Kuwapelekea Watu Magazeti kwa Ukawaida Ni Njia Nzuri ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia
1. Sababu gani tengenezo la Yehova limetutia moyo tuwapelekee watu wenye kupendezwa magazeti kwa ukawaida?
1 Watu wengi wanakataa kujifunza Biblia, lakini wanafurahia kusoma vichapo vyetu. Kwa hiyo, kwa miaka mingi, tengenezo la Yehova limewatia wahubiri moyo wawapelekee watu wenye kupendezwa magazeti kwa ukawaida. Watu wanaposoma magazeti yetu kwa ukawaida, mara nyingi wanachochewa kujifunza Neno la Mungu. (1 Pet. 2:2) Siku moja, jambo fulani wanalosoma linaweza kuwapendeza, na hivyo kuwachochea waitike funzo la Biblia.
2. Namna gani tunaweza kuchochea kupendezwa kwa wale tunaopelekea magazeti kwa ukawaida?
2 ‘Tia maji’ Mbegu ya Ukweli: Kuliko tu kumuachia mutu gazeti, jaribu kuanzisha mazungumuzo naye, na ufanye urafiki naye. Hilo litakusaidia ujue hali yake, mambo yanayomupendeza, na imani yake. Kujua mambo hayo kutakusaidia useme naye kwa hekima. (Met. 16:23) Ujitayarishe kila mara unapomurudilia. Ikiwezekana, zungumuzia kwa kifupi wazo fulani na andiko fulani linalofaa katika gazeti hilo ili kutia maji mbegu za ukweli katika moyo wake. (1 Kor. 3:6) Kila mara unapomurudilia, andika tarehe, gazeti ulilomuachia, na habari na maandiko ambayo mulizungumuzia.
3. Unaweza kuwarudilia mara ngapi wale unaopelekea magazeti kwa ukawaida?
3 Uwarudilie Mara Ngapi? Unapaswa kuwarudilia mara moja kwa mwezi ili kuwapelekea magazeti mapya. Hata hivyo, kulingana na hali zetu na kupendezwa kwa musikilizaji wetu, tunaweza kumutembelea mara mingi. Kwa mufano, juma moja ao majuma mawili kisha kumuachia magazeti, unaweza kumutembelea na kumuambia: “Nilifika ili kukuelezea kwa muda mufupi jambo fulani katika gazeti nililokuachia.” Kwa kufanya hivyo, utamuchochea atamani kusoma habari fulani katika gazeti. Ikiwa amekwisha kuisoma, unaweza kumuuliza mawazo yake juu ya habari hiyo na kuizungumuzia kwa kifupi. Ao kama mutu huyo ni musomaji wa vichapo vyetu, unaweza kurudi ili kumuonyesha vichapo tunavyowatolea watu mwezi huo, ni kusema, trakte, broshua, ao kitabu.
4. Unaweza kufanya nini Mara kwa mara ili kujua kama wale unaopelekea magazeti kwa ukawaida wanaweza kuitika funzo la Biblia?
4 Usingoje musikilizaji ajiombee funzo la Biblia. Jaribu kuanzisha funzo hata kama hapo mbele hakuitika. Unaweza kumuonyesha mara kwa mara habari “Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa” katika Munara wa Mulinzi ili kuona kama anaweza kuitika muizungumuzie. Pengine unaweza kuanzisha funzo. Hata kama haitike funzo, unaweza kuendelea kumuachia magazeti ili kuchochea kupendezwa kwake.