Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/97 uku. 7
  • Majibu Kwa Maulizo Yenu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Majibu Kwa Maulizo Yenu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 4/97 uku. 7

Majibu Kwa Maulizo Yenu

◼ Wakati kutaniko linapoombwa kutayarisha sherehe za mazishi, inaweza kufikia kwamba maulizo kama haya yatokezwe:

Nani Atakayetoa Hotuba ya Mazishi? Uamuzi huo ungepaswa kuchukuliwa na washiriki wa familia. Inawezekana kwao kuchagua ndugu aliyebatizwa aliye na sifa nzuri. Ikiwa wanaomba msemaji kwenye baraza la wazee, baraza litachagua kwa kawaida mzee mwenye kustahili sana ili kutoa hotuba yenye msingi wa muhtasari wa Sosaiti. Haitakuwa vema kumtukuza mfu, lakini itakuwa vizuri labda kuvutia uangalifu juu ya sifa zenye kielelezo alizokuwa akionyesha.

Je! Tunaweza Kutumia Jumba la Ufalme? Inawezekana ikiwa baraza la wazee linakubali na ikiwa hilo halivurugi programu ya kawaida ya mikutano. Tutaweza kutumia jumba ikiwa mfu alikuwa na sifa nzuri na ikiwa alikuwa mshiriki wa kutaniko, au ikiwa alikuwa mtoto mdogo wa mshiriki wa kutaniko. Ikiwa inajulikana na wote kwamba mtu huyo hakuwa na mwenendo wa Kikristo, au ikiwa kwa sababu nyingine kuna hatari sifa ya kutaniko ichafuliwe, wazee hawataruhusu labda matumizi ya Jumba la Ufalme.​—Ona kitabu Huduma Yetu, uku. 62.

Kwa kawaida, Jumba la Ufalme halitumiwi kwa ajili ya sherehe za mazizi za washiriki wasio Mashahidi wa Yehova wa familia fulani ya Kikristo. Tofauti inaweza kufanywa ikiwa washiriki wa familia ya mfu ni wahubiri wenye kubatizwa wenye kutenda, ikiwa mfu alijulikana vya kutosha na akina ndugu na dada kwa mwelekeo wake mzuri kuhusu ukweli na pia sifa ya mwenendo bora, na ikiwa sherehe haina desturi yoyote ya kilimwengu.

Ikiwa wazee wanakubali kwamba jumba litumiwe, wangepaswa kujiuliza ikiwa ni desturi ya mahali kupeleka sanduku kwa ajili ya sherehe za mazishi. Ikiwa ndivyo, wanaweza kukubali kwamba sanduku ipelekwe katika jumba.

Namna Gani juu ya Sherehe za Mazishi za Watu Ambao si Mashahidi wa Yehova? Ikiwa mtu aliyefariki alikuwa na sifa nzuri katika ujirani wake, inawezekana kwamba ndugu atoe hotuba ya kibiblia yenye kufariji kwenye majengo yaliyoko kwenye makaburi ambako familia ya mfu inakusanyika kabla ya mazishi au kwenye kaburi. Kutaniko halitakubali kushughulika na sherehe za mazishi za mtu aliyejulikana kwa mwenendo wake wa ufisadi au ulio kinyume na sheria, au ambaye mtindo wa maisha ulikuwa kinyume kabisa na kanuni za Biblia. Ndugu hatataka hakika kushirikiana na mwanamemba wa viongozi wa kidini ili kuadhimisha sherehe ya tangamano la kidini au kuongoza sherehe za mazishi katika kanisa la Babuloni Mkuu.

Nini la Kufanya Ikiwa Mfu Alikuwa Mtengwa? Kwa kawaida, kutaniko halitashughulikia sherehe zake za mazishi, na hatungepaswa kutumia Jumba la Ufalme. Ikiwa mtu alikuwa akionyesha wazi toba yake na kuonyesha tamaa yake ya kurudishwa, dhamiri ya ndugu itamruhusu labda kutoa hotuba ya kibiblia kwenye majengo yaliyoko kwenye makaburi ambako watu wa familia wanakusanyika kabla ya mazishi au kwenye kaburi katika kusudi la kutoa ushuhuda kwa wahudhuriaji wasio Mashahidi na kufariji familia. Hata hivyo, kabla ya kuchukua uamuzi huo, ingekuwa hekima kwamba ndugu azungumze jambo hilo na baraza la wazee na kwamba afikirie mapendekezo yao iwezekanavyo. Ikiwa, katika hali fulani, si vizuri ndugu huyo atoe hotuba, labda litakuwa jambo lenye kufaa kwamba ndugu aliye mshiriki wa familia ya mfu atoe hotuba ili kuwafariji watu wa jamaa.

Mtapata miongozo mingine katika namba za Mnara wa Mlinzi wa Oktoba 15, 1990, uku. 30-1; wF81 15/12, kur. 29-30; wF80 15/5 kur. 5-7; wF78 1/9 kur. 5-8; wF77 1/9 kur. 539-40; wF71 1/1 kur. 31-2; na Amkeni! ya Septemba 8, 1990, kur. 22-3; gF77 22/7, kur.  12-15.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine