ni lazima wewe ujue mahali alipo sasa. Vivyo hivyo, tunapomuhubiria mutu hatuwezi kumusaidia ajue ukweli kuhusu jambo fulani, ikiwa sisi hatujue maoni aliyo nayo kuhusu jambo hilo. Mara nyingi Yesu alikuwa akiuliza maulizo ili ajue maoni ya mutu mbele ya kuanza kufikiri pamoja naye. Kwa mufano, mutu fulani alipomwuliza Yesu, ‘Nifanye nini ili niuriti uzima wa milele?,’ Yesu alitafuta kujua maoni ya mutu huyo mbele ya kujibu. (Luka 10:25-28) Wakati fulani Petro alipotoa jibu lisilofaa, Yesu alitumia maulizo kwa ufundi ili kurekebisha maoni yake. (Mt. 17:24-26) Kwa hiyo, ikiwa musikilizaji anauliza ulizo ao anaeleza maoni yasiyofaa kuhusu jambo fulani, tunaweza kutumia maulizo ili kumusaidia afikiri kuhusu jambo hilo.
4. Kwa nini tunapaswa kujikaza ili kumusaidia musikilizaji wetu afikiri?
4 Tunapomusaidia musikilizaji wetu afikiri, tunamwiga Yesu, Mwalimu Mukuu na wahubiri wengine wenye ufundi, kama vile mitume. Tunaonyesha kwamba tunamuheshimu musikilizaji wetu. (1 Pet. 3:15) Na hilo linaweza kumufanya akubali tumurudilie wakati mwingine.