Sitawisha Kupendezwa kwa Watu Unaowaachia Magazeti kwa Ukawaida
1 Watu wengi tunaokutana nao katika huduma wanakubali ziara zetu na wanapokea kwa furaha vichapo vyetu lakini wanasita kukubali funzo la Biblia la kawaida. Njia moja ya kusitawisha kupendezwa kwao ni kuwaachia magazeti kwa ukawaida. Unapoachia watu magazeti, andika jina na anwani ya mtu, tarehe ya ziara, matoleo yaliyokubaliwa, na andiko lililozungumziwa, pamoja na jambo lolote ulilotambua ambalo linaweza kuonyesha kupendezwa kwa mtu. Kila toleo mpya la magazeti linapofika, tafuta mambo yatakayovutia wale unaoachia magazeti kwa ukawaida, na uyakazie unapowatembelea. (1 Kor. 9:19-23) Baada ya muda, jambo fulani wanalosoma katika magazeti yetu linaweza kuchochea kupendezwa kwao na kuwafanya watake kujifunza mengi zaidi.
2 Hata hivyo, tunatambua kwamba watu wengi zaidi hawatakuwa watumishi wa Yehova kupitia tu usomaji wao wa magazeti. Kwa kuwa ni jambo la haraka kwamba watu wamtafute Yehova sasa, ni jambo gani zaidi tunaloweza kufanya ili kuwasaidia? (Sef. 2:2, 3; Ufu. 14:6, 7) Tunaweza kusitawisha kupendezwa kwao kwa kuwasomea andiko lenye kuchaguliwa kwa uangalifu kila wakati tunapowatolea magazeti.
3 Mazungumzo Yenye Kukazia Andiko Moja: Fikiria wale unaowaachia magazeti kwa ukawaida, na tayarisha mfululizo wa mazungumzo yenye kukazia andiko moja kuhusu mahitaji kamili ya kila mmoja. (Flp. 2:4) Kwa mfano, ikiwa mtu fulani amepoteza hivi karibuni mpendwa katika kifo, unaweza kutumia ziara za kurudia mbalimbali ili kuzungumzia yale Biblia inayosema kuhusu hali ya wafu na tumaini la ufufuo. Habari iliyo katika kitabu Kutoa Sababu chini ya vichwa vikuu “Kifo” na “Ufufuo” inaweza kutumiwa ili kutayarisha mazungumzo hayo yenye kukazia andiko moja. Mazungumzo zaidi juu ya vichwa vyenye kuhusiana na mambo kama vile jinsi ugonjwa, uzee, na kifo vitakavyoondolewa kikamili, yanaweza kufuata bila shaka. Siri ni kupata habari inayopendeza mtu na kumwonyesha hatua kwa hatua yale Biblia inayosema kuhusu habari hiyo.
4 Saidia Wengine Kuelewa: Ingawa kwa kawaida ni vizuri zaidi kufanya mazungumzo kama hayo yawe rahisi na mafupi, mengi yanahitajiwa zaidi ya kusoma tu andiko lililochaguliwa. Shetani amepofusha akili ya watu kuhusu habari njema. (2 Kor. 4:3, 4) Hata wale wanaozoea Biblia wanahitaji msaada ili kuielewa. (Mdo. 8:30, 31) Kwa hiyo, chukua wakati wa kueleza andiko na kutoa mfano ili kulifafanua, kama unavyoweza kufanya katika hotuba kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. (Mdo. 17:3) Hakikisha kwamba mtu anatambua faida ya kutumia Neno la Mungu katika maisha yake.
5 Ikiwa mtu anafurahia mambo anayojifunza, panua mazungumzo hatua kwa hatua ili kutia ndani maandiko ya Biblia mawili au matatu kwenye kila ziara. Tafuta nafasi ya kuanzisha mazungumzo katika broshua Anataka au kitabu Ujuzi. Katika kufanya hivyo, mpango wa kuachia watu magazeti kwa ukawaida unaweza mwishowe kutokeza funzo la Biblia.
[Maulizo ya Funzo]
1. Tunawezaje kutumia mpango wa kuachia watu magazeti kwa ukawaida ili kusitawisha kupendezwa?
2. Kwa nini ni jambo la haraka kwamba watu wamtafute Yehova sasa, na ni jambo gani zaidi tunaloweza kufanya ili kuwasaidia?
3. (a) Tunawezaje kutayarisha mfululizo wa mazungumzo yenye kukazia andiko moja? (b) Ni habari gani zinazohangaisha zaidi watu katika eneo lenu?
4. Kwa nini ni jambo la maana kusaidia wengine waelewe tunapotumia Maandiko, na namna gani tunaweza kufanya hivyo?
5. Namna gani mpango wa kuachia watu magazeti kwa ukawaida unaweza kutokeza funzo la Biblia?