Jinsi ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia na Watu Tuliotolea Magazeti
1 Kila siku ya Posho, kwa kawaida tunatolea watu magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! katika kazi ya kuhubiri. Hata hivyo, hiyo ni hatua ya kwanza tu katika kutimiza kusudi letu la kufundisha ukweli watu wenye mioyo mizuri. Hapa chini kuna mapendekezo fulani kuhusu jinsi ya kutolea watu kitabu Biblia Inafundisha tunapowarudilia na kuanzisha nao funzo la Biblia. Unaweza kupatanisha mapendekezo hayo na hali ya eneo lenu na kuyatia katika maneno yako mwenyewe. Unaweza kutumia njia nyingine ikiwa ni yenye kukuletea matokeo mazuri.
2 Tumia Kurasa za Utangulizi za Kitabu Biblia Inafundisha: Unaporudilia mtu unaweza kusema hivi: “Magazeti niliyokuachia yanavutia uangalifu kwenye Biblia. Ona kwa nini kusoma Biblia ni kwa maana sana.” Soma Isaya 48:17, 18; Yohana 17:3; au andiko lingine lenye kuonyesha kwa nini kusoma Biblia ni kwa maana. Kisha, baada ya kumwonyesha msikilizaji kitabu Biblia Inafundisha na kumtolea kimoja, unaweza kuendelea kama ifuatavyo:
◼“Biblia inatutolea tumaini la kweli kuhusu wakati ujao.” Onyesha msikilizaji wako ukurasa wa 4-5 na umuulize “Ni ahadi gani kati ya hizi ungependa kuona itimizwe?” Umwonyeshe sura aliyochagua inayozungumzia ahadi inayotolewa na Maandiko na uzungumzie kwa kifupi fungu moja au mafungu mawili ikiwa anaruhusu.
◼Ao unaweza kusema hivi: “Biblia inajibu maulizo ya maana zaidi ambayo tunajiuliza maishani.” Umwonyeshe ukurasa wa 6 na umwulize ikiwa amekwisha kujiuliza ulizo lolote kati ya yale yaliyo chini ya ukurasa. Fungua kitabu kwenye sura inayotoa jibu la ulizo alilochagua na uzungumzie kwa kifupi fungu moja au mafungu mawili.
◼Ao unaweza kumwonyesha mtu sura fulani mbalimbali katika yaliyomo na kumwuliza ni sura gani inayompendeza kati ya hizo. Fungua kitabu kwenye sura aliyochagua na umwonyeshe kwa kifupi jinsi funzo la Biblia linavyofanywa.
3 Umuachie Mutu Ulizo Unapomhubiria kwa Mara ya Kwanza: Unapomhubiria mtu kwa mara ya kwanza, jambo lingine la kufanya ni kutayarisha msikilizaji kwa ajili ya mazungumzo ya wakati ujao. Baada ya msikilizaji kukubali magazeti, tokeza ulizo na umwahidi kwamba utajibu ulizo hilo utakaporudia tena. Jikaze kupanga siku na saa ya kumrudilia na uwe hakika kwamba utatimiza ahadi hiyo. (Mt. 5:37) Unaporudia, kumbusha msikilizaji wako ulizo ambalo ulitokeza mlipokutana kwa mara ya kwanza, na usome na kuzungumzia kwa kifupi jibu linalopatikana katika kitabu Biblia Inafundisha. Umpatie kitabu ili akufuate unaposoma. Tuone mifano michache:
◼Ikiwa gazeti ambalo ulitolea mtu linazungumzia hali za ulimwengu zinazoendelea kuwa mbaya, unaweza kusema hivi: “Wakati ujao tunaweza kuzungumzia jibu ambalo Biblia inatoa kwa ulizo hili, Ni mabadiliko gani ambayo Mungu ataleta duniani?” Tumia ukurasa wa 4-5 unaporudia. Ao unaweza kutokeza ulizo, “Je, misiba inatokea kwa mapenzi ya Mungu?” Unaporudia tena, onyesha msikilizaji wako fungu la 7-8 katika sura ya 1.
◼Ikiwa gazeti ambalo ulitolea mtu linazungumzia familia, mbele ya kuondoka unaweza kutokeza ulizo hili, “Ni kitu gani ambacho kila mshiriki wa familia anaweza kufanya ili maisha ya familia yawe yenye furaha zaidi?” Unapomrudilia, zungumzia fungu la 4 katika sura ya 14.
◼Ikiwa gazeti ambalo ulitolea mtu linazungumzia jinsi Biblia ilivyo yenye kutegemeka, unaweza kutokeza ulizo hili kwa ajili ya mazungumzo yako ya wakati ujao, “Je Biblia inasema kweli kuhusu mambo ya sayansi?” Utakaporudia, zungumzia fungu la 8 katika sura ya 2.
4 Mwishoni mwa kila mazungumzo, tokeza ulizo lingine ambalo utajibu utakaporudia tena. Funzo la Biblia la kawaida litakapokuwa limeanzishwa, chunguzeni kitabu tangu mwanzo mpaka mwisho. Utafanya nini ikiwa msikilizaji wako hakubali kitabu Biblia Inafundisha? Unaweza kuendelea kumletea magazeti na kuzungumzia Maandiko naye. Kadiri unavyokomalisha kupendezwa kwake, anaweza kukubali funzo la Biblia baadaye.
5 Magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yanaweza kuchochea mtu awe na nia ya kujifunza yale ambayo Biblia inafundisha hasa. Kwa hiyo, mjikaze sana kuanzisha mafunzo ya Biblia pamoja na watu wanaokubali magazeti. Kwa njia hiyo, tutatii maagizo ya Yesu ya ‘kufanya wanafunzi na kuwafundisha.’—Mt. 28:19, 20.
[Maulizo ya Funzo]
1. Kusudi letu ni nini tunapotolea watu magazeti?
2. Namna gani tunaweza kutumia kurasa za utangulizi za kitabu Biblia Inafundisha ili kuanzisha funzo la Biblia?
3. Namna gani tunaweza kuanzisha funzo la Biblia baada ya kumtolea mtu magazeti yenye kuzungumzia (a) hali za ulimwengu zinazoendelea kuwa mbaya? (b) familia? (c) jinsi Biblia ilivyo yenye kutegemeka?
4. Tunaweza kufanya nini ikiwa msikilizaji hakubali kitabu Biblia Inafundisha?
5. Kwa nini tunapaswa kujikaza kufanya mengi zaidi ya kuachia tu watu magazeti?