Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kushinda Vizuia-Mazungumuzo
Sababu Gani Ni Lazima Kufanya Hivyo: Wazia unajua kwamba musiba fulani wa asili unakaribia. Watu watakufa ikiwa hawakimbie. Unaenda kwa jirani ili kumujulisha, lakini anakukatiza, na anasema ana kazi mingi. Bila shaka, hautavunjika moyo, utajikaza tu umusadikishe! Watu wengi katika eneo hawatusikilize, hawatambue kwamba ujumbe ambao tunawaletea unaweza kuokoa uzima wao. Pengine tunawatembelea wakati wana kazi mingi. (Mt. 24:37-39) Ao wamedanganywa na habari za uongo juu yetu. (Mt. 11:18, 19) Kwa hiyo, wanaweza kuwaza kama sisi pia tuko sawa na dini ambazo zimetokeza matunda mabaya. (2 Pet. 2:1, 2) Ikiwa musikilizaji hapendezwe, tusivunjike moyo mara moja.
Tumikisha Shauri Hili Katika Mwezi:
Ikiwa musikilizaji anatokeza kizuia-mazungumuzo, kisha kuachana naye, zungumuza na muhubiri mwenzako kuhusu namna mungeshinda kizuia-mazungumuzo hicho kwa njia nzuri zaidi.