‘Tuseme mara moja tulilo nalo!’
1 Je! imekwisha kukufikia kwamba mwenye-nyumba akatize utoaji wako uliotayarishwa kwa makini, akisema: “Unataka nini? Sema mara moja ulilo nalo!” Tunaweza kujifunza nini kutokana na jambo hilo?
2 Watu wengi leo ni wasio wavumilivu. Wanataka kujua sisi ni nani na sababu ya kuwako kwetu mlangoni pao. Wanapotambua kwamba kusudi la ziara yetu ni kuzungumza juu ya Biblia, wanaweza kukataa kusikiliza. Usomaji wa Biblia na mazungumzo ya kiroho si mambo ya maana katika maisha ya watu wengi. Tunawezaje kusadikisha wenye-nyumba kama hao kwamba wangepaswa kuchukua dakika chache ili kuzungumzia habari ya Biblia pamoja nasi?
3 Jambo linalofaa zaidi: Ufunguo ni kuonyesha mwenye-nyumba kwamba Biblia inaandaa utatuzi wenye mafaa wa matatizo yanayomhusu yeye, na kufanya hivyo kwa maneno machache zaidi iwezekanavyo. Utoaji wenye matokeo zaidi huonyesha ulizo la pekee lililotayarishwa ili kufanya mwenye-nyumba afikiri, ulizo hilo likifuatwa na andiko linalolijibu. Mnaweza kufurahia kujaribu baadhi ya madokezo yafuatayo. Yametayarishwa ili kutusaidia ‘tuseme mara moja tulilo nalo’ kwa haraka, huku tukiamsha kupendezwa kwa mwenye-nyumba.
4 Katika eneo ambamo mara nyingi watu husema kwamba hawapendezwi, tokeza ulizo linalowahusu binafsi:
◼ “Kwa kuwa tunakaribia mileani ijayo, je! unajihisi mwenye tumaini au mwenye mashaka? [Acha mtu ajibu.] Biblia ilitabiri matukio yenye kufadhaisha tunayoyaona leo na matokeo yake.” Soma 2 Timotheo 3:1, 2, 5 na Mezali 2:21, 22.
◼ “Katika nchi hii watu huhangaikia sana matunzo ya afya. Je! ulijua kwamba Mungu anaahidi kwamba atatatua matatizo yote ya afya kwa njia yenye kudumu?” Soma Ufunuo 21:3, 4.
◼ “Unafikiri jamii yetu ingefaidikaje ikiwa kila mtu anayeishi hapa angetumia kanuni za Biblia?” Soma Mathayo 22:37-39.
5 Kwa kuwa utume wetu ni kuhubiri habati njema ya Ufalme, popote inapowezekana tungepaswa kuvuta uangalifu juu ya yale ambayo Ufalme utatimiza. Unaweza kusema:
◼ “Je! ulijua kwamba kitabu cha zamani zaidi cha ulimwengu, Biblia, kilitabiri kwamba kutakuwa serikali moja kwa ajili ya ulimwengu wote mzima?” Soma Danieli 2:44.
◼ “Unafikiri hali ingefananaje ikiwa Yesu Kristo angetawala dunia?” Soma Zaburi 72:7, 8.
6 Katika eneo ambamo watu hupenda dini, ungeweza kujaribu moja wa utangulizi ufuatao:
◼ “Watu wengi husumbuliwa na ubaguzi kwa sababu ya kuwa mume au mke, kwa sababu ya dini yao, au rangi yao ya ngozi. Unafikiri Mungu anahisi namna gani kuhusu upendeleo kama huo?” Soma Matendo 10:34, 35.
◼ “Tunajua kwamba Yesu Kristo alifanya miujiza mingi katika siku yake. Ikiwa ungeweza kumwomba afanye muujiza mwingine wa ziada, huo ungekuwa muujiza gani?” Soma Zaburi 72:12-14, 16.
7 Ikiwa mwenye-nyumba anasita kufungua mlango, ungeweza kuanza mazungumzo kwa kusema:
◼ “Watu wengi leo wamechoshwa na kusikia matatizo. Wanataka kusikia utatuzi. Bila shaka, hivyo ndivyo ilivyo kukuhusu wewe. Lakini ni wapi tunapoweza kupata utatuzi wa kweli wa matatizo yetu?” Acha mtu ajibu. Soma 2 Timotheo 3:16, 17.
8 Kwa nini usijaribu hilo? Mara nyingi, ulizo rahisi na fupi hutosha ili kuamsha kupendezwa kwa mwenye-nyumba. Mwanamke mmoja ambaye hapo mbele alipinga alialika dada wawili katika nyumba yake baada ya dada mmoja kumuuliza: “Je! unaweza kutambua ni nini Ufalme wa Mungu ambao wewe huomba katika Sala ya Bwana?” Ulizo hilo lilimfanya mwanamke huyo atake kujua, na alikubali funzo la Biblia. Yeye sasa ni mtumishi wa Yehova aliye wakfu!
9 Unapokuwa ukisema na mwenye-nyumba, uwe mwema katika maneno yako. Uwe mnyonfu. Watu huelekea zaidi kuitikia ifaavyo wanaposadikishwa kwamba tunapendezwa nao.—Mdo. 2:46, 47.
10 Leo, kazi ya kuhubiri habari njema ni mwito wa kushindania. Wenye-nyumba fulani ni wenye mashaka juu ya watu wasiowajua. Wengine wanayo maisha yenye shughuli sana, na wanao wakati mdogo wa kuweka kando. Hata hivyo, tunaweza kuwa hakika kwamba bado kuna watu wengi wenye kustahili ambao tunapaswa kupata. (Mt. 10:11) Jitihada zetu za kuwatafuta huenda zikawa zenye matokeo zaidi ikiwa tunaendelea kufanya utoaji wetu uwe mfupi na ikiwa ‘tunasema mara moja tulilo nalo!’