Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Tuwatolee Watu Kitabu Biblia Inafundisha
Sababu Gani Ni Lazima Kufanya Hivyo: Kitabu Biblia Inafundisha ni chombo cha kwanza kati ya vyombo mbalimbali vya kutusaidia kufundisha watu Biblia. Hata hivyo, tunapaswa kumutolea mutu kwanza kitabu hicho mbele ya kuanza kujifunza naye. Kwa hiyo, tunapaswa kujikaza sana ili kukomalisha ufundi wetu wa kutolea watu kitabu Biblia Inafundisha katika mahubiri. (Met. 22:29) Kuna njia mbalimbali za kuwatolea watu kitabu hicho, na kila muhubiri anapaswa kutumia njia yenye kumuletea matokeo mazuri.
Tumikisha Shauri Hili Katika Mwezi:
Mufanye mazoezi katika ibada yenu ya familia.
Wakati unahubiri, uwaonyeshe wahubiri wengine njia yenye unapanga kutumia. (Met. 27:17) Kama njia hiyo hailete matokeo mazuri, tumia njia ingine.